test
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo MICHEZO. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo MICHEZO. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 15 Februari 2019

Nembo maalum ya mashindano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (AFCON U17) yazinduliwa...Mwakyembe Aifagilia


Nembo maalum ya mashindano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (AFCON U17) imezinduliwa leo  Alhamisi February 14  jijini Dar es Salaam.

Hafla ya uzinduzi wa nembo hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa jijini chini ya Usimamizi wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.


Mwakyembe ameipongeza Nembo hiyo  na kusema kuwa  imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuitangaza Tanzania hasa vivutio vya utalii.

"Nembo hii imebeba vitu vikubwa vitatu katika nchi yetu na mashindano haya. Kwanza imebeba dhana ya utalii. Kivutio chetu kikubwa cha Tanzania Kimataifa ni mlima Kilimanjaro. Tunauona hapa.

Lakini pili imebeba dhana ya uhifadhi. Tumeambiwa kuna pembe ya tembo na ya kifaru. Ambao ni wanyama wetu tunaowahifadhi kwa nguvu zetu zote. Tatu, yote haya yanahusu michezo na ndio maana kuna mpira," alisema Dk Mwakyembe.

Mkurugenzi wa masoko wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Aaron Nyanda alisema kuwa nembo hiyo imechorwa kwa lengo la kuitangaza Tanzania.

"Tulianzisha mchakato kwa watu kubuni nembo ambayo tumeipata hii inayoonyesha vivutio vilivyopo hapa nchini. Na mshindi aliyeshinda atapata fursa ya kwenda nchini Peru ambako kutafanyika Fainali za Dunia kwa vijana wa umri huo iwapo tutafanikiwa kufuzu," alisema Nyanda.

Read More

Jumatano, 13 Februari 2019

Kocha wa zaamani Yanga akubali mziki wa Simba, apagawa na Mkude


Kocha wa zamani wa Yanga Kenny Mwaisabula ‘Mzazi’baada ya Simba kuifunga Al Ahly uwanja wa taifa, ameshangaa ilikuwaje Simba ikafungwa 5-0 na waarabu hao ilipokuwa ugenini.
“Simba wamecheza vizuri, nimekuwa najiuliza maswali mengi ilifungwaje 5-0 kwenye mechi ya awali wakati uwezo wa Al Ahly umeonekana wakawaida sana”-Kenny Mwaisabula.
“Mkude amecheza vizuri, kila aina ya pasi aliyopiga ilikuwa nzuri ni moja kati ya viungo bora katika mechi hii.”
Angalia full video hapa chini #YouTube kwenye channel yangu ya #DaudaTV bofya PLAY▶kuangalia mwanzo mwisho.
Read More

Simba yajipigia tu waarabu taifa


Simba imeibuka na pointi tatu kwa mara nyingine dhidi ya waarabu uwanja wa taifa kwenye michuano ya Caf Champions League hatua ya makundi.

Waarabu wa kwanza kuchezea kichapo cha Simba walikuwa JS Saoura kutoka Algeria ambao walichapwa 3-0 katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi.

Simba sasa imefikisha pointi sita (6) kwenye Kundi C ikiwa nyuma kwa pointi moja dhidi ya Al Ahly ambayo inaongoza kundi hilo kabla ya mchezo wa Saoura vs AS Vita.

Simba imejiweka sehemu nzuri ya kufuzu hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika baada ya ushindi wa leo.

KUNDI C
Kila timu imepoteza walau mchezo mmoja
Simba 3-0 Saoura
AS Vita 5-0 Simba
Al Ahly 5-0 Simba
Simba 1-0 Al Ahly

Al Ahly 2-0 AS Vita
Saoura 1-1 Al Ahly
Al Ahly 5-0 Simba
Simba 1-0 Al Ahly

Al Ahly 2-0 AS Vita
AS Vita 5-0 Simba
AS Vita 2-2 Saoura

Simba 3-0 JS Saoura
JS Saoura 1-1 Al Ahly
AS Vita 2-2 Saoura

Timu zote za Kundi C zimepata matokeo zikiwa kwenye viwanja vya nyumbani, hakuna timu iliyoshinda ikiwa ugenini.
Read More

Jumamosi, 16 Juni 2018

Ratiba Ya Mechi Zote Kombe La Dunia Hadi Fainali


 Fainali za Kombe la Dunia 2018  zilianza rasmini June 14 nchini Urusi ambapo Saud Arabia walitandikwa bao 5-0.

Tazama  hapa  ratiba ya mechi zote za michuanpo hiyo kuanzia ile ya ufunguzi hadi fainali yenyewe.
Read More

Alhamisi, 14 Juni 2018

Michuano ya Kombe la Dunia Kuanza Leo Urusi


Related image
Michuano ya Kombe la Dunia ya Fifa ya mwaka 2018 inaanza leo nchini Urusi ambapo Urusi watacheza dhidi ya Saudi Arabia baada ya kufanyika kwa sherehe ya ufunguzi katika uwanja wa Luzhniki, mjini Moscow.

Mechi hiyo itaanza saa kumi na mbili jioni saa za Afrika Mashariki.

Michuano hiyo itashirikisha mataifa 32, wakiwemo mabingwa watetezi Ujerumani, na itakuwa na mechi 64 zitakazochezwa katika kipindi cha siku 32.

Fainali itachezwa 15 Julai.

Fainali za sasa za Kombe la Dunia ambazo ni za 21 zitachezwa katika viwanja 12 katika miji 11 nchini Urusi, ambayo inapatikana eneo la upana wa maili zaidi 1,800.

Kutokana na hili, kutakuwa na tofauti kubwa katika wakati mechi zinachezwa.

Ujerumani, waliowashinda Argentina katika fainali ya Kombe la Dunia 2014, wanapania kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mtawalia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1962.
Read More

Jumanne, 12 Juni 2018

Orodha yote ya washindi wa tuzo za Mo Simba Awards 2018


Jumatatu usiku  mdhamini mkuu wa Mabingwa wa Ligi Kuu Bara klabu ya Simba SC, Mohammed Dewji aliandaa tuzo maalum ‘Mo Simba Awards 2018’ zilizofanyika Hyatt Regency jijini Dar es salaam kwaajili ya kuwapongeza wachezaji wa klabu hiyo waliofanya vizuri mwaka huu.


WASHINDI WA TUZO ZA MO SIMBA 2018
1.   GOLIKIPA BORA WA MWAKA
A.  Aishi Manula - WINNER
B.  Said Mohamed 'Nduda'
C.   Emmanuel Elias Mseja
2.   BEKI BORA WA MWAKA
A.  Yusuph Mlipili
B.  Erasto Nyoni - WINNER
C.  Shomari Kapombe
3.   KIUNGO BORA WA MWAKA
A.  Jonas Mkude
B.  James Kotei
C.  Shiza Kichuya – WINNER
4.   MSHAMBULIAJI BORA WA MWAKA
A.  Emmanuel Okwi - WINNER
B.  John Bocco
C.  Shiza Kichuya
5.   MCHEZAJI BORA MWANAMKE WA MWAKA
A.  Rukhia Salum
B.  Zainabu Rashidi Pazzi - WINNER
C.  Dotto Makunja
6.   MCHEZAJI BORA MDOGO WA MWAKA
A.  Ally Salim (GK)
B.  Rashid Juma – WINNER
C.  Salumu Shabani
7.   GOLI BORA LA MWAKA
-      John Bocco (Simba VS Mwadui)
8.   TUZO YA BENCHI LA UFUNDI
A.  Pierre Lechantre – Kocha Mkuu
B.  Masoud Djuma – Kocha Msaidizi
C.  Mohamed Aymen – Kocha wa Viungo
D.  Muharam Mohamed – Kipa wa Makipa
E.  Richard Robert – Meneja wa Timu
F.   Yassin Gembe – Daktari wa Timu
G.  Abbas Selemani – Mratibu
9. SHABIKI BORA WA MWAKA
- Fihi Salehe Kambi
10. MHAMASISHAJI BORA WA MWAKA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII
A.  Hamis Mwinjuma (Mwana FA) - WINNER
B.  Salama Jabir – WINNER
C.  Zitto Kabwe
D.  Vyonne Cherrie (Monalisa)
E.  Omary Nyembo (Ommy Dimpoz)
11. MHAMASISHAJI BORA
- Haji Manara
12. TAWI BORA LA MWAKA
A.  Wazo Hill
B.  Ubungo Terminal - WINNER
C.  Vuvuzela
13. KIONGOZI BORA WA MWAKA
          - Kaimu Rais wa klabu ya Simba, Salim Abdallah Muhene
14. TUZO YA WASIMAMIZI WA MCHAKATO WA MABADILIKO

  • A.  Jaji Mstaafu Thomasi Mihayo
  • B.  Wakili Damasi Ndumbaro
  • C.  Abdulrazak Badru 
  • D.  Mussa Hassan Zungu
  • E.  Yusuph Nassoro
  • F.  Brenda Mrema
  • G. Mzee Hamis Boma
  • H.  Revocatus Cosmas Sangu
  • I.    Hashim Nyendage
  • J.   Gervas Alpha Honest
  • K.  Emmanuel Metusela Urembo
  • L.   Mulamu Nghambi
  • M. Selemani Omari
  • N.  Aziz Kifile
  • O. Salim Abdallah Muhene
  • P.  Arnold Kashembe
  • Q. Omari Bakari Mtika
  • R.  Evodius Mtawala

15. TUZO YA HESHIMA (LIFETIME ACHIEVEMENT)
        - Selemani Matola – WINNER
16. MCHEZAJI BORA WA MWAKA
A.  Emmanuel Okwi
B.  John Bocco - WINNER
C.  Shiza Kichuya
Read More

Jumamosi, 9 Juni 2018

Yanga Yaiomba TFF Kujitoa Mashindano ya Kagame CUP


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limethibitisha kupokea barua ya Yanga yenye ombi la kujiondoa kwenye mashindano ya Kagame Cup yanayotarajia kuanza Juni 29 mpaka Julai 13 2018.

Kwa mujibu wa Ofisa wa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, amesema wamepokea barua hiyo inayoeleza kuwa Yanga ina nia ya kuwapa mapumziko wachezaji wake.

Barua hiyo iliyowasili katika makao makuu ya TFF, imesema Yanga inahitaji kuwapa muda wa kupumzika wachezaji wake kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga itakuwa ina kibarua kizito kitakachopigwa nchini Kenya dhidi ya mabingwa wa ligi nchini humo kwa msimu wa 2017/18, Gor Mahia FC Julai 18.

Kutokana na muingiliano wa ratiba hiyo ya Kagame na CAF, Yanga wameona ni vema zaidi kuwapa wachezaji wake mapumziko ili kujiandaa kuelekea mechi hiyo ya kimataifa.
Read More

Jumanne, 5 Juni 2018

Tazama Hapa Ratiba Nzima na Makundi Yote ya Kagame Cup 2018


Wakongwe wa soka Tanzania, Simba SC na Yanga SC wamepangwa Kundi C katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Kagame Cup inayotarajiwa kuanza Juni 28 hadi Julai 13 mwaka huu mjini Dar es Salaam.
 
Akitaja makundi ya michuano hiyo, Katibu wa kudumu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye alisema kwamba pamoja na Simba na Yanga, timu nyingine katika Kundi hilo ni Dakadaha ya Somalia na Saint George ya Ethiopia.
 
Musonye alisema kwamba Kundi A linaundwa na timu za Azam FC, KCCA ya Uganda, JKU ya Zanzibar na Kator FC wa Sudan Kusini, wakati Kundi B linaundwa na timu za Rayon Sport ya Rwanda, Gor Mahia ya Kenya, Lydia Ludic ya Burundi na Ports ya Djibouti. Musonye aliishukuru Tanzania kwa kukubali kuwa wenyeji wa michuano hiyo na akasema kwamba anatarajia itafana kwa sababu ya rekodi ya nchi hii kuandaa mashindano yaliyokuwa na msisimko mkubwa miaka ya nyuma.
 
Musonye ambaye alisema mashindano yatafanyika viwanja vya Taifa na Azam Complex, Chamazi – pia amewapongeza Rwanda na Rais wao, Paul Kagame kwa kuwa wadhamini wa mashindano haya kwa zaidi ya miongo miwili sasa.
 
Musonye amesema kwamba wamelazimika kufanya mashindano ya mwaka huu sambamba na Fainali za Kombe la Dunia nchini Urusi, kwa sababu wasipofanya mwezi huu hayatafanyika tena kwa mwaka wa tatu mfululizo. 
 
Hata hivyo, Musonye amesema kwamba watatoa ratiba nzuri ambayo haitaruhusu mashindano ya mwaka huu kuingiliana na mechi za Kombe la Dunia.  
 
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited, Tido Mhando alisema kwamba wataitumia michuano hiyo kukizindua kituo chao chao Redio, Uhai FM na akawahakikishia kwamba pamoja na mashindano hayo kufanyika sambamba na Kombe la Dunia, lakini yatafana 
 
FIFA imeridhia Kagame kufanyika mwezi huu tofauti na agizo lake la kutotaka katika mwezi wa Fainali za Kombe la Dunia yasifanyike mashindano mengine yoyote, kwa sababu washiriki watano wa michuano hiyo wapo kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Afrika, ambayo kwa sasa imesimama kupisha Kombe la Dunia itarejea Julai baada ya kumalizika kwa michuano hiyo nchini Urusi.
 
Hao ni KCCA ya Uganda iliyopo Kundi A katika Ligi ya Mabingwa Afrika na nyingine nne kwenye Kombe la Shirikisho ambazo ni Gor Mahia ya Kenya, Rayon Sports ya Rwanda, Yanga ya Tanzania zilizopoi Kundi D zote na Al-Hilal ya Sudan iliyopo Kundi A.
 
Na kwa sababu hatua ya makundi ya michuano hiyo ya Afrika itakwenda hadi Agosti, mwezi ambao msimu mpya wa Ligi Kuu nyingi duniani huanza – michuano ya Kagame isipofanyika mwezi huu kuna hatari isifanyike tena na mwaka huu kwa mara ya tatu mfululizo.
 
Azam FC ndiyo mabingwa wa mwisho wa michuano hiyo ilipofanyika Tanzania, walipowafunga Gor Mahia 2-0 katika fainali Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam, mabao ya waliokuwa washambuliaji wake hatari, John Raphael Bocco dakika ya 17 na Muivory Coast, Kipre Herman Tchetche dakika ya 64.
 
Na hiyo ndiyo ilikuwa michuano iliyomtoa mshambuliaji Mkenya, Michael Olunga ambaye kwa sasa anachezea Girona FC ya Hispania kwa mkopo kutoka Guizhou Zhicheng ya China.
 
Baada ya kufungha mabao matano akiwa na Gor Mahia na kuibuka mfungaji bora akiwapiku , Osman Bilal Salaheldin wa Al-Khartoum ya Sudan aliyefunga mabao manne sawa na Tchetche wa Azam FC, Olunga akachukuliwa na Djurgardens IF ya Sweden mwaka 2016 iliyomuuza Guizhou Zhicheng mwaka 2017.
 
Na Tanzania itawakilishwa na Azam FC kama mabingwa watetezi wa mashindano na Yanga SC, kama mabingwa wa nchi.

Credit: Full Shangwe
Read More

Jumatatu, 4 Juni 2018

Simba ‘wanguruma’ kombe la SportPesa Super Cup Kenya, Yanga na JKU wa Zanzibar hoi


Simba
Mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania Simba wametolewa jasho naa Kariobangi Sharks ya Kenya kabla ya kuibuka mshindi kwa mabao 3-2 ya penalti.
Hii ni baada ya sare tasa katika mashindano ya kandanda ya SportPesa Super Cup kwenye uwanja wa Afraha mjini Nakuru eneo la Bonde la Ufa Jumatatu.
Nusra Papa hao wa Kariobangi wameze Simba lakini Jonas Mkude akawapatia mabingwa mara 19 wa ligi kuu ya Tanzania ushindi kwa kufunga bao muhimu lililowawezesha Wekundu wa Msimbazi kufuzu kwa nusu-fainali.
Sasa Simba watakutana na Kakamega Homeboyz ya Kenya Alhamisi wiki hii..

Matokeo ya mechi za sasa

  • Kakamega Homeboyz 3-1 Yanga
  • Gor Mahia 3-0 JKU
  • Simba 3-2 Kariobangi Sharks
Read More

Cristiano Ronaldo Ataka Kurudi Manchester United Kuungana na Mourinho.


Cristiano Ronaldo Ataka Kurudi Manchester United Kuungana na Mourinho.
KOCHA wa zamani wa Real Madrid na England, Fabio Capello amefichua kuwa Cristiano Ronaldo anataka kurudi Manchester United ili aungane na mreno mwenzake Jose Mourinho.

Kitendo cha Zinedine Zidane kuachia ngazi kuinoa Real Madrid kimezua hali ya taharuki ndani ya klabu hiyo, ambapo sasa mustakabali wa nyota wawili wa timu hiyo Ronaldo na Gareth Bale umekuwa suala gumu.

Nyota hao wawili kwa sasa wanahusishwa na kujiunga na Manchester United kwa ajili ya msimu ujao.

Ronaldo alizua mtafaruku baada ya mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Liverpool, ambapo aliwashukuru mashabiki wa Real kwa ushirikiano waliompa kipindi alichokuwa katika timu hiyo akiashiria kama anawaaga.

Kwa miaka mwili sasa kumekuwa kuna uvumi kuwa staa huyo anataka kuihama klabu hiyo akilalamikia ushirikiano finyu kutoka kwa uongozi.

Capello anasema kutokana na Ronaldo na Mourinho kufanya kazi pamoja Real Madrid kuanzia 2010 na 2013 walijenga uelewano mkubwa ukizingatia wote wanatoka Ureno.

“Cristiano anataka kurudi Manchester United ili akafanye kazi na Mourinho,” alisema Capello katika mahojiano na televisheni ya Sky Sport 24.
“Ninadhani hatimaye ataondoka Real Madrid na kurudi zake Manchester United alipotengeneza jina lake,” aliongeza Capello.

Hata hivyo, uamuzi juu ya mustakabali wa Bale na Ronaldo utawekwa bayana baada ya Real Madrid kupata kocha mpya.

Nyota hao wawili walianza kutamba kwenye Ligi Kuu England, ambapo Ronaldo alichezea Manchester United mwaka 2003 hadi 2009 wakati Bale alikuwa Tottenham tangu 2007-2013.

Real Madrid inaendelea na mchakato wa kupata kocha mpya huku kocha wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino akipewa nafasi kubwa ya kukabidhiwa mikoba ya Zidane.
Read More

Ijumaa, 1 Juni 2018

Kinyume na ilivyotegemewa na Wengi...Kocha Zidane Ajiuzulu Real Madrid


HISPANIA: Kocha wa Real Madrid, Mfaransa Zinedine Zidane leo Mei 31, 2018 ametangaza kujiuzulu kufundisha klabu hiyo kwa msimu ujao ikiwa ni siku tano baada ya kuipa ubingwa wa UEFA Champions League mara ya 3 mfululizo.

Zidane anaondoka klabuni hapo kwa heshima baada ya kuitumikia kwa miaka miwili. Mfaransa huyo ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo katika mkutano wake na waandishi wa habari leo.

Mkongwe huyo wa soka mwenye miaka 45, baada ya kutwaa ubingwa wa Uefa ilikuwa inatabiriwa angeongezewa mkataba hadi mwaka 2020. Hata hivyo awali kulikuwa na presha kubwa kutoka uongozi wa Madrid kutokana na kutofanya vyema kwenye La Liga msimu huu ulioisha.

Makocha Arsene Wenger na Antonio Conte ni miongoni mwa wanaotajwa kumrithi Zidane, huku Conte akipewa nafasi kubwa Zaidi.

Zidane alimrithi kocha Rafael Banitez Januari 2016 na msimu huo huo aliipa taji la Ligi ya Mabingwa timu hiyo.

Zidane ameitumikia Madrid tangu (2016-18)
UEFA Champions League🏆🏆🏆
UEFA Super Cup🏆🏆
Club World Cup🏆🏆
Spanish Super Cup🏆
Liga🏆
Read More

BANDA: Nina ofa 15 mkononi



BEKI Mtanzania anayekipiga katika Klabu ya Baroka ya Afrika Kusini, Abdi Banda, ameweka bayana kwamba hadi sasa ana ofa za timu 15 ambazo zinahitaji saini yake baada ya kufanya vizuri katika msimu wake wa kwanza nchini Afrika Kusini.
 
Banda amekuwa na msimu mzuri katika kikosi cha Baroka FC kwa msimu uliomalizika hivi karibuni wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL), ambapo amechangia kwa kiasi kikubwa kuibakisha timu hiyo isishuke daraja.
Beki huyo ndani ya msimu wake wa kwanza akiwa huko amefanikiwa kucheza jumla ya mechi 39 za michuano yote kwa timu hiyo na alichaguliwa mara mbili kuwa mchezaji bora wa timu yake wa mwezi.
Banda amesema timu hizo ni za kutoka ndani na nje ya Afrika Kusini ambazo zinamhitaji baada ya kuonyesha uwezo ndani ya kikosi chake cha Baroka alichojiunga nacho akitokea Simba.
“Hadi sasa kuna timu 15, ambazo zimeonyesha nia ya kunihitaji kwa ajili ya kuzichezea kwa msimu ujao, ambapo mambo yote yanasimamiwa na wakala wangu ambaye ndiye msimamizi wa kila kitu kwangu.
“Zote hizo zimekuja kwa sasa baada ya kuonyesha uwezo nikiwa Baroka FC, ikizingatiwa huu ndiyo kwanza msimu wangu wa kwanza kucheza katika ligi na timu hiyo,” alisema Banda.
Wakala wa Banda, Paul Mitchell, kutoka Kampuni ya Siyavuma Sports Group, alisema: “Banda ni mchezaji mzuri na amekuwa na kiwango kikubwa katika msimu wake wa kwanza akiwa hapa. Ni kweli kuna timu ambazo zimeonyesha nia ya kumtaka kwa ajili ya msimu ujao lakini kwa sasa siwezi kusema ni timu gani hizo.”
Read More

Mo Salah kukosa dakika 90 tu Urusi





STAA wa Misri, Mohamed Salah, atakosa mchezo mmoja tu wa Kombe la Dunia baada ya hapo atakuwa fiti. Salah aliumia bega kwenye mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid baada ya kuumizwa na Sergio Ramos.
Hata hivyo, kulikuwa na hofu kuwa staa huyo atashindwa kucheza fainali hizo lakini sasa imefahamika kuwa atakwenda na kukosa mchezo mmoja tu kwa kuwa kuanzia leo atakuwa nje kwa wiki tatu tu.
Shirikisho la Soka la Misri, limesema kuwa madaktari wanapa-mbana kuhakikisha kuwa mchezaji huyo anakuwa fiti.
Salah anaendelea na matibabu nchini Hispania na ataungana na wenzake hivi karibuni kabla ya safari ya kwenda Urusi kwenye fainali hizo ambazo zitaanza Juni 14.
“Mohamed Salah atakuwa nje kwa wiki tatu, kutokana na jeraha ambalo alilipata kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya nchini Ukraine.
“Atakuwa kwenye Kombe la Dunia, lakini atakosa mchezo dhidi ya Uruguay, ingawa bado juhudi zinaendelea kuhakikisha anakuwa fiti.
“Wakati huu anaendelea na matibabu, atakuwa nje ya kambi ya mazoezi na wenzake,” ilisema taarifa kutoka kwenye shirikisho hilo.
Salah ndiye staa wa Misri baada ya kumaliza msimu akiwa na mabao 44, kwenye klabu yake ya Liverpool na kuibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu England. Misri wapo kundi A, wakiwa na wenyeji Urusi, Saudi Arabia na Uruguay.
Read More

Alhamisi, 31 Mei 2018

Mrisho Ngassa amerudi Yanga


Baada ya kuenea kwa tetesi mbaimbali zikidai kuwa club ya Yanga SC sasa wameyumba kiuchumia kiasi cha kushindwa kufanya usajili wa nafasi tatu za wachezaji watakaoongeza nguvu katika kikosi cha Kombe la shirikisho Afrika.
Jumatano ya May 30 2018 kutoka mtandao wa habari za michezo wa shaffihdauda.com zimeripotiwa taarifa za kufanya usajili wa mshambuliaji wao wa zamani Mrisho Khalfan Ngassa, Yanga imemsajili Mrisho Ngassa kwa ajili ya kuongeza nguvu.
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Mrisho Khalfan Ngassa aliwahi kuichezea Yanga kwa miaka kadhaa kabla ya kuamua kwenda Free State ya Afrika Kusini, Fanja FC ya Oman, Mbeya City ya Mbeya na baadae akajiunga na Ndanda FC kabla ya leo hii kutangazwa kurudi Yanga.
Read More

Mo Salah kushiriki katika kombe la dunia Urusi


Image result for Mo SalahMshambuliaji wa Misri na Liverpool Mohamed Salah ataweza kushiriki katika michuano ya kombe la dunia , tafa lake limetangaza.
Daktari wa timu ya taifa hilo amesema kuwa matibabu ya kiungo huyo wa mashambulizi hayatachukua zaidi ya wiki tatu huku taifa lake likitarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya 

Uruguay mnamo tarehe 15 mwezi Juni.
Salah, 25, alikutana na daktari huyo pamoja na rais wa shirikisho la soka nchini Misri Hany Abu Rida nchini Uhispania siku ya Jumatano.

Shirikisho hilo baadaye lilituma ujumbe wa Twitter likisema: Baada ya kukutana na Abu Rida pamoja na daktari wa timu ya taifa nchini Uhispania leo, Shirikisho la soka linathibitisha kuwa Salah atashiriki katika kombe la dunia, Mungu akipenda.
Awali mshambuliaji huyo hakuwa katika hali ya kuweza kuzungumza zaidi na wanahabari wakati alipowasili nchini Uhispania kwa matibabu ya bega lake.
Mshamuliaji huyo aliyevunja rekodi za ufungaji wa mabao katika klabu yake ya Liverpool alipata jeraha katika mechi ya fainali ya vilabu bingwa ambapo timu yake ililazwa 3-1 na hatimaye mabingwa wa kombe hilo Real Madrid wiki moja iliopita.

Salah alipata jeraha hilo alipokuwa aking'ang'ania mpira na beki wa Real Madrid Sergio Ramos.
Alilazimika kutolewa huku kukiwa na hofu ya iwapo ataweza kuichezea Misri katika fainali za kombe la dunia nchini Urusi mwezi ujao.

Shirikisho la soka nchini Misri FA lilithibitisha siku ya Jumatatu kwamba Salah ataelekea Valencia kwa matibabu ambapo ataandamana na maafisa wa matibabu wa klabu ya Liverpool.

Salah aliwasili mjini humo siku ya Jumanne alfajiri ambapo mwanahabari mmoja wa Uhispania alijaribu kutafuta majibu kuhusu hali yake ,na iwapo ataweza kusafiri kuelekea Urusi na iwapo anamlaumu Ramos kwa jeraha hilo.
Read More

Simba, Azam zaipukutisha yanga



Licha ya ku­maliza msimu kwenye nafasi ya tatu ambayo ni mbaya zaidi kuwahi ku­watokea katika miaka ya hivi karibuni, Yanga im­ekumbana na kasheshe jingine ambalo limefan­ya mambo yao kuwa ma­baya zaidi.


Simba na Azam zimea­mua kuanzia vurugu zake za usajili katika kikosi cha Yanga ambapo zote mbili zimeikomalia kwelikweli huku mastaa wakubwa wa Jangwani wakionekana kupagawa na mafungu waliyowekewa mezani.
 

Usajili rasmi unaanza Juni 15 lakini Simba na Azam zimeanza kuvuna Jangwani. Kwanza Yanga walikuwa wanamtaka Adam Salamba kutoka Lipuli, lakini juzi jioni ali­washangaza wengi baada ya kutua Simba kwa kile kilichodaiwa kuwa Yanga walishindwa kufikia dau linalotakiwa.
 

Simba wamempa Salamba Sh40milioni taslimu na jana Jumanne walimkabidhi gari ya kutembelea aina ya Crown mpya yenye thamani ya zaidi ya Sh15milioni.
 

Kwa mujibu wa gazeti la Championi, limeeleza kuwa linafahamu kuwa wache­zaji muhimu wa Yanga wanaondoka na kujiunga Azam na Simba na kili­chobaki ni ishu ya muda tu kwani wameshashaw­ishika.


Wachezaji wanaotara­jiwa kuondoka ni Papy Kabamba Tshishimbi, Kelvin Yondani, Hassan Kessy na Obrey Chirwa huku Donald Ngoma yeye akiwa ameshasaini Azam, kila mmoja ataondoka kwa dau lake na sababu kubwa ni ukata na maisha magumu ndani ya Yanga ambapo hawapati sapoti yoyote kwa wadau kama awali.
 

Lakini nje ya Yanga Simba wanaweza kuwa­nasa pia, Pascal Wawa na Tafadzwa Kutinyu kutoka Singida United.
 

PAPY TSHISHIMBI:

Huyu bado ana mkata­ba wa mwaka mmoja kwa sasa, lakini Simba wamepa­nia wanamtaka na wana nia kweli, muda wowote unaweza kusikia chochote.
 

“Huwezi kua­mini hata y e y e mwenyewe a n a t o a ushirikiano m k u b w a kwa Simba na hata l e o ( j a n a ) tutawasiliana nae tena,”alisisitiza kiongozi mmoja makini wa Simba.
 

“Huyu Simba wanaweza kuwapa Yanga hata mil­ioni 100,hela ipo sasahivi, Yanga wanatafuta hela ya kusajili,”kiliongeza chanzo chetu cha uhakika.
 

Hata hivyo, imefahamika kuwa mchezaji huyo naye anataka kuondoka kwenye timu hiyo kutokana na hali ya kiuchumi kuwa mbaya hivyo anaweza kuwashawi­shi viongozi wake wakavun­ja mkataba na kujiunga na timu hiyo.
 

Tshishimbi alisaini mkataba wa miaka miwili na sasa amebakiza mwaka mmoja tu na kuna baadhi ya vitu kwenye mkataba wake ambavyo inaelezwa Yanga hawajavitimiza am­bavyo vinaweza kumruhu­su akauvunja mkataba huo.
 

KELVIN YONDANI

Awali ilikuwa inaelezwa kuwa Simba wanamtaka beki huyo lakini kibao kime­badilika na sasa anawe­za kwenda kujiunga na Azam.
 

A n a y e ­t a r a j i w a kuwa ko­cha mpya w a A z a m kuanzia msimu ujao, Hans van Pluijm amepend­e k e z a jina la beki huyo m w e n y e uwezo wa juu kuwa asajiliwe na timu hiyo.
 

H a t a hivyo, haku­na kizuizi chochote kinachom­zuia kwenda kwenye timu hiyo kwa kuwa hadi sasa yeye ni mchezaji huru baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika.
 

HASSAN KESSY

Hakuna aliyekuwa a n a f i k i r i k u h u s u H a s s a n K e s s y k w e n ­d a A z am, l a k i n i m a m ­bo ya­naelezwa kuwa y a m e b a d i l i k a baada ya beki ali­yekuwa anatakiwa na timu hiyo Juma Abdul kugoma kuondoka Yanga, ndiyo wakaweka nguvu kwa Kessy am­baye naye h a n a mk a t a ­ba na timu hiyo ya Jang­wani.
 

Kessy anawadai Yanga na wala hajasaini mkataba hadi sasa, Azam wame­shazungumza naye na kuna uwezekano mkubwa akasaini wiki hii kwa kuwa kila kitu kinaonekana kuwa tayari kukamilika alisema mtu wa karibu na Kessy.
 

PASCAL WAWA

Kwa mashabiki wa soka la Tanzania wanamfahamu beki huyo kisiki raia wa Ivory Coast, lakini habari ya kushtua ni k w a m b a a n a k u j a nchini na k u s a i n i S i m b a mwaka mmoja.
 

Simba wanamtaka Wawa kwa kuwa wanafa­hamu kuwa ana uzoefu wa kimataifa na atawasaidia sana msimu ujao ambao wanaingia kwenye michua­no ya Klabu Bingwa Afrika.
 

Wawa amemalizana na timu yake ya sasa El Mer­reikh ya Sudan na ame­shafanya mazungumzo ya awali na kiongozi mmoja wa Simba na inaelezwa katika mazungumzo yao mchezaji huyo amesema anahitaji mshahara tu kwanza apige kazi bila fed­ha yoyote ya usajili.
 

Inaelezwa kuwa akiwa Sudan alikuwa anaende­lea kuwa mchezaji tege­meo kama wakati akiwa na Azam.
 

TAFADZWA KUTINYU

Habari ny­ingine njema kwa mashabiki wa Azam, ni kwamba klabu yao im­epindua meza na tayari imekamilisha usajili wa kiungo wa Singida United, Mzimbambwe Tafadzwa Kutinyu.
 

Awali uongozi wa Singi­da ulionekana kuweka ngu­mu mchezaji huyo kujiunga na Azam lakini mwenyewe alishinikiza kuwa anata­ka kuondoka na kwenda Azam.
 

Kocha Pluijm al­ishindwa kumshawi­shi kuendelea na timu ya Singida kwa kuwa timu hiyo inashiriki michuano ya kimataifa na hivyo akasema ana­kwenda Azam lakini kwa mzuka wa viongozi wa Azam walionao lolote linaweza kutokea.
 

Siyo kimataifa tu hata fedha kwa kuwa ingekuwa ni hivyo angesubiri Sing­ida wacheze na Mtibwa fainali ya Kombe la FA kwani wangeweza kupa­ta nafasi hiyo lakini yeye alisisitiza kuwa anataka kwenda Azam na inase­mekana amesajiliwa Azam kwa gharama ya dola 20 , kilisema chanzo kutoka Singida.
 

OBREY CHIRWA

S i m b a w a m e ­shasema k u p i t i a msemaji wao Haji Manara kuwa watak­wenda nchini Kenya kwenye mi­chuano ya SportPesa na jina kubwa kwenye mi­c h u a n o hiyo zaidi ya Salamba na taarifa zinasema kuwa wapo ka­ribu sana kumalizana na Chirwa ambaye mambo yake yanasimamiwa na Jo­nas Tiboroha.
 

Habari zinasema kwamba Chirwa anataka kutua Msimbazi na ana na­fasi kubwa ya kumrithi Lau­dit Mavugo ambae bado yupo Sinza, Dar es Salaam anakula bata lakini ame­shapigwa chini.
 

Hata hivyo, inaelezwa kuwa kuna vita kubwa sana kati ya Simba na Azam kuhusu mchezaji huyo.
 

Ofisa Habari wa Simba alisisitiza jana Jumanne kwamba; “Tutalipiza kila aina ya kisasi walichotu­fanyia wakati ule. Kwenye usajili tunafuata maelekezo ya Kocha lakini kuna sehe­mu fulani siasa za usajili zi­naruhusiwa, unachomeka kidogo kumuumiza mtani wako.”
 

“Nakwambia tutashtua, kuna jina moja kubwa tu­nakwenda nalo Nairobi. Nakwambia tutashtua. Hao ambao mmesha­wasikia mpaka sasa ni chamtoto,”alisisitiza Man­ara ambaye amekuwa ni mtu mwenye furaha kwa madai kwamba Yanga iliwazingua sana enzi za Mwenyekiti Yu­suf Manji.
Read More