test

Jumatano, 13 Februari 2019

Simba yajipigia tu waarabu taifa


Simba imeibuka na pointi tatu kwa mara nyingine dhidi ya waarabu uwanja wa taifa kwenye michuano ya Caf Champions League hatua ya makundi.

Waarabu wa kwanza kuchezea kichapo cha Simba walikuwa JS Saoura kutoka Algeria ambao walichapwa 3-0 katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi.

Simba sasa imefikisha pointi sita (6) kwenye Kundi C ikiwa nyuma kwa pointi moja dhidi ya Al Ahly ambayo inaongoza kundi hilo kabla ya mchezo wa Saoura vs AS Vita.

Simba imejiweka sehemu nzuri ya kufuzu hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika baada ya ushindi wa leo.

KUNDI C
Kila timu imepoteza walau mchezo mmoja
Simba 3-0 Saoura
AS Vita 5-0 Simba
Al Ahly 5-0 Simba
Simba 1-0 Al Ahly

Al Ahly 2-0 AS Vita
Saoura 1-1 Al Ahly
Al Ahly 5-0 Simba
Simba 1-0 Al Ahly

Al Ahly 2-0 AS Vita
AS Vita 5-0 Simba
AS Vita 2-2 Saoura

Simba 3-0 JS Saoura
JS Saoura 1-1 Al Ahly
AS Vita 2-2 Saoura

Timu zote za Kundi C zimepata matokeo zikiwa kwenye viwanja vya nyumbani, hakuna timu iliyoshinda ikiwa ugenini.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni