test
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AJIRA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AJIRA. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 2 Novemba 2021

Nafasi Mpya za Kazi 1097 Mamlaka ya Mapato-TRA... Mwisho wa Kutuma Maombi ni Tarehe 4 November 2021


 


 VACANCY ANNOUNCEMENT

 On behalf of Tanzania Revenue Authority (TRA), Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) invites dynamic and suitable qualified Tanzanians to fill 1097 vacant posts mentioned below.

_________________


1. TAX MANAGEMENT OFFICER II -   NAFASI  294

2. TAX MANAGEMENT ASSISTANT II -NAFASI  326
 
3.CUSTOMS OFFICER II -  NAFASI 167

4.CUSTOMS ASSISTANT II NAFASI 114

5.PUBLIC RELATION OFFICER II – NAFASI  3

6. ICT TECHNICIAN II – NAFASI 30


7. ICT OFFICER II (COMPUTER SYSTEMS ANALYSIS AND DEVELOPMENT) - NAFASI 31.

8. ICT OFFICER II (NETWORK ADMINISTRATOR) –NAFASI  2 

________
 
 ๐Ÿ‘‰Kujua zaidi pamoja na kutuma Maombi <<BOFYA HAPA>>

9. ICT OFFICER II (DATABASE ADMINISTRATION) - NAFAS 6 .

10. ICT OFFICER II (ICT SYSTEMS RISKS AND SECURITY) – NAFASI 6.

11. ICT OFFICER II (COMPUTER/BUSINESS APPLICATION SUPPORT) –NAFASI 6.

12. ICT OFFICER II (COMPUTER SYSTEM ADMINISTRATION) NAFASI 19.

13. ICT OFFICER II (BUSINESS ANALYST) COMPUTER SYSTEMS ANALYSIS AND DEVELOPMENT– 1 POST

14. ICT OFFICER II (BUSINESS ANALYST) DATABASE ADMINISTRATION – NAFASI 1.

15.  ICT OFFICER II (BUSINESS ANALYST) SYSTEMS RISKS AND SECURITY-  NAFASI 1 .

16. RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT II - NAFASI 18.

17. DRIVER II  NAFASI 59 .

18.  LEGAL COUNSEL - NAFASI 3

19 RATING IINAFASI 1 .

20.ACCOUNTS ASSISTANT II-  NAFASI 4 .

21. PERSONAL SECRETARY IINAFASI 5.

___________________

 Mwisho wa kutuma maombi ni - 4th November, 2021 

 ๐Ÿ‘‰Kujua zaidi pamoja na kutuma Maombi <<BOFYA HAPA>>

๐Ÿ‘‰Kupata nafasi mbalimbali za kazi Serikalini na mashirika binafsi <<BOFYA HAPA>>
Read More

Jumamosi, 19 Mei 2018

EMPLOYMENT OPPORTUNITY NACTE


NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
EMPLOYMENT OPPORTUNITY
National Council for Technical Education (NACTE) was established by the National Council for Technical Education Act, Cap. 129 (No. 9 of 1997). The Council is a body corporate with a legal mandate of coordinating provision of technical education and training.
Read More

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo


Alhamisi, 13 Julai 2017

Serikali Yatangaza Ajira Mpya 10, 184 Kuziba Mapengo ya Waliogushi Vyeti


Ofisi  ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza kutoa vibali vya ajira 10,184 ili kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, imefahamika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais, Utumishi, Florence Temba, ilieleza kuwa agizo hilo linazihusu Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala wa Serikali, pamoja na Taasisi na Mashirika ya Umma.

Ilimnukuu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki akitoa agizo hilo wakati akizungumza katika kikao kazi na watumishi wa Umma wa Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam jana.

“Mgawanyo wa vibali vya ajira umezingatia upungufu uliojitokeza baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki, vipaumbele vya Taifa kwa sasa na upatikanaji wa watumishi kutoka katika soko la ajira,” alisema Kairuki.

Kairuki aliongeza kuwa taratibu za kukamilisha mgawo wa nafasi za ajira 4,816 zilizosalia unaendelea ili kuwezesha wizara na taasisi nyingine zilizokamilisha uhakiki wa watumishi wa umma hivi karibuni kuajiri watumishi wapya kuziba nafasi wazi zilizojitokeza.

Alieleza kuwa serikali imetoa kibali kuajiri watumishi wapya 15,000 ili kuziba pengo lililosababishwa na kuondolewa kwenye orodha ya malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti baada ya zoezi la uhakiki.

“Watumishi wa umma watakaoajiriwa kuziba nafasi hizo wanatarajiwa kuripoti kazini kuanzia mwezi Agosti, 2017,” alieleza Waziri Kairuki, na kuongeza kuwa utaratibu wa ajira mpya za serikali upo palepale na amewataka wananchi kutokuwa na wasiwasi wowote wa ajira hizo.

“Napenda kusisitiza kuwa vibali tulivyovitoa leo ni vile vilivyoziba pengo la walioghushi vyeti, naomba wananchi watambue kuwa suala la ajira mpya bado liko pale pale kama serikali ilivyojipanga,” alisema Kairuki.

Aprili mwaka huu, Rais John Magufuli alipokea ripoti yenye orodha ya watumishi wa umma ambao kati yao wanadaiwa kuwa na vyeti pungufu, vyenye utata na vya kughushi kutokea kwa Waziri Kairuki.

Waliokuwa na vyeti vya kughushi walikuwa 9,932, na Rais aliapa kwamba hawatarudi kazini. Rais Magufuli aliagiza kufutwa kazi kwa wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo na kuzuia mishahara yao ya mwezi huo, lakini hata hivyo bado mlango uliwekwa wazi kwa wenye pingamizi na wapo waliokataa rufaa huku wengine wakienda kwenye mamlaka husika kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.

Wiki iliyopita akiwa Dodoma, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk Laurean Ndumbaro alitangaza kuwa wiki hii serikali itatoa vibali 3,000 vya ajira katika sekta ya afya vikiwemo vya madaktari na wauguzi pamoja na maofisa hesabu 535 kwa ajili ya vituo vya afya vya kata ili washughulike na ukusanyaji wa mapato kwenye vituo vya afya na zahanati.
Read More

Alhamisi, 29 Juni 2017

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Wahitimu Wa Stashahada Katika Programu Mbalimbali Wanaokusudia Kuomba Kujiendeleza Katika Ngazi Ya Shahada Katika Vyuo Vya Elimu Ya Juu Kwa Mwaka Wa Masomo 2017/2018


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ni chombo kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge, Sura 129, ili kusimamia na kuratibu utoaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini. 
Jukumu kubwa la Baraza ni kuendeleza na kuinua ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi nchini kwa kusimamia kikamilifu shughuli za usajili na ithibati, mitaala na upimaji ili tuzo zitolewazo na vyuo/taasisi ziwe na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa. 
Kifungu cha 5 (1) (e) na (f) cha Sheria hii kinaipa mamlaka NACTE, kuanzisha tuzo mbalimbali zinazotolewa na kuhakikisha kuwa ubora wa elimu na mafunzo ya kada ya kati yatolewayo na taasisi mbalimbali yanazingatia ubora unaokusudiwa. 
Aidha, Kifungu cha 11, kinalitaka Baraza kuhakikisha kuwa Tuzo zitolewazo na vyuo na taasisi zote zinazoendesha mafunzo ya kada ya kati zinatambuliwa na mamlaka husika. Katika muktadha huu, kila chuo/taasisi inayotoa elimu ya ufundi inatakiwa kuwasilisha Baraza matokeo ya mitihani kila mwisho wa semista.

Hivyo, kwa kuwa Udahili na uchaguzi wa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya Shahada mbalimbali yanayotolewa na taasisi/vyuo vyote hapa nchini, utafanyika moja kwa moja vyuoni, Baraza linao wajibu wa kuziwezesha taasisi/vyuo hivyo kudahili wanafunzi wenye sifa stahiki.

Ili kulifanikisha hili, Baraza limeandaa mfumo ambao taasisi/chuo kitapata taarifa za muombaji mwenye sifa linganifu (muhitimu wa Stashahada) moja kwa moja.

Hivyo, wahitimu wote wa Stashahada yoyote wanaokusudia kuomba kujiendeleza katika ngazi ya Shahada wanatakiwa kuhakiki taarifa zao Baraza (NACTE) kabla ya kufanya maombi yao kwenye taasisi/vyuo wanavyotaka kwenda kusoma. 
Uhakiki huo utafanywa kwa njia ya mtandao (online) kupitia Mfumo wa Uhakiki wa Tuzo (NACTE Award Verification System - NAVS) kwa kubofya hapa au kupiti tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz) kwa kubofya kitufe kilicho andikwa Award Verification. 
Baada ya kuhakiki taarifa zake kuwa kamilifu na sahihi, mhakiki atapatiwa Namba ya Utambulisho (Award Verification Number - AVN) ambayo itaambatanishwa na maombi ya Udahili kwenye taasisi/chuo husika. 
Utambulisho huo utatumiwa na taasisi/chuo kujiridhisha kwamba taarifa alizowasilisha muombaji wa Udahili ni sahihi na hivyo kuweza kudahiliwa na kisha kuchaguliwa kwa ajili ya masomo kulingana na mahitaji ya taasisi/chuo husika.

Aidha, Baraza linapenda pia kuwafahamisha wale wote walio na Stashahada walizopata nje ya nchi (Foreign Diploma Awards), nao waziwasilishe kupitia mfumo huu (NAVS) kwa ajili ya kuzifanyia ulinganifu na kuweka taarifa zao kwenye Kanzidata ya Baraza ili nao waweze kupata Namba ya Utambulisho. Maelezo ya namna ya kuziwasilisha tuzo za kufanyiwa ulinganifu yanapatika kwenye tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz).

Ili mwombaji Udahili apate Namba ya Utambulisho atalipa Shilingi Elfu Kumi (10,000/=) kwa njia ya mtandao (Online) kwa kufuata maelekezo yaliyopo kwenye Mfumo wa Uhakiki wa Tuzo - NAVS.  
Kwa wale wanaotaka kufanya ulinganifu wa vyeti vyao, watatakiwa kulipa Shilingi Elfu Ishirini (20,000/=) kwa tuzo za ndani ambazo hazisimamiwi na baraza, na Shilingi Elfu Hamsini (50,000/=) kwa tuzo za nje ya nchi (foreign awards).

Baraza linapenda kuwafahamisha wahitimu wa Stashahada wanaotaka kujiendeleza katika ngazi ya Shahada kuwa wanaweza kufanya uhakiki huo kuanzia leo tarehe 28 Juni, 2017 hadi tarehe 20 Julai, 2017.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE: 28/06/2017
Read More

Jumamosi, 24 Juni 2017

Serikali yatoa kibali cha kuajiri watumishi 535


Read More

Jumanne, 13 Juni 2017

BREAKING NEWS: TAARIFA KWA UMMA JKT IMEONGEZA ORODHA YA MAJINA YA VIJANA WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA MEI 2017 KWA AJILI YA KUHUDHURIA MAFUNZO YA MUJIBU WA SHERIA MWAKA 2017




TAARIFA KWA UMMA
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), linapenda kuutaarifu umma kuwa limeongeza majina ya vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwezi Mei 2017 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria.
Vijana hao wanatakiwa kuripoti kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa kuanzia tarehe 13 Juni 2017 hadi tarehe 20 Juni 2017.
Read More

Ijumaa, 19 Mei 2017

AJIRA MPYA:Nafasi 145 Za Ajira Zatangazwa Nchini


Read More

Jumanne, 31 Januari 2017

Breaking News: Mtokeo ya Kidato cha Nne 2016 Yametoka......Bofya Hapa Kuyatazama


Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ambapo umefaulu wa jumla umeongezeka kwa 2.56% kutoka 67.53% mwaka 2015 hadi 70.09% mwaka 2016.

Katibu Mtendaji wa barza hilo, Dkt Charles Msonde amesema kati ya wanafunzi 408,372 waliofanya mtihani, jumla ya wanafunzi 277,283 wamefaulu, wakiwemo wasichana 135,859 sawa na asilimia 67.06 na wavulana 141,424 sawa na asilimia 73.26.

Kwa upande wa watahiniwa wa shule, Dkt Msonde amesema kuwa 244,762 sawa na asilimia 70.35 ya waliofanya matihani wamefaulu ikilinganishwa na wanafunzi 240,996 sawa na asilimia 67.91 waliofaulu mwaka 2015.

Kwa upande wa ubora wa ufaulu, amesema watahiniwa wa shule wenye ufaulu mzuri wa Daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60
Read More

Wanafunzi 10 Waliofanya Vizuri Zaidi Kitaifa Katika Matokeo Ya Kidato cha Nne 2016


Read More

Shule 10 Bora na 10 za Mwisho katika Matokeo Kidato cha Nne 2016


Leo January 31 2017 Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza matokeo ya kidato cha nne ‘CSEE 2016’.

Hapo chini kuna orodha ya shule 10  bora kitaifa na shule 10 zilizoshika mkia
Read More

Jumatatu, 16 Januari 2017

MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2016


MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2016


Matokeo ya Kidato cha Pili Yatangazwa....... St. Franscis, Kilimanjaro Islamic na Kaizerege Zaongoza


Baraza la Mitihani nchini – NECTA limetoa matokeo ya mitihani ya upimaji kwa wanafunzi wa darasa la nne kwa shule zote za msingi nchini pamoja na ule wa kidato cha pili kwa wanafunzi wa shule za sekondari yanayoonesha ufaulu kuongezeka kwa 1.9%.

Katibu Mtendaji wa Baraza lza Mitihani nchini Dkt Charles Msonde ndiye aliyetoa taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo katika hali isiyo ya kawaida, shule tisa kati ya kumi zilizofanya vibaya katika mtihani wa kidato cha pili nchini, zimetoka mkoani Mtwara kama zinavyoonekana hapa

Amesema ufaulu umeongezeka kwa asilimia 1.9 kutoka 89.12% mwaka 2015 hadi kufikia 91.02% mwaka 2016 ambapo wanafunzi 372,228 wamepata alama zinazowawezesha kuingia kidato cha tatu huku wanafunzi 36,737 wakishindwa kufikisha alama hizo.

Shule ya St. Francis Girls ya Mbeya imeongoza katika shule 10 bora kitaifa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha pili mwaka 2016

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, idadi ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa madaraja ya I, II, na III ni 178,115 sawa na asilimia 43.55

Kuhusu ufaulu wa masomo, amesema, katika masomo ya Civics, History, Geography, Kiswahili, Phiysics, Chemistry, Chemistry, Biology na Basic Mathematics umepanda ikilinganishwa na mwaka 2015.

Aidha ufaulu kwa somo la English Language pekee ndio ambao umeshuka ikilinganishwa na mwaka 2015.

Somo lililofanyika vizuri zaidi ni Kiswahili ambapo asilimia 90.06 ya wanafunzi wote, wamefaulu na soko lenye ufaulu wa chini zaidi ni Basic Mathematics ambapo asilimia 21.55 wamefaulu.

Mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi ni Teckla Erasmo Haule kutoka Canosa ya Dar es Salaam akifuatiwa na Joseph Fabian Kalabwe wa Kwema Modern ya Shinyanga na Mirable Rayner Matowo wa Canosa ya Dar es Salaam.

Katika wanafunzi 10 bora kitaifa, wanafunzi 9 ni wasichana, na watano kati yao wanatoka Feza Girls.

Matokeo ya wanafunzi 31 yamefutwa baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu
.
******
Read More

Jumanne, 13 Desemba 2016

TANGAZO KWA UMMA – AJIRA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI KWA SHULE ZA SEKONDARI



Serikali inatarajia kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati kwa shule za sekondari.
Ajira hii ni kwa walimu wa stashahada na shahada za mafunzo ya ualimu wa masomo ya hisabati na sayansi, waliohitimu mwaka 2015.  wahitimu hao wanatakiwa kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari (kidato cha nne na sita) na taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.
Nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara info@moe.go.tz kuanzia tarehe ya tangazo hili hadi ijumaa tarehe 16/12/2016.
yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa hatafikiriwa katika uajiri.
Tangazo hili linapatikana pia kwenye tovuti za ofisi zifuatazo: OR-TAMISEMI, NECTA, TCU na NACTE.

imetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
Read More

Alhamisi, 20 Oktoba 2016

MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA THIRD ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017



Habari yako,

Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa 


mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa na joining instructions za  kujiunga na vyuo vikuu 2016/2017 THIRD  ROUND





CHUO KIKUU MOUNT MERU                (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU SEKOMU                           (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU TIA-DAR                            (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU IRINGA UNIVERSITY      (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU AJUCO-SONGEA               (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU HURBERT KAIRUKI        (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU NIT                                       (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU ATC ARUSHA                    (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU MUST-MBEYA                   (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU AMUCTA                           (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU MARIAN                           (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU ST.JOHN DODOMA        (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<

CHUO KIKUU MOUNT MERU               (3RD ROUND)  >>BONYEZA HAPA<<
Read More