test

Jumapili, 25 Juni 2017

Mwigulu Nchemba Atoa ONYO Kali Kwa Wanaompinga Rais Sakata la Wanafunzi Kupewa Mimba


Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amezionya taasisi zisizo za Serikali zinazohamasisha kudai haki ya mtoto anayepata mimba kurejeshwa shuleni kuacha mara moja na zikiendelea atazifutia usajili.

Mwigulu ameyasema hayo leo, Jumapili wakati alipomwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika harambee ya kuchangia ujenzi wa Parokia ya Kisasa Mjini hapa.

Amesema Serikali haitaomba ushauri wala maoni kwa sababu maelezo yaliyotolewa na Rais, John Magufuli ni maagizo ya Serikali.

Waziri huyo amesema Serikali imetoa haki ya kila mtoto kupata elimu kwa kuifanya kuwa bure kwa hiyo atakayeikosa asitafute kisingizio.

"Rais ametoa haki hiyo sasa hivi elimu ni bure, halipi tuition wala nini, atakayeamua kuachana na haki hiyo asitafute kisingizio, asipeleke lawama kwa Serikali, "amesema.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

Maoni 1 :

  1. Loooo!!! Uhuru wa kufikiri na kutafakari kwa kina na kutofautiana na mtu YEYOTE na hatimaye kuwa na Naomi yako binafsi Uko wapi??

    JibuFuta