test

Jumanne, 29 Mei 2018

Mpoki apewa shavu na Alikiba


 Katika kuelekea mchezo maalumu wa hisani ya kuchangia elimu, msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba ametangaza kikosi cha wachezaji watakao kuwa upande wake kupambana dhidi ya  kikosi cha wachezaji watakaokuwa upande wa mshambuliaji wa timu ya Taifa na klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta.

Kwenye kikosi hicho, Alikiba amemchukua mshambuliaji hatari wa klabu ya Simba, Emmanuel Okwi na wachezaji wengine kama John Bocco, Msuva, Erasto Nyoni, Abdu Kiba na wengineo kama inavyoonesha hapa chini kwenye picha.

Kikubwa zaidi ni kwamba Alikiba amemchagua mchekeshaji maarufu nchini Tanania, Mpoki kuwa msemaji wa timu yake aliyoichagua.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mnamo Juni 9, 2018 .

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni