test

Jumatatu, 15 Mei 2017

Machinjio Yafungwa kwa Uchafu


Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeyafunga nusu ya machinjio ya ng’ombe, kuku na nguruwe katika Manispaa za Temeke, Ilala, Ubungo na Kinondoni baada ya kufanya ukaguzi.

Mkurugenzi wa TFDA, Hiiti Sillo alisema kuwa ukaguzi huo uliofanyika katika machinjio 55 kwa kushirikiana na Bodi ya Nyama, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na Maofisa Afya na mifugo, umebaini 26 yamekiuka kanuni na sheria, hivyo kuyafunga.

“Lengo la ukaguzi ilikuwa kuangalia utekelezaji wa Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Sura ya 219, hususan kukagua majengo, miundombinu, mfumo wa uchinjaji na uendeshaji wa machinjio kama unazingatia kanuni”, alisema Sillo.

Alitaja sababu za kufungwa kwa machinjio hayo kuwa ni kutokuwa na majengo ya kudumu miundombinu isiyofaa, uchinjaji usiozingatia kanuni, ukiukwaji wa sheria za kuendeshea machinjio na uchafu ndani na nje ya machinjio.

Meneja wa TFDA Kanda ya Mashariki, Emmanuel Alphonce, alisema barua zimeandaliwa ili kupelekwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwaajili ya machinjio ya Vingunguti na uongozi wa Mazizini, baada ya TFDA kutoa siku saba kwa uongozi wa machinjio hizo, kufanya marekebisho ya upungufu uliobainika ambao ni uuzwaji wa nyama ndani ya machinjio na uingiaji wa watu wasiohusika.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni