test

Jumapili, 13 Septemba 2015

UKAWA kutumia rasilimali za ndani ya nchi kumalaiza matatizo ya watanzania


 
Mgombea urais wa vyama vinavyounda UKAWA Mh.Edward Lowassa amesema   akichaguliwa kuwa rais hatakuwa na sababu ya kutegemea misaada kutoka nje  kutekeleza ahadi anazotoa na sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWa badala yake  atasimamia vizuri rasilimali zilizopo kwani zinatosha kutatua matatizo ya  watanzania.
Baada ya kumaliza kazi ya kufikisha ujumbe wa mabadiliko kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma ambao ni ngome na pia  makao  makuu ya CCM kwa mafanikio makubwa  Mh.Lowasa anaingia kwa kishindo katika mkoa wa Singida na  kupokelewa na   umati wa wananchi wakiwa na matumaini makubwa ya kupata mabadiliko ya maisha yao kupitia ukawa chini ya Mh.Lowasa,ambaye amewaomba kumpa nafasi ya kushughulikia kero  zao kwani anazijua  na  asilimia kubwa ufumbuzi  wake  uko  ndani ya uwezo wake.
 
Mh.Lowasa ambaye awali amefanya mikutano katika wilaya ya Manyoni,Ikungi na Singida mjini anasema kupitia sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWA na uwezo mkubwa wa viongozi na watendaji wana kila  sababu ya kubadilisha maisha ya watanzania kwa muda mfupi  na kwa ufanisi mkubwa.
 
Baadhi ya wananchi na viongozi wanaounga mkono mabadiliko wamesema ubora wa sera zilizoko kwenye ilani ya UKAWA kugusa matatizo ya watanzania,UKAWA inaendelea kuwa kimbilio la,wananchi na viongozi wakiwemo wanaotoka CCM huku  wakiendelea kuwaeleza wananchi faida za kubadilika na athari za kuendelea kuvumilia mateso ya CCM na ahadi zinazoonekana wazi kuwa hazitekelezeki.
 

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni