test

Jumapili, 13 Septemba 2015

Rais Kikwete aagiza idara ya mambo ya kale kuhifadhi eneo la Laitoli.


 
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dakta Jakaya Mrisho Kikwete ameiagiza idara ya mambo ya kale kushirikiana na mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kuhakikisha kuwa eneo la laitoli zinapopatikana nyayo za mtu wa kale anayesadikiwa kuwa binadamu wa kwanza linahifadhiwa kitaalamu .
Dakta Kikwete anatoa agizo hilo jijini Arusha katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la jengo la kitega uchumi la mamlaka ya hifadhi Ngorongoro na kuongeza kuwa hifadhi ya eneo hilo itaongeza idadi ya watalii wanaoingia kuona maajabu ya Ngorngoro.
 
Awali akioa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo linalokadiriwa kuwa na ghorofa kumi na tano,mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya Ngorongoro balozi Mwanaidi Maajar aamesema lengo la ujenzi wa kitega uchumi hicho ni kuiwezesha mamlaka kuongeza vyanzo vya mapato nje ya mapato yatokanayo na utalii. 
 
Na hatimaye bodi ya mamlaka ya Ngorongoro na baraza la wafugaji wakatumia fursa hiyo kumuaga rasmi rais Kikwete kwa kumpatia zawadi mbalimbali kikiwemo cheti cha kutambua mchango wake kwenye kutangaza utalii.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni