Baada
ya muigizaji Wema Sepetu kuachia filamu yake ya Heaven Sent, 2017 na
kushinda tuzo, amefunguka kipi kinafuata kutoka kwake.
Mrembo
huyo amesema kwa kushirikiana na timu yake kuna movie wanaandaa ambayo
itakuja kubadili tasnia nzima, pia kuna event nyingine kubwa atafanya
June mwaka huu.
“Heaven
Sent imekuja imeshinda tuzo, so it good thing, tutegemee vitu vikubwa
kama nilivyosema hapo awali kuna kitu kitatokea June kwa hiyo tukae mkao
wa kula kitu kizuri kinakuja nadhani kitabadilisha tasnia ya filamu as a
all, kuna project za kutikisa mji,” Amesema Wema Sepetu.
Usiku
wa April 01, 2018 filamu ya Heaven Sent ilimfanya Wema Sepetu kuwa
mshindi wa tuzo mbili za Sinema Zetu International Film Festival Awards
(SZIFF).
0 comments:
Chapisha Maoni