Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka katika kesi
inayowakabili vigogo wawili wa uthamini wa madini ya almasi wa Serikali,
kwamba kufikia Mei 21, 2018 watoe majibu sahihi kuhusu ulipofikia
upelelezi wa kesi hiyo.
Hakimu
Mkazi Mkuu, Wilbrad Mashauri ameeleza hayo jana Jumatatu Mei 7, 2018
muda mfupi baada ya wakili wa Serikali, Saada Mohammed kueleza kuwa
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba jalada lipo kwa
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).
Baada
ya Saada kueleza hayo, wakili wa utetezi Nickson Ludovick alidai
walitegemea upande wa mashtaka wangeiambia mahakama ni lini wataendelea
na kesi hiyo kwa sababu walishasema upelelezi umekamilika.
Aliiomba
mahakama imwamuru Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kueleza ni lini kesi
itaendelea kwa sababu katika kumbukumbu za mahakama zilizopo,
zinaonyesha kesi ilishakuwa tayari kwa kuanza kusikilizwa.
Akijibu
hoja hiyo, wakili wa Serikali Elia Athanas alidai jalada bado
linashughulikiwa katika sehemu ambazo hazipo sawa na hakuna uzembe
wowote unaofanywa na ofisi ya DPP.
Baada
ya kutolewa kwa hoja hizo, Mashauri aliamuru upande wa mashtaka Mei 21,
2018 kuja na majibu sahihi kuhusu hatua ya upelelezi ilipofikia.
Washtakiwa
wanaokabiliwa katika kesi hiyo ni Mkurugenzi wa Uthaminishaji Almasi na
Vito Tanzania (Tansort), Archard Kalugendo na mthamini almasi wa
Serikali, Edward Rweyemamu.
Washtakiwa hao wanasota mahabusu kutokana na DPP kuzuia dhamana zao.
Kwa pamoja wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wakidaiwa kuisababishia Serikali hasara ya Sh2.4 bilioni.
0 comments:
Chapisha Maoni