test

Jumanne, 8 Mei 2018

Polisi yawasaka walinzi wa mahakama Iliyowaka Moto Mbeya


Polisi imesema hadi sasa haijajua chanzo cha kuteketea kwa moja jengo la Mahakama ya Mwanzo Uyole jijini hapa na kwamba, inaendelea kuwasaka walinzi wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mussa Taibu alisema kwamba jengo la mahakama hiyo na mali zote zilizokuwamo ndani, ziliteketea saa tatu usiku wa kuamkia juzi.

‘Tulipata taarifa kwamba mahakama inaungua tuliwataarifu wenzetu wa zimamoto, lakini wote tulikuta jengo limeshateketea na nyaraka zote zikiwamo pikipiki mbili ambazo zilikuwa ni kielelezo katika moja ya kesi,” alisema Taibu na kuongeza:

“Baada ya kukuta hali hiyo tulijiuliza maswali kadhaa imekuaje. Je, mahakama ile ina walinzi, tukaambiwa inao, bahati mbaya walinzi hawakuwapo wakati huo na hatujui walikwenda wapi?”

Alisema hawajajua chanzo cha tukio hilo hivyo jitihada zinaendelea ikiwamo kuwasaka walinzi hao.

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Moses Mwidete alisema hakuna kilichookolewa kwa kuwa inaonyesha wakati moto huo unazuka hapakuwapo na mtu yeyote, hivyo nyaraka zote muhimu ziliungua.

“Ulinzi upo na ni walinzi wetu (mahakama), lakini hatujui kilichotokea kwa kuwa mlinzi aliyekuwa zamu hatujui alipo hadi muda huu (jana mchana), kila tukipiga simu yake inaita tu haipokelewi na muda mwingine anakata kabisa simu,” alisema Mwidete na kuongeza:

“Tumeomba wenzetu wa polisi na watu wa mitandao watusaidie kupitia utaalamu wao wa kimtandao kumpata.”

Alisema kazi ya kupata ukweli wa chanzo hicho unaendelea na kitengo cha ulinzi na usalama kupitia ofisi ya kamanda wa polisi mkoa na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji.

“Tumewaomba wenzetu wa zimamoto na polisi kutusaidia hili haraka iwezekanavyo.”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni