Polisi
wa India wamesema kwamba , msichana wa miaka 16 nchini humo amechomwa
moto akiwa hai baada ya wazazi wake kulalamika kwa wazee wa kijiji kuwa
binti huyo amebakwa.
Inspekta
wa Polisi, Shambhu Thakur alipozungumza na gazeti la Hindustan Times
amesema kwamba watu 14 wamekamatwa wakihusishwa na mashambulizi hayo
katika Jimbo la Mashariki mwa India Jharkhand.
Kwa
mujibu wa Shirika la Habari la BBC, Polisi huyo amesema wazee wa kijiji
waliamuru wanaotuhumiwa kuhusika na ubakaji huo walipe faini ya Pauni
550 kama adhabu.
Watu hao walikasirishwa na uamuzi huo na kuamua kuwapiga wazazi wa msichana huyo kisha kumchoma moto binti yao.
''Watuhumiwa
wawili waliwapiga wazazi kisha wakakimbilia kwenye nyumba yao wakiwa na
washirika wao na kumchoma moto msichana,” Ofisa wa Polisi, Ashok Ram
alisema.
Polisi
wanasema binti alibakwa na wanaume wawili katika eneo lenye msitu
karibu na kijiji cha Raja Kendua baada ya kutekwa akiwa peke yake
nyumbani kwao baada ya wazazi wake kuelekea kwenye harusi.
Baada ya tukio hilo wazazi walikwenda kupeleka mashtaka kwa wazee wa kijiji kuwashtaki wabakaji.
Mabaraza
ya kijiji hayana nguvu kubwa ya kisheria, hata hivyo yana ushawishi
mkubwa kwenye sehemu nyingi ya vijiji vya nchini India katika
kusuluhisha migogoro kuliko kutumia gharama nyingi kwenye mfumo wa
mahakama.
Polisi katika jimbo hilo wamesema wamewakamata watu 14 kati ya 18 ambao watachunguzwa kutokana na madai ya ubakaji na uuaji.
0 comments:
Chapisha Maoni