test

Jumatatu, 15 Mei 2017

MWENYEKITI WA KAMATI YA USAJILI KATIKA KLABU YA SIMBA AJIUZULU RASMI


MWENYEKITI wa kamati ya Usajili katika klabu ya Simba Sports Club Zacharia Hans Poppe amethibitisha rasmi kuandika barua yake ya kuachia ngazi kwenye kamati ya utendaji.
Mtazamo wa haraka haraka bila kuumiza akili ni kwamba,Hans Poppe anaondoka kwenye kamati ya usajili klabuni hapo.


Inadaiwa kwamba Mwenyekiti huyu wa kamati hii ya usajili ndugu yetu Hans Poppe hakuridhishwa na namna viongozi wa juu wa klabu ya Simba walivyoshiriki katika mchakato wa mkataba mpya na kampuni ya ubashiri ya SportPesa yenye maskani yao makuu nchini Kenya.



Mwenyekiti huyu alisema kwamba“Nimeamua kuondoka, utaona mambo hayakuwa sawa. Kulikuwa na siri na uficho na hata ushiriki wa kamati ya utendaji haukuwa sawa.
“Waliamua kufanya mambo kwa uficho na hadi wanasaini mkataba hakukuwa na uwazi wa mambo. Sitaki kuwa sehemu ya maamuzi ambayo yanakiuka uungwana."


Klabu ya Simba imeingia mkataba wa Sh bilioni 4.9 pesa za kitanzania ambao utadumu kwa miaka mitano.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni