test

Jumatatu, 10 Oktoba 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 65 & 66 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )



Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa
Ilioishia
“chumbani”
Nilizungumza huku nikizidi kupiga hatua za haraka, nikaingia kwenye lifti pamoja na john, ambaye alikuwa akinifwata kwa nyuma, ikasimama kwenye ghorofa ya tatu, kama jinsi nilivyo minya batani ya ghorofa hii ambayo niyatatu, nikaanza kukimbia kuelekea chumbani kwangu, nilipo muacha mke wangu akiwa amelala, wasiwasi mwingi ukiwa umenitawala, nikafika kwenye mlango wachumba changu, nikaufungua kwa nguvu, kitu cha kwanza kutazama nikitandani, nikastuka kukuta mke wangu hayupo huku shuka jeupe lililo tandikwa juu yakitanda likiwa limejaa damu nyingi, jambo lilizozidi kutustua mimi na john

Endelea
Nikakimbilia kwenye mlango wa kuingilia bafuni, ila sikufanikiwa kumuona phidaya, joto kali la mwili likaanza kuambatana na woga ambao tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kuupata siku hata moja, nikatizama kila shemu ya chumba hadi chini ya uvungu ila sikumuona mke wangu, machozi kwa mbali yakaanza kunilenga lenga, huku nikijaribu kutafakari ni nini nifanye

“kwani alikuwa humu ndani?”
Nilijikuta nikiachia msunyo mkali, baada ya john kuniuliza swali ambalo jibu analo kichwani mwake, kwani muda nilipokuwa ninatoka nilikuwa nipo mwenyewe, na sote tumekuta damu juu yakitanda iweje aniulize kwamba alikuwepo humu ndani, nikatoka kwa hatua za haraka, huku shati nililo livaa likiwa linavuja jasho jingi, sana

“sasa eddy unakwenda wapi?”
John aliniuliza huku akinifwatwa kwanyuma tukielekea zilipo lifti za ghorofa hili, sikumjibu john chochote kwa maana ninahisi, hatambui nini umuhimu wa mke, isitoshe mke mwenye kiumbe change tumboni, kupotea katika mazingira yakutatanisha, tukaingia kwenye lifti ambayo kuta zake nne zina vioo, nikawa na kazi yakujitazama jinsi macho yangu yanavyo tiririsha machozi yanayotoka pasipo kuwa na kilio, huku wekundu ukiwa umetawala kwenye macho yangu, john akanipa kitambaa chake ili nikisaidie kufuta machozi

“nimepata wazo, hembu twende kwenye chumba cha ulinzi kwa maana humu ndani kuna kamera za ulinzi kila kona”

John alizungumza huku akinitazama usoni, wazo lake kidogo likarudisha ufahamu kwani kitu ninacho kifikiria ni phidaya na kiumbe change, kitarajiwa

“samahani dada”
John alizungumza na muhudumu mmoja kwa kingereza, mara baada ya sisi kutoka kwenye lifti iliyo tufikisha chini kabisa katika eneo tulilokuwepo

“bila samahni?”
“ninaomba kuuliza ni wapi kwenye chumba cha cctv camera”
“kwani kuna tatizo?”

“ndio lipo, kuna dada mmoja, ni mjamzito amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha, mume wake alimuacha chumbani akiwa amelala ila tulipo kwenye hatujamkuta”

“mmmm kuseme ukweli, mimi sijaona dada mjamzito akitoka, labda chakuwasaidia nyinyi, nikuwapeleka kwa meneja na yeye ndio atatoa idhini ya nyinyi kupelekwa kwenye hicho chumba”

“asante dada”
Sikuchangia neon lolote zaidi yakuwasikiliza john na muhudumu jinsi wanavyo zungumza, huku macho yangu yakitazama kila upande wa sehemu tulipo simama, nikastukia nikuvutwa mkono na john ambao tayari walishaanza kuondoka na kuniacha mimi nikiwa nimesimama kama sanamu, lakuongozwa na betrii

“kaka, usijali shemeji atapatikana, ninaimani hawezi kuondoka humu ndani ya hoteli kwa hali ile”

John aliendelea kuzungumza huku tukipiga hatua tukimwafwata dada, huyu kwanyuma, tukaingia kwenye moja ya chumba ambapo macho yangu hayakuwa ngeni kwa mtu aliye kaa kwenye kiti hichi huku akionekana kwamba ndio meneja wa hii hoteli

“meneja kuna, hawa wageni wa…..”

Meneja wake akainua mkono, kwa ishara ya kumkatisha mfanyakazi wake, na meneja wake akapiga hatua za haraka hadi sehemu nilipo simama mimi, huku akiwa ametabasamu usoni mwake, akanikumbatia kwa furaha, hapa ndipo nikapata uhakika kwamba ni mlinzi wa baba, ambaye kuna kipindi alinipeleka kwenye benki, nikatoe pesa kwa ajili ya kununulia siku ila ndipo nilipokutana na sheila baada ya jamaa kumkuta akiminyana na sheila aliyekuwa amechanganyikiwa

“eddy umekuwa mkubwa mdogo wangu”
Jamaa alizungumza huku akitabasamu, na mimi nikajikaza niweke tabasamu lakinafki ili mradi tu nisalimieane naye

“eddy mbona kama umepoteza furaha usoni mwako, unatatizo gani?”

Nikamuelezea jamaa jambo linalonisumbua,bila kupoteza muda akaniomba tuelekea chumba maalumu chenye video nyingi zinazoonyesha maeneo mbalimbali ya hotel, tukaanza kuonyeshwa matukio yaliyo pita muda mchache kwenye eneo la chumba chetu kilipo, tukashuhudia kumuaona mwanake aliye valia baibui lililo mficha sura yake akiingia ndani ya chumba change, muda mchache baada ya mimi kutoka, ndani ya dakika kadhaa akatoka akiwa amembeba mke wangu, kwenye mikono yake huku akiwa amemfunika kwa shuka jeupe, kama mtu aliye uwawa.

“peleka mbele kidogo”

Jamaa alizungumza na kumfanya muongozaji wa video hizi kupeleka picha za video mbele kidogo, ambapo tukamshuhudia mwanamke huyo ambaya hadi sasa, hivi sura yake hatukuiona, akimuingiza mke wangu kwenye gari yawagonjwa na kuondoka naye, pasipo watu kumshuhudia

“ujinga huu, ulipo kuwa unafanyika mulikuwa wapi?”

Jamaa alizungumza huku akimfokea mfanyakazi wake anaye ongoza mitambo ya kamera za ulinzia, mwili mzima ukaanza kunitetemeka na kujikuta nikizidi kuchanganyikiwa pasipo kujua ni kitu gani ambacho, nilimemkosea huyu mwanamke aliye mteka mke wangu, kila mmoja akabaki kimya akimtazama mwenzake asijue nini chakufanya

“sasa hapa itakuwaje?”
John alizungumza na kumfanya jamaa, ambaye hadi sasa hivi jina lake silifahamu kutokana sikuwa na mazoea naye sana kipindi yupo nyumbani kwa baba, akatoa simu yake na kuminya baadhi ya namba na kuiweka simu yake sikioni, akaanza kuzungumza lugha ya kizulu, ambayo kwangu si ngeni sana japo siifahamu.Akamaliza kuzungumza na simu na kututazama

“nimewasiliana na makao makuu ya polisi hapa ‘johannesburg’ na wameniambia wanaanza kulifanyia kazi muda huu”

“sa..Sa umesema wanafanyia kazi?”
Nilizungumza kwa kiwewe kikubwa huku nikimtazama jamaa
“ndio wameshaanza kulifanyia kazi, kwani nimewatajia hadi namba za gari kuhakikisha wanalinasa gari husika”

Jasho halikuacha kunitiririka japo kuwa ndani ya chumba hichi kuna baridi nzuri yajutosha, jamaa akamuomba mtu wake azitume picha za gari na mwanamke hukyo makao makuu ya polisi kupitia mtandao(internet), ili kuzidi kuwarahisishia kazi askari polisi

“eddy usiwe na wasiwasi, kama tukio limefanyika kwenye hoteli hii basi, muhalifu aliye mteka mke wako atapatika tu”

“ila mke wangu atakuwa amesha fariki”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga, twasira za sura ya mke wangu masaa machache ya nyuma yaliyo pita zikaanza kunisumbua kichwani mwangu, nikajikuta nikianza kujilaamu nikwanini nilitoka chumbani kwangu na kumuacha phidaya wangu akiwa amelala peke yake, jamaa akasogea pembeni na kuzungumza na simu, sikujua anazungumza na nani, baada ya muda akarudi tulipo

“eddy nilikuwa nikizungumza na baba yako, na yupo njiani anakuja”
“baba yake!?”

John aliuliza huku akiwa ameshangaa, sikutaka kumjibu kitu chochote zaidi ya kujikalia zangu kwenye kiti huku mapigo ya moyo yakianza kunienda mbio, ndani ya dakika ishirini, mlango ukafunguliwa na akaingia baba akiwa na walinzi wake wanne walio valia suti nyeusi pamoja na miwani, nikanyanyuka kwenye kiti na kukumbatiana na baba huku akionekana kuwa nafuraha usoni mwake, kwani hakuamini uwepo wangu, jamaa akaanza kumuelezea baba kila kitu kilicho tokea na kumuonyesha baadhi ya video hizo za mwanamke aliye mteka mke wangu

“pole sana eddy”

Baba alinipa pole na mimi nikaiitikia kwa sauti ya chini, tukatoka ndani ya chumba nikiwa nimeongozana na baba pamoja na walinzi wake, huku jamaa na john wakifwata kwa nyuma, tukakuta polisi wakiwa wanafanya vipimo kwenye chumba change

“mumefikia wapi?”
Baba alimuuliza mmoja wa polisi
“hii damu, inaonekana si damu ya mauaji”
“kivipi?” baba aliuliza tena
“inaonekana mtekaji alimwaga damu kwenye shuka kutoka kwenye pakti za kuhifadhia damu”

Askari alituambia huku akituonyesha pakti mbili za kuhifadhia damu, walizo zitoa ndani ya chumba changu baada ya kukifanyia uchunguzi sana

“ila mtekaji atapatikana kwa maana inaonekana hajatoka mbali sana na hapa”

Polisi alizungumza, ila moyo wangu haukuwa na furaha hata kidogo japo wanadai kwamba ni damu ndizo zilizo mwagwa kwenye shuka la chumbani kwetu, tukatoka na baba hadi sehemu ya kupumzikia, ukimya ukatawala kati yetu, hapakuwa na aliye zungumza kitu chochote zaidi ya mimi kutazama tazama mandhari yaliyomo humu ndani

“eddy, ulikuwa wapi mwanangu?”
“baba, ngoja hayo mazungumzo tutayazungumza baada ya kufikia muafaka kutambua ni wapi alipo mke wangu”

Nilizungumza kwasauti nzito iliyo jaa hasira ndani yake, baba alinielewa na kukaa kimya hakutaka aendelea kunigusia kuhusiana na kitu cha aina yoyote.Simu ya baba ikaita na akaanza kuzungumza na mtu aliye mpigia

“eddy twende sehemu, lile gari lawagonjwa limepatikana”

Baba aliniambia mara baada ya simu kukata, nikawa wakwanza kunyanyuka kwenye kiti na kuanza kuongozana, tukaingia kwenye gari huku john akiingia kwenye gari ya jamaa ambaye ni meneja wa hoteli.Tukatembea umbali wa kilomita kumi, tukafika pembezoni mwa mlima na kuwakuta polisi wengi wakiwa wamelizingira gari lawagonjwa, kwa umbali kidogo ambalo pembeni limezungushiwa mabomo yakutega yapatayo sita, bomo moja nikaliona likiwa limebakisha sekunde hamsini huku zikiendelea kurudi nyuma taratibu

“phidaya”
Nilianza kukimbia kuelekea lilipo gari lawagonjwa polisi wakanidaka, na kunizuia nisiendelee kwenda mbele, gafla mlipuko mkubwa ukalipuka kwenye gari na kusababisha polisi walio nikamata kuniangusha chini na kunifunika na miili yao waliyo valia nguo maalumu zinazo zuia kuadhirika na vipande pande vya vyuma vitokanavyo na mabomu endapo vitawaangukia

“phidayaaaaaaaaaaaaaaaaaa”

Nilizungumza kwa sauti ya juu huku machozi ya uchungu yakinimwagika usoni mwangu, huku nikilishuhudia gari alilopo mke wangu likiteketea kwa moto mkali


    *****sory madam*****(68)

Askari wa kikosi cha zima moto wakaanza kulishambulia gari la wagonjwa kwa kutumia mipira mirefu inayotoa maji kwa kasi kiasi kwamba, moto ukaanza kupunguza makali yake ya kuteketea, amchozi yalizidi kunitoka huku askari wakiendelea kunizuia nisikaribie eneo ambalo lipo gari, wakanikabidhi kwa walinzi wa baba, ambao waliendelea kunishika.Si mimi tu ambaye nipo kwenye huzuni, ila hata rafiki yangu john, machozi yalianza kumtoka, na kuzidi kunizidishia hisia ya kumwagikwa na machozi mengi

“eddy, jikaze mwanangu”

Baba alizungumza huku akinikumbatia, akiendelea kunipigapiga mgongoni ikiwa ni ishara ya kunituliza hasira na uchungu ambao nimeupata, askari wengine wakaanza kazi ya kuchambua kama kuna kitu kilicho salia kwenye gari, ikiwemo kupata udhibitisho wa kama kuna mwili wa mtu ambaye alikuwepo ndani ya gari, mwili mzima ukazidi kunitetemeka kwa woga, kila ninapojaribu kutazama gari lililo teketea kwa moto, dua yangu kubwa ni kumuomba mungu aweze kutenda miujiza phidaya asiwepo ndani ya gari hilo.

Askari mmoja akatufwata sehemu nilipo simama mimi pamoja na askari wa baba, huku mkononi mwake akiwa ameshika kibegi kidogo, na viganjani mwake akiwa amevaa gloves nyeusi.Akamsalimia baba, kasha akatusalimia na sisi, akamuomba baba wazungumze pembeni, baba akatii ombi la askari huyo, sikusikia kitu ambacho wanakizungumza

Mlio wa simu ya john, ukanistua kutoka katika dimbwi kubwa la mawazo na kujikuta nikimgeumkia na kumtazama kwa macho yaliyo jaa huzuni nyingi, john akaitazama simu yake kwa muda huku akiwa amekunja ndita, akaipokea na kukaa kimya

“nani mwenzangu?”

John alizungumza baada ya sekunde kadhaa ya simu yake kuwa sikioni

“hapana, mimi ninawapa watu wengi namba yangu, kwahiyo usipo taja jina lako mimi siwezi kutambua kwamba wewe ni nani?

John alizungumza kwa sauti  ya ukali huku macho yake akiya pepesa pepesa

“wee mwendawazimu nini, usinichangenye”

John alizungumza huku akiachia msunyo mkali na kukata simu yake, nikaanza kupiga hatua kulifwata gari lililo teketea ambapo kuna askari, pamoja na madaktari wakiendelea kufanya uchunguzi na vifaa vyao maalumu.Nikafanikiwa kufika pasipo mtu yoyote kunishika mkono, nikakuta wakiyapiga picha, mafuvu mawili ya watu, yaliyo tekete kwa moto, ikiashiria kwamba miili yao, imesha teketea, nikajikuta nikianguka chini kama mzigo, kutokana na kuishiwa na guvu za mwili wangu.

Madaktari wakaniwahi kunipa huduma ya kwanza, ikiwemo kuniwekea mashine ya kunisaidia kuhema, japo fahamu hazijanipotea, ila sikuwa na uwezo wakuuamuru mwili wangu kufanya kitu, ambacho ninakihitaji, machozi yakaanza kunichuruzika, kumbukumbu za gari kulipuka dakika chache zilizo pita zikaanza kunijia kichwani mwangu, nikaanza kuisikia sauti ya phidaya kwa mbali ikiniita masikioni mwangu, nikataka kunyanyuka, ila madaktari wakanizuia nisinyanyuke

“mwanangu atapona?”

“ndio mzee atapona, ni mstuko tu, ndio umempata ulio pelekea yeye kuishiwa na nguvu, kidogo na uwezo wa moyo wake ulishindwa kudunda kama inavyo paswa ufanye”

Daktari mmoja nilimsikia akimjibu baba, huku wezake wakiniinyanyua kwenye machela, waliyo kuwa wameniweka wakinipatia huduma ya kwanza na kuniiingiza ndani ya gari.John akawahi kuingia ndani ya gari la wagonjwa, lililokuja muda mchache baada ya mimi kuanguka chini.

“eddy”
John aliniita, na kumtazama taratibu, pasipo kumjibu kitu chochote, kwani hata kuzungumza kumenishinda kabisa
“mungu, atasaidia kila kitu kitakuwa sawa”

John alizungumza kwa kunifariji tu, kwani ukweli halisi nimeshaujua, kwamba phidaya sipo naye tena duniani, kwani mafuvu mawili ni yawatu ambao nimeyakuta kwenye gari, yanaashiria kwamba ni mke wangu ni marehemu.

Wakanishusha kwenye gari, wakaniweka kwenye kitanda cha kusukuma, manesi wawili wakaanza kukisukuma kitanda nilicho lalia hadi kwenye moja ya chumba na kuniingiza humu, nikakuta madaktari wawili wakiwa ndani ya chumba wakiwa tayari kwa kunihudumia.Wakanichoma sindano kwenye mkono wangu wa kushoto sehemu ya mshipa wa damu, kasha waniwekea baadhi ya vifaa kifuani kwangu, ambavyo sikuelewa kazi yake ni nini.Wakamaliza kufanya kazi yao, ya kunihudumia na kutoka ndani ya chumba, msongamano wa mawazo ukazidi kunipelekesh, huku sura ya mke wangu phidaya ikiwa haichezi mbali na fikra zangu

“eddy I love you”(eddy ninakupenda)

Sauti ya phidaya ikaendelea, kusikika kwenye masikio yangu, nikajitahidi kuyazungusha macho yangu kila pande ya chumba kutazama kama nitaweza kumuona mke wangu ila sikufanikiwa, kuiona sura yake.Baada ya masaa manne mlango ukafunguliwa na akaingia baba pamoja na john, kila mmoja anaonekaa kuwa na huzuni, baba akasimama pembeni ya kitanda change, huku john akikaa sehemu ndogo ya kitanda nilicho lalia

“unajisikiaje mwangu”
“safi”
Nilimjibu baba kwa sauti ya chini, iliyo jaa mkwaruzo
“baba, yale mafuvu yapo wapi?”

 Baba hakunijibu zaidi ya kumtazama john, kisha wakanitazama hakuna aliye jibu swali langu, ila macho yao nikatambua kwamba yanakitu wanacho kijua ila wananificha

“ahaa…., inabidi kwamba…… ahaaa kesho urudi nyumbani, ukapumzike kwa muda kidogo ili uwe sawa”

Baba alizungumza kwa kubabaika, nikamtazama john, akatizama chini baada ya macho yangu kukumbana na macho yangu.Simu ya baba ikaita ikambidi atoke nje kwenda kuipokea

“john niambie ukweli mke wangu amekufa?”
“eddy………………”

John aliniita, nikabaki nikimtazama pasipo kumuitikia.Ukimya ukatawala, kama dakika mbili john hakunijibu swali langu nililo muuliza.Kijimlio kifupi kikasikika kwenye simu ya john iliyopo mfukoni, ikamlazimu kuitoa simu yake, mfukoni.Akasoma meseji aliyo ingia, akanitazama kwa jicho la kuiba na kuitazama tena meseji anayo isoma

“kaka hembu soma hicho kilicho indikwa”

John akanipa simu, kabla sijaisoma meseji iliyopo kwenye simu, baba akaingia ndani akiwa ameongozana na madaktari walio, nitibu muda mchache ulio pita, wakafika kwenye kitandani nilicho lala.Daktari mmoja akanitoa vifaa walivyo niwekea kifuani,

“how do you feel?”(unajisikiaje?)
Daktari mmoja aliniuliza
“najisikia powa”

Daktari wa pili akaniwekea kifaa kigo cha kusikilizia mapigo ya moyo, akamtazama baba

“kwa sasa yupo salama, tunaweza kumruhusu kurudi nyumbani”
“shukrani daktari”

Baba alizungumza, huku akimpa mkono dokta, wakanipa vidonge vya kuupa mwili wangu nguvu, nikaruhusiwa kutoka hospitalini, tayari giza lilisha anza kutawala anga, kwa mbali, ikiwa ni majira ya jioni, tukaingia kwenye gari moja mimi pamoja na john, huku baba akiwa katika gari lake jengine

“uliisoma ile meseji?”
“ngoja noisome”

Nikaitoa simu mfukoni na kumpa john anitolee namba za siri alizo ziweka kwenye simu yake upende wa meseji kisha akanirudishia

{kaa mbali na hii vita kati yangu mimi na eddy, utaumia}

Nikairudia kuisoma tena meseji kwa msisitizo, kisha nikamtazama john, huku mapigo ya moyo yakianza kunienda mbio

“nani aliye ituma hii meseji?”
“mimi wala sijui, kutoka hata namba yenyewe haionekani”
“mmmmmm, ulimuonyesha mtu mwengine tofauti yang?”
“pale ilipokuwa inaingia, ndio nikakukabidhi hiyo simu”

Nikashusha pumzi kubwa huku nikiendelea kumtizama john machoni, nikajaribu kuipiga namba iliyo tuma hii meseji ila haikenda zaidi ya kukatika.Tukafika nyumbani kwa baba, mazingira nikayakuta yamebadilika kwa kiasi kikubwa sana, kuanzia nje hadi ndani, sikumkuta yule mama wa kambo aliyekuwa akinisumbua akili yangu kipindi nilipokuja kwa mara ya kwanza

“una mpango gani, juu ya hili eddy?”

Baba aliniuliza mara baada ya mimi, kukaa kwenye moja ya sofa lililopo hapa sebleni, nikakaa kimya kwa muda kabla sijamjibu baba, kwani akili yangu ikaanza kutafakari juu ya meseji aliyo tumiwa john, inavyo onekana mtu huyo ananijua mimi vizuri ndio maana ameamua kunifanyia unyama wa kumuangamiza mke wangu

“sijajua baba”
Jibu langu, likamfanya john kunitazama kwa mashangao
“ngoja tupate ripoti ya polisi juu ya muhusika, wa tukio zima kisha tutajua nini cha kufanya”
“sawa baba”

Baba alizungumza na kuanza kupandisha ngazi kuelekea ghorofani, nikasikia sauti ya kike ikizungumza na baba, ikanilazimu kusimama kutazama ni nani anaye zungumza naye, macho yangu yakakutana na macho ya mototo wa mama wa kambo, ambaye kipindi ninakuja kwa mara ya kwanza nyumbani kwa baba, yeye alikuwa chuo akisoma

“waoooo kaka eddy”

Alinikimbilia na kunikumbatia kwa furaha, sikuamini macho yangu kwani mimi na yeye kidogo kuta tofauti zilizo tokea kipindi cha nyuma, hususani swala la mimi kumpiga mama yake

“za huku utokapo?”
“si salama”

Nikamuona john akimshangaa huyu dada yangu, akataka kumpa mkono ila akasita, ikanilazimu nimtambulishe mimi

“dada huyu ni rafiki yangu anaitwa john, na john huyu ni motto mwengine wa baba yangu”
“nashukuru kukufahamu”
John alizungumza huku akimpa mkono dada yangu
“eddy unatabia mbaya”
“kwa nini dada?”
“hadi leo hulitambui jina langu”
“ahaaa”

Nilibaki nikitabasamu tu, kwani ni kweli jina lake sikuwa ninalikumbuka vuzuri

“mimi ni victori”
“ahaaa, kama lilikuwa likinijia kwenye akili yangu vile?”
“kwenda kulee, ulikuwa hulijui”

Alizungumza kwa utani, huku akiichezea chezea mikono yangu, tukatizamana kwenye macho kwa sekunde kadhaa, sote tukajikuta tukiwa kimya

“mama yupo wapi?”

Nilimuuliza na kumfanya apooze gafla, akaniachia mikono yangu na kwenda kukaa kwenye moja ya sofa, huku machozi yakimlenga lenga, akainyanyua sura yake kidogo na kunitazama

“mama, amesha fariki”

Alizungumza kwa sauti ya upole huku machozi yakianza kumtoka, nikapiga hatua hadi alipo kaaa, nikamkumbatia, huku na mimi hisia za mke wangu kufa, zikaanza kunijia kichwani

“eddy kwa nini unalia?”
“mke wangu amekufa”
“weeee”
Victoria alistuka baada ya kusikia maneno haya

“amefariki lini?”
“leo”
“leoooo?”
“ndio”
“kwa nini?”
“amefariki kwa mlipuko wa bomu baada ya kutekwa, na mtu asiye julikana”

John akabaki akitutizama jinsi tunavyo zungumza mimi na dada yangu, victoria akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kunibembeleza kwa hisia kali, tukaachana na stori za kufa kwa mke wangu, tukaendelea kuzungumza kuhusiana na mambo mengine, muda wa chakula ukawadia na sote tukakaa kwenye meza maalumu ya chakula, nikagundua kitu kutoka kwa john, wakati wote alikuwa na kazi ya kumtazama victoria kwa macho ya kumtamani.Tukamaliza kula mimi na john, tukaelekea kwenye chumba change

“john mbona ulikuwa unamtazama sana victoria?”
“hapana”
“mmmmm john wewe hakuna cha hapana, au umempenda nikuunganishine”
“ahaaa eddy, ila ngija kuna kitu ninakichunguza, kikikamilika nitakuambia”
“kitu gani?”

John akautazama mlango wa kuingilia humu ndani ya chumba change, akapiga hatua za taratibu huku akiniomba ninyamaze kuzungumza, akaliweka sikio moja kwenye mlango, huku mkono wake mwingine ukishika kitasa cha kufungulia mlango, akaanza kuufungua taratibu, mimi nikawa na kazi ya kumtazama jinsi anavyo fanya.Akauvuta kwa nguvu, macho yetu yote yakakutana na victoria akiwa amevalia nguo ya kulalia, inayo onyesha nguo yake ya ndani

“vicktoria vipi?”

Nilimuuliza victoria baada ya yeye kushindwa kuzungumza kitu kinacho mfanya asimame nje ya mlango wetu, akaanza kuvunja vinja vidole vyake kwa aibu, akamtazama john, ambaye hakuwa amezungumza kitu cha aina yoyote, akamshika john shati lake, kisha akamvuta karibu yake na kumpiga busu la mdomo na kunifanya nibaki nikiwa ninamshangao

“I need you john”(john, ninakuhitaji)

Victoria alizungumza huku akimsukumia john ndani ya chumba, changu, kama simba mwenye njaa victoria akamsukumiza john kitandani na kuanza kumvua shati, lake, kwa aibu ikanilazimu mimi kutoka ndani ya chumba nikawaacha waendelee na mambo yao

  Itaendelea...

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx