test

Ijumaa, 5 Juni 2015

Linah ashtushwa na uhusiano kati ya ex wake na Wema Sepetu>>SOMA HAPA




Linah Sanga amesema taarifa kuhusu uhusiano kati ya Wema Sepetu na aliyekuwa mpenzi wake umemshangaza.

Akiongea kwenye kipindi cha Ala za roho cha Clouds FM, Linah alisema yeye na mpenzi wake waliachana rasmi miezi miwili iliyopita.
 
“Hata mimi nasikia kuwa sasa hivi anatoka kimapenzi na Wema Sepetu,” alisema Linah. “Unajua mtu kama alishawahi kuwa mtu wako lazima upate mshtuko, kwakweli hata mimi imenishtua sana. 
 
"Kwahiyo mimi namuachia Mungu, nina imani aliyopanga Mungu binadamu hawezi kupangua. Na pia nawatakia kila lakheri katika mahusiano yao.
 
" Sasa hivi nipo busy na kazi zangu maana mimi sikuzaliwa naye na wala sitozikwa naye. Na mimi kwa upande wangu nipo poa kabisa.”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni