Vikosi vya vijana hao wanaoiunga mkono serikali viliwaambia waandishi wa habari Ijumaa kwamba mashambulizi yalitokea Jumatano usiku.Gazeti la taifa la Nigeria liliripoti kwamba vijiji vyote katika jimbo la Borno,vilikuwa Koshifa , Matangle ,
Buraltuma,Darmanti, Almeri na Burmari.
Mmoja wa askari sungu sungu hao Ahmed Ajimi aliliambia shirika la AP kwamba waathirika walikuwa wakulima ambao hivi karibuni walirudi vijijini kwao baada ya askari wa Nigeria kuwaondoa Boko haram katika maeneo mapema mwaka jana.
0 comments:
Chapisha Maoni