Dora
anayedaiwa kujifungua nazi. Ilidaiwa kuwa, chanzo cha Dora kujifungua
nazi ni maneno aliyoambiwa na mke mwenzake aliyefahamika kwa jina la
Jamila ambapo aliambiwa hatajifungua kiumbe cha kawaida na ndipo
alipokimbilia Dodoma kukwepa matatizo.Na waandishi Wetu
Maajabu! Msichana aliyefahamika kwa jina la Dora mkazi wa Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani, hivi karibuni amejikuta akijifungua nazi badala ya mtoto, jambo lililomshangaza kila mtu.
Ushirikina watajwa
Msikie Dora
Akizungumza na Amani hivi karibuni akiwa nyumbani kwake Bagamoyo, Dora alisema:
“Nilihamia Bagamoyo nikitokea Mwanza, nikakutana na mwanaume anayeitwa Pascal, tukakubaliana tuishi kama mke na mume.
“Baada ya kukubaliana hilo, nikapata ujauzito lakini nikashangaa siku moja akaja mwanamke na kusema yeye ni mzazi mwenzake na Pascal.“Alifanya vurugu, akanijeruhi kisha akachukua TV na vitu vingine, akaondoka huku akiniambia lazima nijifungue kiumbe cha ajabu. Nilipata hofu kubwa, mara nikaanza kusumbuliwa na tumbo, nikapelekwa kwa mganga ambapo niliambiwa nimerogwa.
Mume
wa Dora akihojiwa na mwandishi wa habari (hayupo pichani) “Nikatibiwa
kisha nikafungwa kitambaa chenye dawa mkononi na kuambiwa nisikivue.
“Siku moja kikapotea kimaajabu, baadaye tukakiona juu ya mti nje ya
nyumba. Nikaachana na masuala ya kienyeji, nikaamua kwenda kanisani,
hata hivyo mauzauza hayakuisha,” alisema Dora na kuongeza:
“Siku uchungu uliponijia nikiwa Dodoma, ndugu zangu na wakunga wakaja kunisaidia lakini cha ajabu wakashangaa kuona nazi ndiyo inatoka.“Wakakimbia na kuniacha nikipandisha mashetani, akaitwa mganga wa kienyeji lakini naye aliogopa ndipo nikapelekwa kwa walokole kuombewa.
“Nilipopata nafuu na kurudishwa nyumbani, polisi wakaja na kutuambia eti tumetupa mtoto, wakasachi hawakuona kitu, wakatupeleka kituoni.“Huko nako nikapandisha mashetani, nilipotulia nikapelekwa hospitali ambako nilisafishwa lakini ishu ikawa kubwa, polisi wakatuchukua mimi na mume wangu na kutuweka ndani, tulitoka baada ya kutoa pesa.
Mfano
wa nazi aliyojifungua Dora. “Cha ajabu niliporudi nyumbani ili nichukue
kadi niende kliniki, nikakuta shanga kibao, ndipo tukaona cha msingi ni
kurudi Bagamoyo na kuhama pale tulipokuwa tunaishi,” alisema Dora huku
akiungwa mkono na mumewe, Pascal.
Imeandaliwa na Chande Abdallah na Deogratius Mongela
Maajabu! Msichana aliyefahamika kwa jina la Dora mkazi wa Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani, hivi karibuni amejikuta akijifungua nazi badala ya mtoto, jambo lililomshangaza kila mtu.
Ushirikina watajwa
Msikie Dora
Akizungumza na Amani hivi karibuni akiwa nyumbani kwake Bagamoyo, Dora alisema:
“Nilihamia Bagamoyo nikitokea Mwanza, nikakutana na mwanaume anayeitwa Pascal, tukakubaliana tuishi kama mke na mume.
“Baada ya kukubaliana hilo, nikapata ujauzito lakini nikashangaa siku moja akaja mwanamke na kusema yeye ni mzazi mwenzake na Pascal.“Alifanya vurugu, akanijeruhi kisha akachukua TV na vitu vingine, akaondoka huku akiniambia lazima nijifungue kiumbe cha ajabu. Nilipata hofu kubwa, mara nikaanza kusumbuliwa na tumbo, nikapelekwa kwa mganga ambapo niliambiwa nimerogwa.
“Siku uchungu uliponijia nikiwa Dodoma, ndugu zangu na wakunga wakaja kunisaidia lakini cha ajabu wakashangaa kuona nazi ndiyo inatoka.“Wakakimbia na kuniacha nikipandisha mashetani, akaitwa mganga wa kienyeji lakini naye aliogopa ndipo nikapelekwa kwa walokole kuombewa.
“Nilipopata nafuu na kurudishwa nyumbani, polisi wakaja na kutuambia eti tumetupa mtoto, wakasachi hawakuona kitu, wakatupeleka kituoni.“Huko nako nikapandisha mashetani, nilipotulia nikapelekwa hospitali ambako nilisafishwa lakini ishu ikawa kubwa, polisi wakatuchukua mimi na mume wangu na kutuweka ndani, tulitoka baada ya kutoa pesa.
Imeandaliwa na Chande Abdallah na Deogratius Mongela
0 comments:
Chapisha Maoni