test

Alhamisi, 24 Mei 2018

Lukuvi, Mengi Wakutana Kujadili Fursa za Uwekezaji


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amekutana na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dkt. Reginald Mengi ili kuzungumza na kutambua fursa zinazopatikana za uwekezaji katika sekta ya Ardhi nchini.

Dkt. Mengi amekutana jana na Mhe. Lukuvi ofisini kwake kanda ya Dar es salaam ambapo walijadili mambo mbalimbali ambayo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeyafanya katika sekta ya ardhi  na kutoa fursa  kwa wawekezaji wa ndani kuwekeza kwa urahisi.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni