Watu
watatu wamefariki dunia papo hapo na wengine takribani 7 kujeruhiwa
vibaya baada ya Lori la mchanga aina ya SCANIA lililodaiwa kupata
hitilafu katika mfumo wake wa breki kuwagonga.
Taarifa za ajali hiyo zinasema, ajali imetokea katika maeneo ya Boko Magengeni, jana Mei 7, 2018 ambapo inadaiwa lori hilo liliwaparamia watu waliokuwa pembezoni mwa barabara huku likisaga pikipiki kadhaa ambazo lilizipitia.
Kufuatia
tukio hilo, RPC Kinondoni, Jumanne Murilo amethibitisha kutokea kwa
ajali hiyo na kusema bado wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo hasa
cha ajali hiyo.
Mbali na watu hao kupitiwa na roli hilo, zimo bodaboba na gari nyingine za abiria (coaster) ambazo zilipitiwa na lori hilo.
Pia
inadaiwa wengine waliojeruhiwa ni wauza mitumba ambao hupanga kando ya
barabara huku wengine wengi wakinusurika baada ya kukimbia walipoona
ajali.
Credit: GlobalPublisher
0 comments:
Chapisha Maoni