test

Jumatano, 31 Mei 2017

Yeriko Nyerere Atiwa Mbaroni saa tisa usiku


Kada wa Chadema Yeriko Nyerere, amekamatwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni polisi au usalama wa taifa  leo akiwa nyumbani kwake Kigamboni, Mbutu.

Taarifa iliyotolewa na Meya wa Ubungo, Boniphace Jacob imeeleza kuwa Nyerere alikamatwa na watu hao ambao waliambatana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbutu.

“Nimepata taarifa kutoka kwa ndugu wa Yeriko ambao wamenipigia simu alfajiri leo. Wamesema amekamatwa saa tisa usiku na watu hao ambao walivalia kiraia.  Viongozi wa Chadema wanaelekea polisi kufuatilia kwa kina chanzo cha Yeriko kukamatwa,” amesema Jacob

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni