test

Jumatatu, 22 Mei 2017

Ben Pol amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu picha zake za uchi mitandaoni


Ben Pol ambaye aliachia picha kadhaa akionekana uchi amefunguka kwa Mara ya kwanza kuelezea kilichomkuta.

Ben Pol alichapisha picha hiyo kwenye ukurasa wake wa Instagram inayomuonyesha akiwa amekaa kwenye kiti mtupu huku mikono yake ikiwa imefungwa nyuma ya kiti. 
Baada ya kuchapisha picha hiyo, hakuandika maelezo yoyote huku washabiki wake na watu wengine wengi wakionyesha kuchukuzwa na picha ile.

Mbali na mashabiki wake waliyotoa maoni yao, wasanii wenzake pia walionyesha kutoelewa Ben Pol amemaanisha nini kwa kuchapisha picha ya namna ile kwani wengi walimchukulia kama mtu mstaarabu asiye na mambo ya hivyo.

Licha ya hayo yote kuzungumzwa na watu mbalimbalia, mhusika mkuu wa tukio hilo, Ben Pol amewataka watu kutokuhumu jambo wasilolijua kabla hayajaelewa lengo kuu.
 
Kupitia kwa mtandao wake wa Instagram ,Ben Pol ameweka ujumbe ambao ameambatanisha na wimbo unaosikika ukiimbwa, kitu kinachomaanisha ni ujio wa wimbo wake mpya
Ben Pol aliandika, “Usi-judge kitabu kama hujakisoma ndani
A post shared by BEN POL (@iambenpol) on

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni