test

Alhamisi, 10 Novemba 2016

VIDEO:MWILI WA MAREHEMU WAZIRI WA ZAMANI WA AWAMU 4 ZA KWANZA UKIAGWA RASMI KARIMJEE HALL LEO LIVE!!


Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza kwa niaba ya Serikali. Shughuli za kuaga zinaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli.
 
Marehemu Mungai amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi na utumishi katika Chama na Serikali. Alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Mkuu wa Mkoa, Mbunge kuanzia miaka ya 1970 hadi 2010, na pia amekuwa Waziri katika wizara mbalimbali za Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuanzia Awamu ya 
kwanza mpaka ya nne.
Viongozi Wastaafu, kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya pili Mh.William Benjamin Mkapa pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu awamu ya Pili Mh.Frederick Sumaye na viongozi wengine waandamizi wakiwa tayari kwa kuanza kuaga mwili wa marehemu Joseph Mungai ndani ya ukumbi wa Karimjee jijini Dar.
Viongozi Wastaafu mbalimbali wakiwa tayari kwa kuanza kuaga mwili wa marehemu Joseph Mungai ndani ya ukumbi wa Karimjee jijini Dar.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx