test

Jumapili, 13 Novemba 2016

Maandamano ya Kumtaka Rais wa Korea Kusini Ajiuzulu yaingia Wiki ya Pili



Maelfu ya watu wanaendelea kuandamana katika mitaa mbalimbali ya mji mkuu wa Seoul, Korea Kusini kwa wiki ya pili mfululizo wakimtaka Rais wa nchi hiyo, Park Geun-hye ajiuzulu.

Mandamano ya jana yalitarajiwa kuwa makubwa zaidi yaliyowahi kutokea huku viongozi wa maandamano hayo wamesema mamilioni ya watu watashiriki huku wakiwa na nia ya kufika ikulu ya nchi hiyo.

Wakati huo huo serikali imewatuma maelfu ya maafisa wake wa polisi kwenye mji huo kwa ajili ya kukabiliana na ghasia za waandamanaji hao wanaopinga serikali.

Rais Hye anatuhumiwa kwa kuvujisha nyaraka za serikali kwa rafiki yake wa karibu anayefahamika kwa jina la Choi Soon-Sil ambaye alijaribu kuibia serikali fedha nyingi kupitia kampuni kadhaa za taifa hilo.

Hata hivyo Choi amekamatwa na kushtakiwa kwa ubadhirifu wa fedha za umma alizowahi kuziiba na kutumia vibaya mamlaka yake huku maafisa kadhaa waliopo kwenye ofisi ya Rais Guen wanachunguzwa dhidi ya sakata hilo.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx