test

Jumatatu, 17 Oktoba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 25 & 26



MWANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA....
“Raisi……!!”
Rahab alizungumza baada kwa mshangao baada ya kutokumuona Raisi Praygod kwenye usawa wa bahari jambo lililoanza kumpa wasiwasi mwngi.Ikamlazimu kurudi tena ndani ya maji, kutazama kama anaweza kumuona raisi, ila hakumuuona
“Mungu wangu!!”
Rahabu alizungumza kwa kuhamaki baada ya kuona kitu kikija kwa kasi katika upande aliopo yeye, kwa haraka haraka akagundua kwamba ni samaki mmoja hatari aina ya Papa, ndiye anaye karibia kufika katika eneo alilopo.

ENDELEA.....
Rahab akaanza kujipapasa mwiki mwake kwa haraka, kwabahati nzuri akakikuta kisu kwenye mguu wake wa kulika katika sehemu ya kiatu alipo kichomeka kipindi alipokuwa akivaa, nguo alizo nazo kwenye chumba maalmumu cha kuhifadhia nguo katika ndege ya raisi iliyo anguka muda mchache uliopita.

Akajiweka tayari kwa kupapambana na samaki huyu anaye mfwata kwa kasi katika eneo ambalo  ameangukia, kufumba na kufumbua samaki huyu tayari akawa aweshafika katika eneo alipo Rahab, kwa ustadi wa hali ya juu Rahab akajigeuza ndani ya maji na kushuka kwa kasi ndani ya maji, na kusababisha samaki huyu mkubwa kupita juu yake, kwa kasi jambo lililo zidisha ukali wa samaki huyu mwenye uchu wa kutafuna kiumbe chochote kitakacho ingia kwenye enoa la bahari alipo yeye

Rahab akakishika vizuri kishu chake chenye ncha kali, na kutazama jinsi samaki huyu anavyo kunja kona na kurudi katika eneo alipo kwa kasi kubwa, samaki akamfikia Rahab kwa karibu kabla samaki hajafanya maamuzi ya aina yoyote, Rahab akamuwahi kumchoma kisu kwenye eneo la tumbo la samaki huyu, lenye ngozi laini na kuanza kulichana kwa kutumia nguvu nyingi, jambo lililo sababisa damu nyingi kutapakaa katika enoa la sehemu walipo, huku utumbo mwingi wasamaki huyu ukitapakaa kwenye maji
“Haaaaaaaa”

Rahab alizungumza huku akichomoza kichwa chake kwenye maji, huku akivuta pumzi kwa wingi, akajilegeza mwili wake na kuufanya uanze kuelea elea juu ya maji, huku akitazma juu mwili wake ukiwa umechoka sana
                                                                                                  Agnes akamgeuza mtu aliye anguka na kumchunguza vizuri na kugundua kwamba anamajeraha kadhaa kwenye mwili wake, Agnes akapiga mluzi ulio mfikia Halima aliyekuwa katika eneo la karibu, Halima akapa hatua za haraka hadi katika sehemu alipo simama Agnes
“Best kuna mtu hapa nimemuona”

Agnes alizungumza huku akimgeuza mtu aliye lala chini huku damu zikimvuja, Halima akamtazama mtu aliye lala chini kwa umakini, pasipo kuzungumza kita cha aina yoyote, kiasha akaikoki bastola yake akiziweka risasi zilizopo kwenye magazine yake, kuwa tayari kutoka nje, kitu kikubwa alicho kibakisha ni kuivuta traiga ya bastola yeka kuziruhusu risasi atakazo zihitaji kutoka nje

“Halima unataka kufanya nini?”
“Hastahili kuishi, mtu mwenye ni mfu huyu”
“Hembu ngoja kwanza?”
“Nini?”
“Usimuue?”
“Sasa anabaki duniani wa kazi gani, unamtambua huyu mtu”
Halima alizumgumza kwasauti iliyo jaa msisitizo mwingi
“Hata kama, simfahamu ila kuna kitu ninacho kihisi kwa huyu jamaa”

“Kwanza ametokea wapi?”
“Mimi sifahamu, ila nilisikia kishindo, nilipo kuja hapa ndipo nilipo muona huyu jaamaa akiwa amelala hapa”
Halima pasipo kuuuliza akafyatua baadhi ya risasi, jambo lililo muudhi sana Agnes na kumfanya amsukume Halima na kuangukia pembeni

“Mbona unakuwa mpumbavu wewe, nini unafanya”
Agnes alizungumza kwa hasira huku akimfokea kwa nguvu Halima aliye angukia pembeni, kwa bahati nzuri risasi alizo zifyatua Halima alizipiga pembeni ulipo mwili wa jamaa na hapakuwa na risasi iliyo ingia katika mwili wa mtu waliye muona.

Milio ya risasi ikawastua Fetty pamoja Anna ikawalazimu kutoka nje ya ‘submarine’ na kuelekea sehemu walipo isikia milio ya risasi huku wakiwa makini sana, kila mmoja akiwa ameishika bastola yake mkononi, waakawakuta Agnes na Halima wakiwa wanafokeana huku kila mmoja akionekana kuwa na jazba ya ajabu, Fetty akafyatua risasi mbili hewani nakuwafanya  Agnes na Halima kunyamaza
“Nyingi mumechanganyikiwa?”
Fetty aliuliza kwa sauti juu huku akiwatazama Halima na Agnes

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx