test

Jumamosi, 1 Oktoba 2016

Maalim Seif atua Dar kimyakimya


KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ametua jijini Dar es Salaam kimyakimya ingawa hakutokea kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Buguruni kama ilivyokuwa imetangazwa.

Kufika kwa Maalim Seif katika ofisi za makao makuu Buguruni kulitangazwa juzi na Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Uhusiano wa Umma, Mbarara Maharagande, alipohojiwa na gazeti la Mtanzania na kueleza kuwa atasindikizwa na wabunge wanane wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, mameya na madiwani.
Maharagande alisema Maalim Seif angeripoti Buguruni jana saa 2:00 asubuhi na kupokewa na wanachama wa CUF wa Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia wangewakaribisha wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa waliotarajiwa kuambatana na Seif kutoka Zanzibar walikoketi kutengeneza kile alichokiita mustakabali muhimu wa chama.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx