test

Jumatano, 10 Juni 2015

Nape: Malalamiko ni mengi kwa watendaji wabovu




KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Nape Nnauye, amesema katika ziara zote walizofanya katika kipindi cha miaka mitano bado wananchi wanalalamikia utendaji mbovu kwa baadhi ya viongozi wa serikali.

Kauli hiyo aliitoa juzi Wilayani  Muleba,  alipokuwa akizungumza na wana CCM ambapo alisema watendaji hao wamekuwa wakishindwa kukamilisha miradi ya maendeleo.
 
Alisema katika kipindi hiki ambacho wananchi wanaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu idadi kubwa ya miradi iliyotakiwa kutekelezwa kipindi kilichopita bado haijamilika.

“Muda mwingi ambao tumepita kwa wananchi ili kukagua miradi ya maendeleo tumekuta bado haijakamilika zaidi ya kusikia malalamiko ya wananchi ya utendaji mbovu wa watumishi wa serikali.
 
“... sasa nasema hivi kama wamechoka waondoke, kuna vijana wengi wanataka ajira hatuwezi kuwavumilia watendaji wabovu ambao kila kikucha wamekuwa wakirudisha nyuma miradi ya maendeleo kwa wananchi,” alisema Nape.
 
Alisema kuna watendaji wengine wakiwaona viongozi wanapita kwenye maeneo yao wanakasirika, huku wakishindwa kutoa ushirikiano wa miradi inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Kazi hii ya kukagua miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya nchi, tunayoifanya inawakera baadhi ya watumishi wa Serikali kutokana na kushindwa kuitekeleza kwa kiwango kilichokubalika,"alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo wanapaswa kukubali kukosolewa pale wanapofanya makosa ili waweze kurekebisha makosa yao na kuendelea na majukumu yao.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni