Dakika ya 3 tu Joshua Kimmich aliwanyanyua kwenye viti mashabiki wa Bayern Munich baada ya goli la utangulizi, goli ambalo limemfanya Kimmich kuhusika katika mabao 7 ya Bayern Munich katika CL msimu huu(kafunga 4 na assist 3).
Karim Benzema aliongeza bao la pili dakika ya 46 na hii kuwa mara yake ya kwanza kufunga mabao 2 katika mechi moja ya Champions League tangu afanye hivyo mara ya mwisho mwaka 2014 vs Schalke 04.
James Rodriguez dakika ya 63 aliufanya ubao wa matokeo kusomeka 2-2 na sasa anakuwa mchezaji wa saba katika historia ya Champions League kuwahi kuifungia pamoja na kuifunga Real Madrid, sasa Madrid wanafudhu kwa aggregate ya bao 4-3.

0 comments:
Chapisha Maoni