Waziri
Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema kuwa Iran inawapa Syria
silaha zenye ubora zaidi ambazo nitishio kwa Israel ni vyema kuikabili
Tehran hivi sasa kuliko hapo baadae.
Netanyaju
ameliambia Bunge la nchi hiyo linalokutana Jumapili kuwa “Tunadhamira
ya kuzuia vitendo vya uchokozi vya Iran dhidi yetu hata kama hilo
litakuwa kwa njia ya mapambano. Ni bora hilo lifanyike hivi sasa kuliko
hapo baadae.” Aliongeza: Hatutaki kuongeza mvutano, lakini tuko tayari
kwa hali yoyote.”
Israel imerudia mara kadha kuonya kuwa haiwezi kuvumilia uwepo wa kudumu wa majeshi ya Iran katika nchi jirani ya Syria.
Iran ni mshirika muhimu wa Rais wa Syria Bashar Assad, na imekuwa ikitoa misaada muhimu ya kijeshi kwa majeshi ya Assad.
0 comments:
Chapisha Maoni