test

Jumatatu, 30 Aprili 2018

pika amtaka Waziri Mpango kukutana na Waziri wa Nishati ujadili kusuasua kwa miradi wa REA


Spika wa Bunge, Job Ndugai amemtaka Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kukutana na Wizara ya Nishati ili kujadili kusuasua kwa miradi wa Wakala wa Umeme Vijijini (Rea).

Ndugai ametoa kauli hiyo leo Aprili 30, 2018 baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu bungeni mjini Dodoma kutokana na wabunge wengi kusimama na kutaka kuuliza maswali ya nyongeza, zaidi katika maswali yanayohusu wizara hiyo, wakigusia zaidi kukwama kwa miradi ya umeme vijijini.

“Miradi ya Rea imesimama maana kuna wakandarasi wapo lakini mambo hayaendi, miradi hiyo ndio mkombozi wa Watanzania. Waziri wa Fedha hebu kaa karibu na Wizara ya Nishati katika hili,” amesema Ndugai.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni