test

Alhamisi, 23 Novemba 2017

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kifo cha Mzee Kleist Sykes



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Mzee Kleist Sykes kilichotokea jana tarehe 22 Novemba, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli amesema amepokea taarifa za kifo cha Mzee Kleist Sykes kwa majonzi na huzuni hasa akikumbuka mchango mkubwa alioutoa katika ujenzi wa Taifa akiwa mmoja wa viongozi waliokuwa mstari wa mbele katika kupiga vita umasikini, kuilinda misingi ya uhuru na kujenga uzalendo kwa Watanzania.

Ameongeza kuwa Mzee Kleist Sykes na familia yake walijitoa kwa hali na mali kukijenga chama tangu TAA, TANU na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kushiriki katika harakati kubwa za uhuru, kwa kuweka mbele maslahi ya Taifa licha ya changamoto mbalimbali walizokabilina nazo.

“Mchango wa Mzee Kleist Sykes na familia yake katika nchi yetu hautasahaulika, uzalendo wake utakumbukwa na kudumishwa na hakika kifo chake kimetuachia majonzi na huzuni hasa kwa kuwa kimetokea wakati ambapo busara zake bado zinahitajika”

“Nawapo pole wanafamilia, ndugu, jamaa, wana CCM, marafiki na wote walioguswa na kifo hiki, naungana nao katika majonzi na sala za kumuombea Mzee Kleist Sykes apumzike mahali pepo, Amina”

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

23 Novemba, 2017

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni