test

Jumanne, 27 Juni 2017

SORRY MADAM -Sehemu ya 74 & 75 (Destination of my enemies)



MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
  Hisia za mapenzi zikazidi kupanda kati yao, mikono ya Eddy ikawa na kazi ya kupita kila kona ya mwili wa Phidaya. Kwa nguvu alizo nazo akamnyanyua na kumkalisha kwenye sehemu maalumu ya kunawia mikono. Hapakuwa na mtu aliye kuwa na kipingamizi cha kumpatia mwenzake denda la kutosha.
Kwa haraka Phidaya akaanza kuufungua mkanda wa suruali ya Eddy, hakuishia hapo akafungua na zipu ya suruali hiyo na kiganja chake akakiingiza sehemu lilipo tango lililo simama kidedea.
Viganga vya Eddy vikawa na kazi ya kuyaminya minya mziwa ya Phidaya yaliyo simama vizuri.
“Eddy tizama nyuma yakoooo”
Phidaya alizungumza kwa sauti ya juu huku macho yakimtoka huku kiganja chake akikitoa sehemu lilipo tango la Eddy
 
ENDELEA
Kitendo cha Eddy kugeuka nyuma, akakutana na ngumi nzito iliyo tua usoni mwake na kumfanya apate kizunguzungu cha gafla. Kwa haraka Phidaya akaiweka nguo yake vizuri, huku macho yake yopte yakiwa kwa mwanaume aliye jazia misuli. 
Mwanaume huyo aliye ingia ndani ya choo hicho, kwa lengo la kujisaidia haja ndogo. Ila alipo iona sura ya Eddy, akatambua ya kwamba ndio mtu wanaye mtafuta katika kundi lao lenye watu wengi karibia dunia nzima. Eddy akajaribu kusimama, ila mwanaume huyo aliye na umbo refu kwenda juu na mwenye kifua kilicho gawanyika kwa mazoezi makali aliyo yafanya. Akampiga Eddy teke moja lililo tua kwenye mbavu na kumfanya Eddy kutoa ukelele mkali wa maumivu. 
Phidaya bila ya kujifikiria mara mbili akamrukia mwanaume huyo mgongoni na kunaza kumpiga makofi ambayo kwa ukakamavu wa mwanaume huyo hayakuwa na maumivu ya aina yoyote. Kwa nguvu alizo nazo mwanaume huyo akamshika Phidaya kwa mikono yake yote miwili na kumrushia kwenye moja ya kioo cha ukutani mwa  choo hicho, kitendo kilicho mfanya Phidaya kugugumia kwa maumivu makali huku damu zakimtoka kwenye upande wake wa kushoto ambao alipigizwa kwenye kioo hicho kilicho pasuka.
 
   Mwanaume huyo hakutaka kudili sana na Phidaya, akamsogelea Eddy ambaye anajizoa zoa kunyanyuka kutoka chini. Akamshika kwa mikono yake yote miwili na kumyanyua usawa wake. Akampiga Eddy kichwa kimoja cha uso kilicho mzidisha Eddy kulegea kwa kukosa nguvu. 
Akiwa emeendelea kumshikilia Eddy akamtandika kichwa cha pili cha uso kilicho mfanya Eddy kutulia tuli na kupoteza fahamu. Mwanaume huyo pasipo kuchelewa, akamuweka Eddy begani mwake, akamtazama Phidaya anaye gugumia kwa muamivu makali chini alipo lala. Akataka kutoa bastola na kumpiga Phidaya, ila akamuonea huruma kwa maana si muhusika katika sekeseke hilo.
 
Akafungua mlango wa kutokea kwenye choo hicho. Akachungulia pande zote mbili za kordo hiyo ndefu ila hakuona mtu yoyote akikatiza. Alipo hakikisha usalama upo, taratibu akaanza kutoka na kutembea kwenye kordo hiyo kuelekea nje, huku Eddy akiwa amembeba begani.
 
    Mwaname huyo mwenye asili ya kiarabu, aliye changanyia na asili ya Kirusi(Russia). Akazidi kutembea kwa kwa kujiamini kwenye kordo hiyo hadi akafanikiwa kufika sehemu ya mapokezi ambapo ndipo kuna lango la kutokea kwenye hospitali hiyo. Manesi na watu walipo kwenye eneo hilo, wakabaki wakimshanga mwanaume huyo.
“Samahani muheshimiwa, mtu huyo unampeleka wapi?”
Askari mmoja wa ulinzi wa eneo hilo alimsimamisha mwanaume huyo, aliye mbeba Eddy. 
 
“Ni ndugu yangu nimekuja kumchukua nimrudishe nyumbani”
“Mbona huyo ni mwafrika na wewe si muafrika imekuwaje akawa ni ndugu yako?”
Mwanaume huyo akaka kimya huku akiwatazama askari wawili wanao sogelea eneo hilo, baada ya kumuona mwenzao akimuhoji mwanaume huyo mwaswali. Mwanaume huyo akamtazama askari huyo anaye muhoji maswali anayo hisi yanampotezea wakati. Taratibu akaurudisha mkono wake wa kulia nyuma, ili kuichomoa bastola yake aliyo ifunika na jaketi lake zito.
 
“Ahaaaaaaaaaa bastolaaaaaaa”
Binti mmoja aliye kaa kiti cha nyuma ya jamaa huyo aliweza kuona kitendo anacho taka kukifanya jamaa huyo. Askari wawili ambao wanao mfwata jamaa huyo wakaongeza mwendo huku kila mmoja akijaribiu kuwahi kuichomoa bastola yake kiunoni mwake. Kufumba na kufumbua wakastukia wakitupiwa Eddy, ikawabidi wamdake na wote wakaanguka chini. Askari aliye simama karibu yake aliye kuwa akimuhoji maswali, alistukia akitandikwa teke la sehemu za siri lililo mfanya ajikunje huku akilia kwa maumivu makali sana. 
Askari wengine walipo eneo hilo wakaongezeka kukabiliana na mwanaume huyo, ambaye tayari alisha ichomoa bastola yake na kuanza kukabiliana na askari wanamfwata huku wakiwa wameshikilia mitutu ya bunduki. Watu wote waliopo katika eneo hilo la mapokezi walijikuta wakilala chini huku wachache wakiamua kukimbilia nje kuyaokoa maisha yao.
 
Mashambulizi ya polisi na mwauamue huyo yalizidi kuwa makali, baada ya mwanaume huyo kujibanza kwenye moja ya nguzo iliyopo katika eneo hilo. Iliyo msaidia kukinga risasi zinazo toka kwa askari. Macho ya mwanaume huyo muda mwingi yaliweza kumtazama Eddy aliye lala mita chacha kutoka sehemu alipo jificha na ni ngumu kwa yeye kuweza kumchukua kwa maana akifanya hivyo basi risasi za askari wanao ongeze kila muda basi zinaweza kuishia kwenye mwili wake. 
 
Mwaname huyo aliye fika hospitalini hapo kwa lengo la kumtembelea bibi yeka, aliye lazwa kwenye hospitali hiyo, lengo lake liliweza kuvunjika baada ya kuibanwa na haja ndogo na kuingia kwenye moja ya choo ambacho pasipo kutazama kama kimewekewa tangazo la matengenezo, alijikuta akiingia tu kuitua haja yake hiyo na ndipo hapo alipo weza kumuona Eddy akiwa na Phidaya kwenye choo hicho wakiendelea kuogelea kwenye dibwi zito la mahaba. Alipo hakikisha kwamba mtu huyo ndio wanaye mtafuta baada ya kuiangalia picha ya Eddy kwenye simu yake, ndipo alipo amua kufanya shambulizi lililo mzidi Eddy na kumchukua kiurahisi.
“F……k”
Mwanaume huyo alizungumza huku akimtazama Eddy kwa macho ya hasira. Akachomoa magazine ya bastola yake na kukuta ikiwa imesalia na risasi tano tu na wingi wa askari hao ni mkubwa kuliko wingi wa risasi zake. 
 
“I wiil be back”(Nitarudi tena)
Mwanaume huyo alizungumza huku akijiandaa kukimbia kwa kutokea kwenye moja  mlango mmoja wa kioo uliopo mbele yake. Akaikoki bastola yake vizuri akafyatua risaasi mbili kuelekea walipo askari, kisha akachomoka kwa kasi kubwa, na kuwaacha askari wakifyatua risasi ambazo zote zilipita pembeni. Mwaume huyo akadandia pikipiki yake kubwa aliyo kuja nayo na kuondoka eneo hilo la hospitaloi kwa mwnedo  kasi.
                                                                                                       ***
   Milio ya risasi iliweza kusikika eneo zima la hospitalini. Mlinzi mmoja anaye linda jengo la kuhifadhia maiti(Mochwari). Kwa woga akajikuta akifungua mlango na kuingia ndani ya jengo hilo huku akihema. Kitendo cha mlinzi huyo kuingia ndani ya jengo hilo Shamsa aliweza kuona  sehemu mwanga wa mlango ulipo tokea na mtu huyo kuingia ambaye hakujua kwamba ni nani. Kwa haraka Shamsa akaanza kutembea kwa haraka kuelekea eneo la mlango huku akiomba msaada.
 
Mlinzi huyo akasikilizia sauti ya msichana huyo inayo omba msaada akahisi labda ni wenge la woga wake, kwa maana tangu afanye kazi hiyo ni mwaka wa kumi na mbili hajawahi kusikia wala kuona kitendo kama hicho kilichopo mbele yake. Kwa haraka mlinzi akakimbilia swichi ya kuwashia taa. Kwa haraka akawasha taa, eneo zima la ndani likatawala mwanga.
 
Macho ya mlinzi yakakutana na macho ya Shamsa, ambaye alishuhudia akiingizwa humu ndani maasaa machache yaliyo pita, ikisadikia kwamba amefariki dunia.
“Usinisogelee”
Mlinzi huyo alumuambia Shamsa huku akiwa ameishia bastola yake mkononi na mwili mzima akitetemeka kwa woga.
“Naomba unisaidie kaka yangu”
Shamsa alizungumza huku akiwa amesimama, akifwata amri ya mlinzi huyo anaye onekana kuwa na woga mwingi.
“Wewe umekufa”
“Nimekufa!?”
“Ndio umekufaaa”
 
Mlinzi huyo alizungumza hivyo huku akijikaza tu, ila miguu yake na mikono yake ilionyesha kwamba anashindwa kusimama kutokana na woga mwingi ulio mjaa. Shamsa akatazama eneo alilopo, hapo ndipo akaelewa kwamba sehemu aliyopo ni katika chumba cha kuhifadhia maiti.
“Ahaa……ka…aaka mi sijafaaa”
Shamsa alizungumza huku machozi yakimlenga lenga.
“Tazama viungo vyangu sijafa kabisa, ona niniatembea”
Shamsa akapiga hatua mbili mbele na kiumfanya mlinzi kuishikilia vizuri bastola yake na kumuamrisha tena asimama alipo kwa maana haamini kama Shamsa ni binadamu wa kawaida.
“Ukisogea nakumwaga ubongo zombie mkubwa weee”
Mlinzi huyo alizungumza huku akirudi rudi nyuma kuufwata mlango wa kutokea sehemu ulipo.        
                                                                                                        ***
   Sa Yoo na Raisi Praygod walibiki wakisikilizia milio hiyo ya risasi wakiwa nje ya chumba alicho ingizwa Rahab kwa ajili ya kufanyiwa matibabu. 
“Kumevamiwa”
Raisi Praygod alizungumza huku akihema kwa woga, wakawaona askari kadhaa wakikatiza mbele yao wakikimbilia sehemu kunapotekea milio ya risasi. Sa Yoo baada ya kuona hivyo na yeye akaanza kufwata kwa nyuma.
 
“Wee Sa Yoo rudi hapa”
Raisi Praygod alijaribu kuita ila Sa Yoo tayari alisha fika mbali. Sa Yoo akafika sehemu ya mapokezi. Katika kuangaza angaza Sa Yoo akamuona Eddy akiwa amelala chini akiwa hajitambui. Mapigo ya moyo yakaanza kumenda mbio. Kwani hakujua ni kitu gani kimempata Eddy, kila alivyo tizama jinsi askari wakirushiana risasi na mtu aliye jificha nyuma ya nguzo moja kubwa, huku Eddy akiwa amelala pembeni, alihisi kuchanganyikiwa. 
Akataka kwenda ila risasi moja ikatua karibu na askari aliye kaa naye pembeni na kumfanya askari huyo kudoka chini na kanza kuvujwa damu. Sa Yoo kuona hivyo na yeye akalala chini huku akizidi kuchanganyikiwa. Kitu kilicho zidi kumuumiza kichwa zaidi ni jinsi Eddy alivyo baki katika sura yake ya kawaida na hakuina sura ya bandia ambayo alitengenezewa akiwa Japani.
 
  Sa Yoo akafanikiwa kuweza kumuona mwanaume aliye kuwa akifyatua risasi nyingi, akichomoka kwa kasi na kutoka nje katika eneo hilo. Kwa haraka Sa Yoo akanyanyuka kutoka katika eneo aliko kuwa amelala na kuanza kukimbia kueleka sehemu alipo lala Eddy. Kwa haraka akapiga magoti chini, kuitazama hali ya Eddy. Sa Yoo akaanza kuuchunguza mwili wa Eddy kama umejeruhiwa na risasi, ila hakukuta damu yoyote, ila usoni mwa Eddy kidogo kukawa na mabadiliko. Pua ya Eddy kidogo iliuweza kuvimba hakujua ni nini kilicho ifanya pua hiyo kuvimba. 
 
“Msaadaa jamani”
Sa Yoo alizungumza kwa sauti ya juu. Menesi na madaktari wakaanza kuwashuhulikia askari majeruhi walio jeruhiwa kwa risasi ikiwemo na Eddy. Sa Yoo hakutaka kukaa mbali na Eddy akanza kufwata nyuma kitanda cha matairi alicho lazwa Eddy kinacho sukumwa na manesi wawili.
Eddy akaingizwa kwenye chumba cha huduma ya kwanza, akawekewe mirija ya gesi puani mwake. Sa Yoo hakuruhusiwa kuingia kwenye chumba hicho.
“Madam Phidaya”
 
Sa Yoo alikumbuka huku akiangaza macho yake huku na kule, hakujua ni wapi alipo. Kumbu kumbu ya mwisho aliyo ikumbuka ni jinsi Eddy alivyo ondoka na Phidaya huku akimburuta kutoka katika eneo la ugomvi.  Kwa haraka Sa Yoo akaanza kutembea kuelekea katika sehemu ambayo walimiucha madam Mery. Hakutumia dakika nyingi akawa amesha fika katika eneo hilo ambapo akamkuta Madam Mery akiwa amejiinamia kwenye kitia alicho kaa.
“Madam Mery umemuona wapi Madam Phidaya?”
Sa Yoo aliuliza swali ambalo fika alitambua kwamba hato jibiwa sahihi. Madam Mery akanyanyua sura yake na kumtazama Sa Yoo kisha akajibu kwa kutingisha kichwa kwamba hatambui ni wapi alipo.
 
“Mungu wangu, sasa itakuwaje?”
Sa Yoo alizungumza huku jasho likimwagika. Madam Mery akamtazama Sa Yoo usoni mwake na kutambua kuna kitu ambacho kinaendelea kwa maana sura yake imejawa na masha makubwa sana.
“Kuna nini kimetokea?”
“Eddy amevamiwa na majambazi”
“Ehheee……..!!?”
Madma Mery alishaanga huku akisimama kwenye kiti, habari hiyo fika ilionyesha kumstua sana Madam Mery.
“Yuu…….uuuu..po wapi Edddy”
“Yupo wodini anashuhulikiwa, hapa ninamtafuta madam Phidaya”
 
Kutokana na mawazo mengi Madam Mery aliisikia miliio ya risasi ila hakujishuhulisha nayo, alihisi labda ni mawazo yake ndio yanayo mtuma hivyo.  Sa Yoo akaitazama korodo ambayo Eddy na Phiday waliondoka pamoja. 
Bila hata ya kuuliza akaanza kutembea kwa mwendo wa haraka kuifwata kordo hiyo iliyo ndefu na iliyo tulia, huku  madam Mery naye akifwata kwa nyuma. Wakapita kwenye mlango wa choo, kilicho wekwa tangazo kwamba kipo katika matengenezo. Sa Yoo hakukitilia maanani sana, hatua mbili mbel, akasikia sauti ya mtu akigugumia kwa maumivu kutoka katika choo hicho.
 
“Vipi?”
Madam Mery aliuliza baada ya kumuona Sa Yoo akisimama na kugeuka nyuma. Sa Yoo hakujibu chochote zaidi ya kuanza kurudi taratibu huku masikio yake yote na macho akiwa amevielekezea inapo tokea sauto hiyo. Akautazama vizuri mlango wa kuingilia chumba hicho, akakuta ukiwa wazi kidogo, taratibu akausukuma na kuingia ndani. Hakuamini macho yake baada ya kumkuta Phidaya akiwa amekaa kitako akijitahidi kunyanyuka. Vipande vya vioo vilivyo anguka chini vilizidi kumkata kata Phidaya pale alipo jaribu kuweka mikono yake chini ili anyanyuke.
 
“Madam”
Sa Yoo alizungumza huku kwa haraka huku akimfwata Phidaya. Kwa kusaidiana na Madam Mery wakamnyanyua.
“Eddy ametekwa jamani”
Phidaya alizungumza kwa shinda huku akimtazama Sa Yoo usoni.
“Yupo yupo tayari amesha okolewa na polisi”
Sa Yoo alijibu kwa haraka. Madam Meri aliweza kuiona sura ya bandia ya Eddy aliyopo juu ya sinki la kunawia mikono. Akaiokota kisha wakatoka katika choo hicho. Madam Mery hakujali tofauti zilizopo kati yake na Phidaya. Moja kwa moja wakaeleka katika chumba ambacho Eddy anapatiwa huduma ya kwanza. Manesi wakampokea na Phidaya, wakaanza kumshuhulikia.
                                                                                                               ***
“Samahani kaka usitoke, mimi sio Zombi”
Shamsa alizungumza huku akizidi kumfwata mlinzi aliye simama karibu na mlangoni. Mlinzi akazidi kutetemeka hadi bastola ikamdondoka chini. Ikawa ni nafasi nzuri kwa Shamsa kutembea kwa mwendo wa haraka hadi karibu kabisa na mlinzi huyo, kitendo cha kumshika mlinzi huyo aliye toa macho kwa woga. Mlinzi akaanguka chini na kupoteza fahamu.
 
Shamsa akashangaa sana, hakutaka kupoteza muda akamfungua mlango na kutoka eneo hilo. Milio ya risasi ikamfanya agundue kuna tatizo katika eneo hilo  la hospitalini kwa haraka akaanza kutembea kueleka inapo tokea milio hiyo ya risasi ili kuweza kujua ni nini kitanacho endelea.
 
Akafika karibu na lango la kuingilia katika eneo la mapokezi, ila mwanaume mmoja mrefu akachomoka kwa kasi na kudandika pikipiki na kuondoka kwa kasi. Akabaki kumshangaa mwanaume huyo anavyo tokomea kwenye geti la kutokea katika eneo la hospitali. 
Mwanaume huyo anaye onekana kuto kuwa na huruma, alimbabiza teke moja mtoto mmoja mlemavu wa miguu  anaye tumia kiti cha magurudumu kutembelea, akaangukia pembeni na mwanaume huyo akapita kwa kasi. Kitendo hicho kikamkera sana Shamsa na kuanza kukimbilia sehemu alipo angukia mototo huyo.
“Umeumia?”
 
Shamsa alimuuliza mtoto huyo hakujibu kitu chochote zaidi ya kugugumia kwa maumivu makali aliyo yapata. Kwa haraka Shamsa akamnyanyua mtoto  huyo na kumuweka kwenye kiti chake. Akatoka nje ya geti hilo huku akiwa anakimbia akamuona mwanaume aliye fanya tukio hilo akikatiza kwenye moja ya barabara. Katika kuangaza angaza macho upande wa pili akaona sharobaro mmoja akishuka kwenye moja ya pikipiki kubwa na nzuri ya kifahari na kuingia dukani. 
Kwa kasi Shamsa akakatiza kwenye barabara hiyo, akaifikia pikipiki hiyo kwa bahati nzuri akakakuta funguo ikiwa juu ya pikipiki hiyo. Kwa haraka akaidanda pikipiki hiyo na kuondoka eneo hilo kwa kasi na kumfanya sharobaro huyo kutoka nje ya duka hilo kushuhudia pikipiki yake inavyotokomea, kitendo kilicho mfanya amwagikwe na machozi.
 
Kwa bahati nzuri Shamsa akafanikiwa  kumuona mwanaume huyo kwa mbali akizidi kutokomea katikati ya barabara yenye magari mengi yanayo kwenda kwa kasi. Kitu kilicho mfanya Shamsa kuzidi kuongeza mwendo kasi wa pikipiki yake na kuzidi kumsogelea mwanaume huyo ambaye bado hajafahamu ni nini alicho kitenda ndani ila kwa kitendo alicho mfanyia mtoto mlemavu  akaapa ni lazima amtie mikononi mwake na alipe kwa kitendo hicho.
                                                                                                          
   SORRY MADAM (75)  (Destination of my enemies)
 
Shamsa akajaribu kadri ya uwezo wake kumfukuzia mwanaume huyo ila, akashindwa kutokana na msongamano wa magari kuwa mengi na kitu kingine kilicho mfanya kumpoteza mwanaume huyo ni pale magari ya upande wake yalipo simamishwa na taa za barabarani zinazo ongoza magari hayo.
 
“Shitiitiiii”
Shamsa alizungumza huku akigeuza na kupita barabara nyingine kurudi hospitalini. Safari haikumchukua muda mwingi akwa amefika hospitalini. Lengo la yeye kufika hapo ni kutaka kujua ni kitu gani kilicho sababisha hadi akapelekwa katika jengo la kuhifadhia maiti. Hali ya ukimya na ulinzi mkali aliyo ikuta mapokezi, haikumshangaza sana kwa maana naye aliweza kuisikia miliyo ya risasi.
“Samahani nesi?”
Alimuuliza nesi mmoja aliye kaa kwenye moja ya dirisha la mapokezi.
“Bila sahamani?”
“Kuna jambo ambalo linanichanganya kidogo?”
“Jambo gani?”
Shamsa akaka kimya huku akipangilia ni kitu gani atamuelezea nesi huyo hali ambayo imetokea. Ila kabla hajazungumza kitu cha aina yoyote akastukia akishikwa bega kwa nyuma.
                                                                                                                ***
    Eddy akazinduka kutoka katika usingizi mzito alio kumbana nao kwa kipigo alicho pigwa na mwanaume ambaye hakumtambua. Macho yake yakaangaza chumba kizima. Akamuona Sa Yoo akiwa amesimma pembeni yake huku Phidaya akiwa amekaa kwneye moja ya kiti akiwa amefungwa bandeji. Akageuka upande wa pili akamuona Madam Mery akiwa ameegemea ukuta.
“Vipi?”
Eddy alimuuliza Sa Yoo aliye tazamana naye.
“Safi unajisikiaje?”
“Ahaaa kichwa kinaniuma”
Taratibu Phidaya akanyanyuka kutoka katika kiti alicho kaa na kupiga hatua hadi kitandani na kukaa pembeni mwa kitanda.
 
“Honey pole”
“Asante mke wangu, vipi umeumia sana?”
“Hapana ni chupa chupa ndio zimenichoma kwenye mkono”
“Pole”
Taratibu Phidaya akainama na kumbusu Eddy mdomoni kwa mahaba makubwa sana.
“Muheshimiwa raisi yupo wapi?”
“Ahaa ngoja nikamtazame kwenye wodi alipo lazwa Rahab?”
Sa Yoo baada ya kuzungumza hayo akatoka ndani ya chumba hicho na moja kwa moja akaelekea hadi kwenye wodi aliyo lazwa Rahab, akamkuta Raisi Praygod akimsaidia Rahab kukaa kitako kwenye kitanda.
 
“Madam Rahab umeamka?”
“Ndio, vipi Eddy yupo wapi?”
Swali la Rahab kumuulizia Eddy likamfanya raisi Praygod kuguna kimoyo moyo, kwa maana alihisi labda mke wake atafurahia uwepo wake hapo.
“Eddy naye yupo kwenye wodi amelazwa?”
“Amelazwa?”
“Ndio, alivamiwa na jambazi ambaye hajulikani?”
“Mmmm, ilikuwaje akavamiwa?”
“Hata mimi sifahamu, ila amesha ivua sura ya bandia aliyo kuwa anaitumia”
“Akhaaaa, hembu naomba viatu vyangu hapo”
Rahab alimuagiza Sa Yoon aye akafanya hivyo.
“Baby unataka kwenda wapi?”
“Ninakwenda kumuona Eddy”
“Hali yako haipo vizuri mke wangu, jaribu kutulia japo kidogo upate nguvu”
 
“Hapana honye mbona nina nguvu tu za kutosha”
Rahab alizungumza huku akivaa viatu vyake. Akasimama wima, akajiweka sawa nguo zake, akapiga hatua na kufungua mlango, akatoka na kuwaacha Sa Yoo na raisi Praygod wakifwata kwa nyuma. Ikafika sehemu Rahab akasimama kwa maana hakujua ni wapi alipo lazwa, ikamlazimu Sa Yoo kuwaongoza hadi kwenye chumba alipo Eddy. Wakamkuta akisaidiwa na Phidaya kuvalishwa shati alilo kuwa amevuliwa alipo kuwa akipatiwa huduma ya kwanza.
Rahab akaachia tabasamu pana baada ya kumuona Eddy akiwa katika sura yake ya halisi. Taratibu akasogea hadi kitandani, akamkumbatia Eddy kwa sekunde kadhaa kisha akasimama wima.
“Kimetokea nini?”
 
“Daa sielewi yaani, nihisi kuna watu wanao nifwatilia?”
Eddy alizungumza kwa sauti iliyo poteza uchangamfu kabisa.
“Hao wana kufwatilia ni D.F.E’s”
Madam Mery alizungumza na kuwafanya watu wote ndani ya chumba hicho kumgeukia na kumtazama kwa umakini.
“Ndio nini hiyo D.F.E?”
Raisi Praygod aliuliza huku akimtumbulia macho Madam Mery
“Si vyema kuweza kutoa ufafanuzi, hapa tulipo kwa maana sio sehemu salama tena na tukiendelea kubaki hapa ninaamini shambulio jengine linaweza kutokea muda wowote”
 
Kila mmoja aliyesikiliza maneno ya madam Mery kwa umakini, wasiwasi ukaanza kuwatawala kila mmoja, hususani Phidaya, ambaye kwa haraka akaanza kuvuta kumbukumbu, siku ambayo aliweza kushika waleti(pochi) ya aliye kuwa mume wake dokta Ranjiti na kukuta kitambulisho kilicho kuwa kimefichwa ndani kabisa ya waleti hiyo. 
Kitambulicho hicho kiliweza kuonyesha jina sahihi la dokta Ranjiti pamoja na jina la kundi hilo. Alipo jaribu kumuuliza dokta Ranjiti kuhusiana na kitambulisho hicho hakupata jibu lolote la maana zaidi ya dokta Ranjiti kumpokonya na alionekana kuwa na hasira sana.
 
‘Sinto hitaji uniulize swali lolote kuhusiana na D.F.E tena’
Maneno hayo ya dokta Ranjiti, Phidaya aliweza kuyakumbuka vizuri kichwani mwake. Phidaya akashusha pumzi nyingi huku akimtazama madam Mery usoni.
“Jamani tuondokeni”
Phidaya alizungumza huku akisimama, na kuwafanya watu wote kumshangaa.
“Ngoja nisubirie ruhusa ya madaktari mke wangu?”
“Baby hii sehemu sio salama kwa ajili yako na mimi pia?”
“Madam Phidaya kwa nini unaseme hivyo?”
 
Sa Yoo aliuliza huku akiwa amemkazia jicho Phidaya.
“Sina cha kujibu kwa sasa, ila Eddy kama unanipenda ninakuomba sana tutoke hapa”
“Je mwili wa Shamsa tutakwenda kuuona saa ngapi?”
Eddy aliuliza huku akishusha miguu chini kutokea kitandani.
“Hata kesho tutakuja kuuchukua, muda umesha kwenda, na jinsi tunavyo zidi kukaa hapa ndivyo jinsi tutakavyo zidi kupatwa na matatizo”
Phidaya aliendelea kusisitiza kwa umakini huku mapigo ya moyo yakizidi kumuenda kasi. Eddy akavaa viatu vyake. Alipo hakikisha kwamba yupo sawa wakatoka kwenye chumba hicho.
                                                                                                                   ***
“Yassin ni nini kimetokea mbona mbio mbio hivyo”
Khalid alimuuliza Yassin baada ya kuingia sebleni hapo akiwa anamwagikwa na jasho. Yassin akatazama vijana wake wapatao sita walio jiachia kwenye masofa wakitazama mpira.
 
“Zimeni Tv kuna kazi nahitaji sasa hivi tukaifanye na laity tukishindwa kuifanya sasa hivi nitakosa pesa nyingi sana”
Kutokana Yassini ndio bosi wao na ndiye anaye waongoza katika kazi zote haramu wanazo zifanya zinazo waingizia pesa. Hapakuwa na aliye weka kipingamizi kila mmoja akasimama kutoka kwenye sofa alilo kali. Yassin akasimama katikati ya sable na kuwaomba wamsogelee. Akatoa simu yake mfukoni na kuwaonyesha picha ya Eddy, ambaye alishindwa kuondoka naye hospitalini baada ya polisi kumshinda nguvu.
“Tunatakiwa huyu kumkamata, namuhitaji mzima”
“Bosi anaitwa nani?”
 
“Anaitwa Eddy, ni Mtanzania. Ila hicho si kitu cha kukiangalia kwa sasa. Kitu ninacho kitaka ni kwenda hospitali ya Dellhan kumchukua kwani nina imani atakuwa bado anahudimiwa kwenye hospitali hiyo”
“Sawa bosi”
“Dulla andaa magari mawili, na kila mmoja achukue risasi za kutosha kwa maana nilisha sababisha huko na ulinzi wa askari wa polisi upo vizuri sana”
“Bosi nina wazo?”
“Wazo gani?”
“Kama umetoka kusababisha, basi unaonaje tukavalia mavazi ya polisi na tukaendea pale kama polisi wa kitengo maalumu, na itatuwia urahisi kuweza kufahamu ni wapi alipo lazwa Eddy na tukamchukua kiulaini kabisa pasipo kutumia silaha”
 
“Wazo  zuri Khalid. Nguo na vitambulisho vyote view tayari. Asmah, wewe huto valia mavazi ya askari. Valia suruali ya suti pamoja na shati yeupe. Ila hakikisha kwamba unavalia jaketi la kuzuia risasi sawa”
“Sawa mkuuu”
“Haya tawanyikeni dakika tano za kujiandaa. Picha ya huyu mtu nitaituma kwenye kila simu ya mmoja wetu hakikisheni munaikariri sura yake vizuri. Sihitaji uzembe kazini”
 
“Sawa mkuu”
Kila mmoja akatawanyika na kuingia kwenye chumba chake. Huku Yassin naye akiingia kwenye chumba chake na kuanza kujiandaa, huku sura yake akibandika ndevu ndogo za bandia chini ya kidevu chake ili kubadilisha muonekano wake. Pesa ambayo anaivuna kutoka D.F.E pamoja na matukio mengi ya kiharamu. Yassin huitumia pesa hiyo kuimarisha kikosi chake chenye vijana watano huku mwanamke akiwa mmoja na mwenye uwezo mkubwa katika kupambana hata na wanaume kumi na anawaangusha chini ndani ya muda mchache. Vii faa vingi anavyo vinunua ikiwemo mavazi ya polisi pamoja na magari ya polisi, vinamsaidia sana kufanya kazi yake kwa usahihi mkubwa pasipo kustukiwa hata na polisi wenyewe.
 
   Ndani ya dakika tano alizo waamuru vijana wake kuweza kuzitumia, akawa amemaliza kazi yake na kutoka chumbani kwake. Akawakuta vijana wake wakiwa sebleni kila mmoja akiwa amesha jiandaa.
“Bosi gari zipo tayari”
“Tutagawanyika katika makundi mawili. Asmah, utakuwa name Mudathiri utakuwa na Khalid. Mulio salia mutajigawa sawa”
 
“Sawa mkuu”
“Kumbukeni, tunakwenda hospitalini. Kazi inayo tupeleka pale ni mtu mmoja tu na si mwengine. Narudia tena sinto hitaji makosa ya kizembe”
Wakatoka, jinsi walivyo jigawa ndivyo jinsi walivyo ingia kwenye magari mawili ya polisi ambayo wamepanga kuyatumia katika kazi iliyopo mbele yao. Safari ikaanza kuelekea hospitalini huku kila mmoja akiwa ameishika simua yake na kurudia kuitazama sura ya Eddy kwa mara nyingine.
                                                                                                           ***
     Wakafika mapokezi, Eddy akajikuta akishangaa hali ya hapo mapokezi kwani, ulinzi ni mkali sana na kunaonyesha kuna tukio ambalo limetoka. 
 
“Kumetokea nini?”
Eddy aliuliza na Sa Yoo akadakia kumjibu.
“Yule jambazi aliye kuteka, alizuiliwa hapa na askari na ndio akakucha hapa baada ya kuzidiwa na yeye akaondoka”
Sa Yoo alizungumza huku akitazama tazama eneo zima, la hapo mapokezi ambalo ni kubwa sana. Macho yake yakautua kwa mtu aliye simama kwenye moja ya dirisha. Moyo ukaanza kumdunda, akataka kutoka nje, ila akasimama.
“Naomba munisubiri”
Sa Yoo alimuambia Eddy na Phidaya ambao anatembea nao karibu, huku madam Mery, raisi Praygod na Rahab tayari walisha toka.
 
“Unakwenda wapi?”
“Nakuja naomba munisubiri hapo nje”
Sa Yoo hakutaka kumueleza mtu yoyote kitu anacho taka kukifanya. Eddy na Phidaya wakatoka nje, Sa Yoo akaaza kutembea kwa mwendo wa wasi wasi kuelekea kwenye dirisha moja la mapokezi. Kila jinsi alivyo zidi kupiga hatua ndivyo woga ulivyo zidi kumtawala. Akamkaribia mtu aliye kusudia kabisa kumtazama kwamba ni yeye au laa. Bila kusita akamgusa begani na mtu huyo akageuka.
“SHAMSAAAAA…………!!?”
Sa Yoo aliita kwa mshangao mkubwa kiasi cha kumfanya hadi nesi kushangaa. Shamsa kumuona  Sa Yoo, akajikuta akipatwa na kugugumizi. 
 
“Sa…aaa Y…OO”
Wakatazama kwa sekunde kadhaa huku kila mmoja akionekana kuto mtarajia kumuona mwenzake katika sehemu hiyo hususani Sa Yoo ambaye anaamini kwamba rafiki yake huyo amesha fariki dunia. Wakakumbatiana kwa pamoja huku machozi yakiwamwagika.
“Nimeambiwa umekufa”
Shamsa hakujibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kumwagikwa na machozi. Sa Yoo akamuachia Shamsa kidogo na kumuangalia vizuri, akahakikisha kwamba huyu ni Shamsa, kwa maana hata nguo alizo vaa ndio nguo alizo vaa jana usiku.
“Tuondoke rafiki yangu tunasubiriwa huko nje”
“Na nani?”
 
“Wewe twende, tu utawaona”
Shamsa hakuwa na kipingamizi cha aina yoyote ziadi ya kukubaki kuondoka na Sa Yoo. Wakatoka nje ya hospitali na kuelekea katika sehemu ambayo wapo Eddy na wezake. Kila walivyo zidi kulikaribia eneo walipo simama Eddy na wezake, ndivyo jinsi kila mtu alibaki akishangaa, kumuoan Sa Yoo akija na Shamsa eneo hilo. Wakafika eneo walipo simama.
“Shamsa?”
Eddy aliita huku macho yakimtoka, hakuamini anacho kiona mbele yake. Phidaya akamuachia Eddy mkono na kumsogelea Shamsa, ambaye naye alibaki akimshangaa Phidaya. Wakatazamana kwa sekunde kadhaa na kukumbatiana huku wote wakilia kwa furaha.
 
“Mama nimekumsi”
“Hata mimi pia mwanangu”
Phidaya alizungumza huku akizidi kumkumbatia Shamsa. Wakiwa katika hali bado ya kushangaa, madam Merya akaona gari mbili za polisi zikisimama katika maegesho yaliyopo mbele yao. Wakashuka watu sita kwenye gari mbili hizo. Kwa haraka madam Mery akamkumbatia Eddy na kumgeuza upande mwengine na kuanza kumnyonya denda huku viganja vyake vyote viwili vikiufunika uso wa Eddy na kuzidi kumnyonya denda Eddy pasipio kumuhofia mtu wa aina yoyote. Shamsa akalishuhudia tukio hilo na kumuonyesha Phidaya kitua anacho kifanya Madam Mery, jambo lililo ipandisha hasira ya Phidaya mara dufu na kuanza kuwafwata madama Merry na Eddy sehemu walipo simama.
==>ITAENDELEA...

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni