test

Jumapili, 2 Aprili 2017

SORRY MADAM -Sehemu ya 45 & 46 (Destination of my enemies)



MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
Makachero wanao uongoza msafara huo wakashuka kwenye magari yao kila mmoja akiwa na bastola iliyo jaa risasi mkononi mwake. Wakatembea kwa tahafhari kubwa wakijaribu kuchunguza kila sehemu ya msitu huo kwa umakini wa hali ya juu. Umakini wao ulizidi kuongezeka kwani wana kiongozi wao mkubwa wa nchi. Wakafika hadi eneo la handaki. Makachero wawili wakaingia ndani ya handaki hilo. Gafla milio mingi ya risasi ikasikika ndani ya handaki hilo jambo lililo wachanganya raisi na watu wake walio baki nje ya handaki.

ENDELEA
   Milio hiyo ya risasi ikawafanya makachero wengine kumzunguka raisi Praygod Makuya kuzuia hata kama kuna tatizo baya litatokea waweze kumlinda. Ikawalazimu makachero wawili kuingia katika handaki bastola zao zikiwa mikononi mwao. Cha kushangaza wakawakuta wezao wakiwa wamesimaa huku wanatetemeka mithili ya watu walio mwagiwa maji ya baridi  na kusimamishwa kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.
 
Wakajaribu kuwauliza kwa ishara ni kitu gani kimepelekea hadi wakawa wanafyatua risasi ovyo ovyo. Ila hakuna aliye weza kutoa jibu kati yao zaidi ya wao kuendelea kutetemeka.  Ikawalazimu wezao hao wawili kuanza kutembea taratibu ndani ya handaki hilo kuchunguza ni nini ambacho kimetokea. 
Wakaingia kwenye moja ya chumba ambapo cha kwanza kukutana nacho chini ni damu nyingi za mwanadamu. Katika kupitisha pitisha macho yao huku na huku. Wakamkuta mke wa raisi akiwa amelala juu ya kitanda huku damu nyingi zikiwa zinamwagika mwilini mwake, akikaribia kuiaga dunia.
 
 ***
 Kitu kisicho onekana kikazidi kuwateketeza makachero walio mshambulia Priscar hadi wote wakafa.
Katika hali ya kumshangaza Priscar akajikuta akivutwa nje ya gari na kulazwa pembeni pasipo kumuona mtu anaye mfanyia mambo yote hayo. Jeraha la risasi iliyo mpiga ndani ya dakika moja likawa limekauka na mwili wake ukarudi katika hali yake ya kawaida.
“Wewe ni nani unaye nifanyia haya yote”
Ilimbidi Priscar kuuliza kwani hisia za kusnikwa na mtu huyo asiye oenekana kwenye mwili wake mara kadhaa, anazihisi ila tatizo ni mboni zake za macho haziwezi kumuona mtu huyo. 
Hakuna ambacho aliweza kuambulia kujibiwa. Gari lake ambalo limeingia kwa nyuma ndani ya mtaro akashangaa likisitolewa taratibu na kusimamishwa barabarani. Kisha akajikuta akishikwa mkono wa kulia akikokotwa hadi kwenye mlango wa kuingilia ndani ya gari hilo. Mlango ukafunguliwa bila hata ya kupenda akajikuta akinyanyuliwa na kuingizwa kwenye gari na kukalishwa kwenye siti ya dereva. 
Akafungwa mkanda, gari ikawashwa na mikono yake ikashikishwa kwenye mskani wa gari hiyo na mlango ukafungwa. Ikiashiria aondoke katika eneo hilo haraka iwezekanavyo kwani kuna gari baadhi za polisi zinakuja kuwapa nguvu makachero wanao pambana na mtu aliye hitaji kuuvamia msafara wa raisi.
 
 ***
Dokta akamuachia simu Shamsa kisha yeye akazidi kusonga mbele. Kulifwata gari lililo kosa kosa kuwagonga.  Shamsa kabla hajafika hatua nyingi simu hiyo ikaita kuangalia vizuri akakuta ni jina la baba yake, hakuona haja ya kuelekea anapo kwenda dokta wake. Akaipokea na kuiweka sikioni mwake.
 
“Baba habari”
“Ohoo Salama binti yangu, mumefika salama”
“Ndio baba hapa tumefika hospitalini”
“Mbona unazungumza kwa furaha sana?”
“Hpana baba kidogo nimebadilisha mazingira, kidogo ninafurahi sana”
Shamsa akiendelea kuzungumza na simu tayari dokta wale alisha fika kwenye  gari na kukutana na binti anaye mfahamu akitokea ndani ya gari hilo huku akimwagikwa na machozi.
“Sa Yoo unatatizo gani?”
Daktari alimuuliza huku  hasira yake ikiwa imebubujika kifuani mwake mithili ya barafu la maji liwekwapo juani
“Bibi yangu hali yake ni mbaya”
 
Dokta baada ya kusikia hiyo na kutokana anamfahamu vizuri binti huyo pamoja na bibi yake ambaye pia alisha wahi kumuhudumia katika maswala ya saikolojia, hakuwa na budi zaidi ya kuondoka na Sa Yoo wakielekea ndani. Wakaungana na Shamsa kuingia ndani ya hospoitali hiyo pasipo Eddy kumjua binti wa tatu anaye ingia na kina Sa Yoo ni nani, kwani binti huyo ameziachia nywele zake ndefu kwa nyuma nakuizuia sura yake kuweza kuonekana vizuri kwa mbele
 
Kutokana na uhalifu alio ufanya Eddy, ikamuwia ugumu kushuka ndani ya gari kuhofia kuingia mikononi mwa polisi, moja ni lazima astakiwe kwa kusa la kuwapiga polisi, mbili ni lazima atakabidhiwa katika ubalozi wa Tanzania aweze kurudishwa Tanzania, jambo ambalo hakuhitaji kuweza kulisikia kwa wakati huo.
Sa Yoo na daktari wakakimbilia kwenye  chumba cha wagonjwa mahututi huku wakimuacha Shamsa akiwa amekaa sehemu maalumu ya mapokezi akimsubiria mwenyeji wake afike. Shamsa akaitumia nafasi hiyo kuweza kumfikiria ni wapi ambapo anaweza kumpata Eddy. 
Mwanaume anaye muheshimu kama baba yake, wazo la kurudi kwenye familia ya magaidi wa Al-Shabab likaanza kumpotea taratibu kichwani mwake, akaanza kufikiria kuungana tena na Eddy ambaye aliamini kwamba amekufa na hilo ndio jambo ambalo lilimfanya akubali kurudi katika familia ya Al-Shabab watu walio muulia wazazi wake baba na mama akiwa mdogo kisha akachukuliwa mateka na kuwa miongoni mwa askari wakikosi  hicho akiwa mdogo sana.
“Nilazima niwaue Al-Shabab wote”
Shamsa alizungumza huku picha ya askari wa kikosi hicho ikiwajia jia kichwani mwake. Hasira dhidi ya kikosi hicho ikazidi kumpanda moyoni mwake hadi mwili mzima ukaanza kumtetemeka.
 
Kwa kupitia kioo cha pembeni cha gari alilomo Eddy, akaona gari mbili za polisi zikija katia maeneo ya maegesho ya hospitalini hapo. Wasiwasi mwingi ukazidi kumpanda, akataka kushuka na kukimbia akaoona itakuwa ni hatari sana kwake na itakuwa ni rahisi kwa yeye kuweza kukamatwa na askari hao. Gari hizo zikazidi kulisogelea gari ambalo Eddy yupo, kwa haraka ikamlazimu kuweza kuinama ndani gari hilo ili asiweze kuonekana.
Gari hizo za polisi zikasimama karibu kabisa na gari alilopo. Wakashuka askari wanne walio valia nguo nyeusi huku viunoni mwao wakiwa wamening’iniza pingu pamoja na kuchomeka bastola zao zilizomo kwenye vifuko maalumu vya kuchomekea bastola.
 
   Askari hao wakatizama tizama kila sehemu ya maegesho ya magari hayo wakionekana kwamba kuna gari wanaitafuta, mmoja wao akaanza kupiga hatua za kulifwata gari hilo taratibu huku akijaribu kutazama namba ya usajili ya gari hilo kwani ni gari lililo mbebea muhalifu anayetafutwa ndani ya Japan nzima.
                                                                                              ***
  Miliyo ya risasi ilipo kata ndani ya handaki makachero wote walio nje ya handaki wakiongozwa na raisi Praygod wakaingia ndani huku wakionekana kuwa na shauku kubwa ya kujua ni kitu gani kinacho endelea ndani ya handaki. Wakawakuta makachero wa kwanza wakiwa hai huku wamesimama, hata kabla hawajawauliza wakawaona makachero wengine  wakitoka ndani ya chumba kimoja huku wakiwa wamembeba Rahab anaye endelea kuvujwa na damu nyingi.
Ikabaki nusu Raisi Praygod kuchanganyikiwa baada ya kumuona Rahab akiwa katika hali hiyo. 
 
“Ah…aaa aahme faafaanyaa nini mke wangu”
Raisi Praygod aliuliza huku mwili ukimtetemeka, makachero walio tangulia kuingia ndani ya handaki hilo wakakosa jibu la kuzungumza na fika wanatambu kwamba wao ndio wameusika katika kumpiga risasi Rahab baada ya Rahab kuanza kufanya jaribio la kuwashambulia makachero hao ila akashindwa na kujikuta akipigwa risasi kadhaa zilizo mfanya kuingia ndani ya chumba huku hali yake ikiwa mbaya sana.
Kutokana hapakuwa na jibu kwa makachero hao, raisi Praygod akatoa amri ya mke wake awaishwe mara moja kwenye gari wampeleke hospitali.
 
Safari ya kurudi jijini Dar es Salaam ikaanza huku gari hizo zikiendeshwa kwa mwendo kasi. Ndani ya dakika arobaini na tano wakawa wameingia ndani  ya hospitali ya taifa muhimbili huku hali ya raabu kizidi kuwa mbaya kila jinsi dakika zilivyo zidi kwenda.
Madaktari wakaanza kazi ya kumuhudumia mke wa raisi, raisi Praygod akashindwa kuyazuai machozi yake.kumwagika. Hakujali kama ni kiongozi wa nchi alicho kihitaji kwa wakati huo ni kusikia mke wake anaendelea vizuri.
 
Madaktari ndani ya chumba cha upasuaji wakafanikiwa kutoa risasi zote sita zilizo ingia ndani ya mwili wa Rahab.
“Dokta…….”
Nesi mmoja alimuita daktari kiongozi wa opereshini hiyo, macho yao wote yakatua kwenye mwili wa Rahab, hapakuwa na mtu aliye weza kuamini kitu walicho kiona, woga kati yao ukazidi kutawala madaktari wote sita pamoja na nesi mmoja waliomo ndani ya chumba hicho.  Vidonda vilivyo kuwa kwenye mwili wa Rahab vilijiziba na kurudi katika hali ya kawaida.
 
Kitendo cha Rahab kuyafumbua macho yake yaliyo mekundu mithili ya damu kikawafanya madaktari wpte waliomo ndani ya chumba kuanza kukimbilia mlangoni, kila mmoja akijaribu kuyaokoa maisha yake. Hadi wanafika mlangoni tayari Rahab alisha simama wima na kuchomo sindano zote za madripu zilizo kuwa zimechomwa mwilini mwake. Kila walipo jaribu kuufungua mlango haukufunguka na taa zilizomo ndani ya chumba hicho zikaanza kufifia na kigiza cha mbali kikaanza kutawala ndani ya chumba.
 
***
   Njia nzima Priscar akajikuta akijiuliza maswali ni kitui gani kilicho weza kutoke katika muda mchache uliopita. 
 
“Au naota?”
Swali hilo alilipatia jibu akilini mwake kwamba kila kitu kinacho tokea kwa wakati huo si ndoto bali ni hali alisi inayo jitokeza.
“Madam”
Priscar aliwaza sehemu alipo mucha Rahab, ikamlazimu kuongeza mwendo kasi wa gari lake kuelekea nje ya jiji la Dar es Salaam. Hadi anafika katika maeneo ya hamdaki ikamlazimu kusimaisha gari lake mbali kidogo na sehemu na lilipo hamdaki, akashuka na kuanza kukimbia kuelekea sehemu ya handaki, kabla hajalifikia akasikia milio kadhaa ya risasi ikirindima ndani ya handaki hilo. 
Alipo chunguza vizuri akaziona gari za ikulu zikiwa zimesimama nje ya handaki hilo, huku Raisi Praygod akiwa wamezungukwa na walinzi wake. Baada ya milio ya risasi kunyamaza akawashuhudia walinzi hao wakiongozana na raisi wakiingi ndani ya handaki hilo. Baada ya dakika tano mbeleni akawaona wakitoka wakiwa wamembeba Rahab akionekana akiwa katika hali mbaya.
Priscar akataka kujitokeza ili  akasaidiane nao ila akaona itakuwa ni hatari kwake, akaendelea kujibanza kwenye mti huo hadi wakaondoka kwa kasi katika eneo hilo.
Kudhibitisha ni kitu gani kilicho weza kutokea ndani ya handaki hilo, kwa haraka akakimbia nje ya handaki hilo kutazama ni nini kilicho tokea.
 
Hakuamini macho yake baada ya kukuta damu nyingi zikiwa chini ya sakafu zikitokea katika chumba alipo ingia akazidikuta zikiwa nyingi jkuu ya kitanda. Jasho likaanza kumtirirka akifikiria ni kitu gani ambacho kimetokea bosi wake.
Kwa haraka akatoka ndani ya handaki na kurudi alipo liacha gari lake. Akaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea Dar es Salaam akiamini kwamba ni lazima Rahab atakuwa amepelekwa kwenye moja ya hospitali iliyopo jijini Dar es Salaam.
 
  Kwa bahati nzuri akabahatika kuweza kuuona msafara wa raisi kwa mbali, kwa tahadhari kubwa akaufwatilia hadi katika hospitali ya Muhimbili. Magari yalipo ingia katika geti kubwa la Muhimbili na yeye akalisimamisha gari nje na kushuka na kuanza kuelekea katika geti. Walinzi wa getini wakamzuia asiingie ndani ya geti hilo kutokana ni majira ya usiku.
Akatoa kitambulisho chake, baada ya askari mmoja kukisoma akamuamuru wezake wamruhusu Priscar kuingia ndani ya hospitali. 
 
“Samahani nesi kuna mgonjwa ameletwa hapa dakika mbili zilizo pita amepelekwa wapi?”
“Aliye letwa wakati huu ni mke wa raisi na amepelekwa chumba cha upasuji”
“Asante”
Shamsa akaondoka na kuanza kutembea kwa mwendo wa haraka kuelekea  kwenye chumba cha upasuaji, kabla hajafika akawaona baadhi ya makachero wezake wa ikulu wakiwa nje ya chumba hicho wakiwa wameimarisha ulinzi mkali nje ya chumba hicho kuku raisi akimwagikwa na machozi.
 
Katika hali ya kustaajabisha Priscar akashuhudia damu nyingi zikiruka kwenye kioo cha dirisha cha chumba hicho pasipo hata walinzi walio kipa mgongo  chumba hicho kushuhudia tukio hilo.
Kwa haraka akaanza kukimbia kuelekea kwenye chumba hicho, makachero wezake wanao mfahamu wakabaki wakimshangaa, mmoja wao akataka kumzuia ila akaambuliwa kusukumwa pembeni hadi raisi aliye kuwa emekaa akanyanyuka kumshnagaa binti huyo aliye mpa majukumu ya kumlinda mke wake na akashindwa.
 
Priscar bila hata kumjali mtu akaupika teke mlango huo ila haukufunguka, hapo ndipo watu wote wakatambua kwamba kuna tatizo limetokea ndani ya chumba hicho baada ya kuziona damu nyingi kwenye kioo cha mlangoni kikiwa kimetapakaa damu na mbaya zaidi hawasikii kitu chochote mutoka ndani ya chumba hicho kilicho tengenezwa kwa utaalamu mkubwa wa kuto kutoa sauti nje wala kuingiza sauti ndani pale mlango unapokuwa umefungwa vizuri.
                                                                                         
SORRY MADAM (46) (Destination of my enemies)

Makachero wote wakisaidiana na Priscar wakaendelea kuusukuma mlango kwa nguvu zao zote ila hawakupata mafanikio ya kuweza kuufungua mlango huo. Mwanga wa taa ambao ulikua unafifia ndani ya chumba hicho zikazima na giza likatawala.
Kila mtu hususani raisi Pryagod wakawa wamechanganyikiwa hapakuwa na mtu aliye weza kuelewa ni jambo gani ambalo linaendelea ndani ya chumba hicho.
“Pigeni risasi mlango hadi uvunjike”
Raisi Praygod alizungumza huku jasho likimwagika, macho yake yote mawili yalitwaliwa na rangi ya uwekundu ulio sababishwa na kulia kwa muda mrefu.
 
“Muheshimiwa hapa ni hospitali kuna….”
“Pumbavu nimesema vunjeni”
Raisi Praygod alimfokea mlinzi wake, huku akimpokonya bastola aliyo ishika. Raisi akaikoki bastola hiyo vizuri kisha akaanza kufyatua risasi kwenye mlango huo ulio tengenezwa kwa aluminium. Milio ya risasi ikawastua baadhi ya watu walio kuwa karibu na jengo la upasuaji. Baadhi ya madaktari na walinzi wa hospitali ikawabidi kukimbila katika jengo hilo kushuhudia ni jambo gani linalo toklea isitoshe wanafahamu uwepo wa raisi katika eneo la hospitali.
 
Wakawakuta makachero wa raisi wakiushambulia mlango wa chumba cha upasuaji hadi ukalegea, wakaanza kuupiga mateke ya nguvu hadi ukaanguka chini.
Kwa giza ambalo limetawala ndani ya chumba hicho hapakuwa na mtu aliye weza kuona kitu chochote ndani. Kachero mmoja akatoa simu yake mfukoni na kuwasha tochi, iliyo fanya kila mtu kushuhudia viongo vya binadamu vilivyo achanishwa na mwili vikiwa vimezagaa zagaa chini, huku damu nyingi zikiwa zimetapakaa kila kona ya chumba.
 
 ***
Askari akazidi kulisogelea gari ambalo Eddy yupo ndani yake. Katika kutazama vizuri akaona mtu akiwa ameinama ndani ya gari hilo. Ikamlazimu kuchomoa bastola yake kiunoni na kuishika vizuri na kuzidi kupiga hatua za umakini kuelekea kwenye mlango wa gari hilo.
  Sa Yoon a daktari wa Shamsa wakaruhusiwa kuingia katika chumba cha wagonjwa mahututi. Sa Yoo akamkuta bibi yake akiwa amejilaza kitandani huku manesi wawili wakiwa wamesimama karibu  na kitanda chake nyuso zao zikiwa hazina uchangamfu wowote.
 
“Bibi…..!!”
Sa Yoo aliita huku akikaa  kwenye kitanda hicho. Kilicho mshangaza katika siku ya leo ni mashine ya kupumulia iliyo kuwa puani mwa bibi yake leo haipo. Akaita kwamara ya pili hadi ya tatu machozi yakiendelea kumwagika. Bibi yake akafumbau macho yake kwa mbali, taratibu bibi huyo aliye zeeka kutokana na umri mkubwa akaunyanyua mkono wake wa kulia taratibu na kumshika mjuu kuu wake. Akaachia tabasamu dogo kiasi kisha akayafumba macho yake moja kwa moja na mauti yakamchukua.
 
Huzuni na majonzi ikazidi kutawala kwa kila mtu aliye kuwamo ndani ya chumba hicho. Sa Yoo, alijikuta akilia kama mtoto mdogo huku akigara gara chini, kwa msaada wa manesi walifanikiwa kumnyanyua na kumtoa ndani ya chumba hicho na kumpelekea katika chumba maalumu kwenye hospitali hiyo ambacho mara nyingi hutumiwa na watu walio fiwa wakiwa katika hospitali hiyo.
“Daktari vipi mbona umenyongea hivyo?”
“Bibi yake yule binti ameaga dunia”
“Masikini weeee”
Shamsa alizungumza kwa unyonge ikiashiria hata yeye kifo hicho kimemgusa kidogo japo hamfahamu marehemu ila kitendo cha kukutana na Sa Yoo muda mchache ulio pita, moyo wake ulitokea kumepnda binti huyo wa kijapan.
“Nenda kwenye gari yake kula kuna rafiki yake nenda kamuite. Samahani lakini kwa usumbufu”
 
“Hakuna tatizo daktari”
Shamsa kwa haraka akaanza kutembea kuelekea nje. Dakika mbili tayari akawa amefika kwenye gari ya Sa Yoo. Hali aliyo ikuta kwenye gari hiyo kidogo ikaanza kumpa mashaka kwani mtu aliye ambiwa akamuite hajamkuta. Na kioo cha pembeni cha gari hiyo kimepasuliwa kwa kupigwa na kitu kizito.
 Kila alipo angaza katika maeneo hayo ya maegesho ya magari hakuweza kuona dalili yoyote ya mtu aliye ambiwa aende kumuita. Ubaya mtu mwenyewe hamfahamu ni nani.
 
Ikamlazimu Shamsa kurudi ndani ya hospitali akamuelezea hali halisi daktari wake aliyo ikuta kwenye gari la Sa Yoo. Daktari hakuwa na lolote la kumueleza Shamsa zaidi ya kunyanyuka katika sehemu waliyo kuwa wamekaa na moja kwa wakaongozana na Shamsa hadi kwenye chumba alichopo Sa Yoo. Wakamkuta akiwa amesimama karibu na dirisha macho yake yote yakiwa yatazama nje.
“Sa Yoo”
Daktari alimuuita, Sa Yoo akageuka taratibu na kuwatazama. Shamsa akapiga hatua za haraka hadi alipo simama Sa Yoo na kumkumbatia kwa nguvu, jambo lililo mfanya Sa Yoo kuangua tena kilio kikubwa
                                                                                                   ***
   Manka akiongozana na Fetty, Jaquline, Halima na Anna, wakatua ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA) majira ya saa tano usiku, wakitumia shirika la ndege la QATAR. Wakapokelewa na mshauri wa raisi bwana Mgwira aliye wapeleka moja kwa moja kwenye hoteli ya kitalii ya  iitwayo Bilila Louge.
“Hapa mutakuwa salama zaidi kuliko kwenye mahoteli mengine”
 
Bwana Mgira alizungumza huku akitabasamu kwani anatambu ni kazi gani ambayo masichana hao imewaleta ndani ya Tanzania japo ni wazawa wa Tanzania na kukulia Tanzania ila matatizo ya hapa na pale yamewafanya kuonekana kama wageni ndani ya Tanzania.
 “Sawa muheshimiwa”
“Hakikiheni hakuna mtu anaye weza kuwatila mashaka, ili kazi iliyo walete isije ikaingia dosari”
“Kwa hilo usijali”
Manka ndio alikuwa kiongozi wa kumjibu bwana Mgwira. Simu ya bwana Mgwira ikaita na kuwafanya wote wakae kimya kusikilizia anacho kwenda kuzungumza.
“Kuna matatizo?”
“Mke wa raisi amefanyeje tena?”
“Mungu wangu!!  Ngoja nakuja nachukua ndege ya kukodi”
“Sawa sawa”
 
Bwana Mgwira akakata simu na kuirudisha kwenye koti la suti.
“Jamani kuna matatizo ya kiofisi yametokea inanilazimu kurudi Dar es Salaam usiku huu huhu”
“Ngoja kwanza mke wa raisi anaitwa nani?”
Fetty alimuuliza bwana Mgwira huku akiwa amemkazia macho.
“Anaitwa Rahab Praygod Makuya”
Fetty na wezake wakatazamana kila mmoja akawa na shahuku ya kutaka kujua ni jambo gani limepata rafiki yao waliye potezana naye kwa miaka mingi ya nyuma.
 
“Amepatwa na nini?”
Halima aliuliza
“Hata mimi sijaelezwa kwa kina ila nimeambiwa kwamba ana matatizo makubwa sana, hapa raisi nasikia amechanganyikiwa ndio maana  ninahitajika. Cha kufanya nitawapa ripoti ya kila jambo ambalo litakuwa linaendelea. Hii ndio nafasi yetu ya nzuri ya kusimamisha Godwin kama raisi wa hii nchi”
“Sawa”
Bwana Mgrira akatoka na kuwaachia maswali mengiu Fetty na wezake kila mmoja akiwa anahitaji kufahamu kilicho mpata Rahab
                                                                                                 ***
“Nikiendelea kukaa hapa itakuwa ni matatizo”
Eddy alijisemea kimya kimya huku akiendelea kuchungulia kwa kuibia katika kioo cha pembeni cha gari akimtazama askari anaye kuja katika eneo la mlango wa gari, kwa haraka akaufungua na kumbamiza nao askari huyo, aliye yumba kidogo. Bila kupoteza muda akatoka ndani ya gari, askari huyo akarusha teke zitro lililo mpiga Eddy kifuani na kumyumbisha  kidogo, kutokana na mazoezi aliyo nayo, alijizuia kwa asilimia kubwa asianguke chini kwani hiyo itawapa nafasi askari wengine wanao kuja kwa kasi katika eneo hilo, kumkamata.
 
Eddy akamtazama askari huyo aliye amua kuupanga mkono kupigana na Eddy, askari akarusha ngumi nzito ambayo Eddy akaikwepa na kwenda kutua kwenye kioo cha gari, hapo ikawa nafasi kwa Eddy kuanza kurusha makombora ya ngumi mfululizo, zilizo mpata askari huyo maeneo ya kicchwani.
 
“POLISIIIIII”
Askari mmoja alizungumza huku akiwa amemnyooshea bastola Edddy, wakaongezeka askari wengine ambao walifika kwa pamoja kuifatilia gari ambayo ilimbeba Eddy. Yote yakiwa yanaendelea Sa Yoo aliweza kuyaona kupitia juu dirishani, kutokana akili yake kwa wakati huo haikuwa na jambo jengine la kuwaza zaidi ya bibi yake. Hakulichukulia uzito tukio hilo la Eddy na maaskari.
‘Siwezi kukamatwa kizembe hivi’
Eddy akamvuta askari aliye mpiga ngumi kadhaa, zilizo mfanya aonekane kama mlevi kwa kuyumba yumba kwake. Akampiga kabari na kuwaonya askari wengine kwamba wakifanya jambo lolote baya mwenzao ataiaga dunia.
 
Kutokana aliye kabwa ni kiongozi wao hawakuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kuendelea kumnyooshea Eddy bastola zao.
Ukaribu wa futi chache kutoka sehemu walipo simama askari na Eddy, ukampa umakini wa kufikiria jambo jengine kwa haraka kujiokoa mikononi mwa askari hao.
Akamsukumia askari aliye mkamata kwa wezake, jambo lililo wafanya askari wawili kumdaka mkuu wao asianguke chini. 
 
Wakiwa kwenye kurupushani ya kumdaka kiongozi wao, kipondo kikali kutoka kwa Eddy kikaanza kutembea kwenye miili yao. Baadhi ya wananchi walio karibu na eneo la maegesho ya magari hawakusita kuchukua video na simu zao za mikononi kwani wengi wao walihisi ni kama mkanda wa sinema, kwa maana mapigo ambayo askari hao wanayapokea ni kama anayopiga msanii maarufu katika bara lao la Asia Jat Lee. Hapakuwa na mtu aliye weza kuamini kwamba Eddy ni mwalifu, kila mmoja alisha sahau ni wapi alimuona ila walijikuta wakifurahia tukio hilo.
 
Ndani ya dakika mbili askari wote kila mmoja akawa anaugulia kivyake vyake, Eddy akaingia kwenye moja ya gari ambalo alibahatika kukuta mlango wake ukiwa wazi, kwa bahati nzuri zaidi akakuta funguo ya gari hilo, kwa haraka akaliwasha na kuondoka. 
 
Askari hao nao wakajizoa zoa na kuingia kwenye magari yao na kuanza kumfukuzia Eddy. Kutokana na kuto ifahamu Japan vizuri, ikamlazimu kulitekeza gari hilo kwenye moja ya kichochoro na kuanza kukimbia kwa miguu kuelekea asipo pafahamu.
 
Kutokana na mitaa mingi na idawi ya watu, askari wakajikuta wakimpoteza Eddy wasifahamu ni wapi alipo elekea.
Eddy akafika kwenye moja ya kichochoro chenye viajana wengi wengi wanao onekana ni wala unga na vibaka.  Kutokana anajiamini sana akazidi kukatiza katika kichochoro hicho, kila alivyo zidi kwenda ndivyo vijana hao walivyo zidi kuongezeka nyuma yake huku wengine wakitokea kwa mbele wakiziba njia ya yeye kupita. Huku kila mmoja akitoa kisu kwa ajili ya kumshambulia Eddy.
 
 ***
Kila mmoja akajikuta akiwa amemkodolea macho Rahab aliye kaa chini, kwenye kona huku akiwa amejikunyata. Mwili mzima wa Rahab umejaa damu kuanzia kichwani hadi miguuni. Japo na ujasiri wote wa mafunzo ya ukachero, ila kila mmoja alijikuta akimuogopa mke wa rasisi isipo kuwa Priscar na raisi Praygod.
“Madama”
Priscar aliita kwa sauti ya unyonge huku akichuchumaa, akajaribu kumshika ila Rahab akazidi kujikunja kama aneye uogopa mkono wa Priscar.
 
“Madam ni mimi Priscar”
Raisi Praygod na makachero wengine wote wakawa kimya wakimsikiliza Priscar, swali ambali lilianza kuwaumiza makachero walio mpiga risasi Rahab, imekuwaje kuwaje hadi Rahab kuwa hai na kujikunyata katika kona hiyo, ikiwa risasi walizo mpiga ni nyingi za kumuhatarishia maisha yake.
Kitu kingine kilicho zidi kuwaogopesha ni viungo vya binadamu, vikiashiria kwamba madaktari wote walio kuwa wakimfanyia oparesheni wameiaga dunia.
 
Rahab akainyanyua sura yake iliyo kuwa imefunikwa na nywele zake ndefu zilizo kuwa zimelowana damu. Akamtazama Priscar usoni, gafla machozi yakaanza kumwagika. Taratibu rasisi Praygod akapiga magoti chini huku akiwa hamuamini amini mke wake. 
 
“Mke wangu”
Rahab akamtazama raisi Praygod na kumkumbatia, wote wakajikuta wakimwagikwa na machozi, jambo lililo wafanya makachero wengine kuwa katika hali ya simanzi iliyo changanyikana na furaha. 
Gafla Rahab akaanza kuisikia milio ya risasi masikioni mwake, alipo nyanyua kichwa chake akawaoa makachero walio mpiga risasi kwenye handaki. Macho yake gafla yakabadilika na kuzidi kuwa mekundu,  akamsukuma raisi Praygod pembeni na kumrukia kachero mmoja aliye mpiga risasi, akambwaga chini na kuanza kuliminya koo la kachero aliyeanza kutapatapa akijitahidi kuutoa mkono mmoja wa Rahab ulio mkaba shingoni.
ITAENDELEA...

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx