![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4RkpZKlq2ggrQFhSEWiM6ofoy1uq5E5azC7SN9ysl3Pz6A-y3dqaa_XAvwpy69KugubtoQF1WB7UBK9vMk5ltMU8OwmbwGvdwchbSydqNMuzKPnNCYvLAsRrwChsMKD9m5DgKel1-2IZo/s640/%25255BUNSET%25255D.jpg)
Wanasayansi wafahamisha kuwa bara la 8 lawezekana kuwa lipo chini ya bahari ya Pasifiki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika jarida la Marekani la 'Geological Society of America' ni kwamba bara hilo limepewa jina la Zealandia .
Bara hilo lililokubalika na wanasayansi linasemekana kupatikana katika upande wa Kusini Magharibi mwa bahari ya Pasifiki.
Liko na ukubwa wa kilomita milioni 5 za mraba sawa na thuluthi ya ardhi ya bara la Australia .
Wanasayansi wamesema kuwa bara hilo limefinikwa na maji ya bahari .