Simba ilikuwa na nafasi ya kusawazisha katika mechi hiyo lakini beki, Janvier Bokungu akakosa penalti. Kipigo cha Simba, kinapunguza makali ya watani wake Yanga ambao walichapwa kwa mabao 2-0 na JKU ya Zanzibar wikiendi iliyopita.
Kipigo cha Yanga kiliwaamsha Simba ambao walitumia muda mwingi kuwananga watani wao, lakini leo mambo yamegeuka. Unaweza kusema hakuna kuchekana kwa kuwa Yanga ndiyo wanaotamba sasa.