test

Jumanne, 6 Desemba 2016

HIZI NDIZO ZILIZOMFANYA HUSSEIN PAMBA KALI KUPANDISHWA KIZIMBANI



MFANYABIASHARA na mmiliki wa maduka ya nguo jijini Dar es Salaam, Hussein Mkangala (38), maarufu ‘Hussein Pamba Kali’ amepandishwa kizimbani wiki hii funguliwa kesi ya madai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni
 
Upende wa mashtaka umedai  Mkangala anadaiwa Sh milioni 75 na   Anna Kiabi.
Shauri namba 146/2016 kwa mara ya kwanza lilitajwa jana katika mahakama hiyo ambapo upande wa mdai ulikuwa unasimamiwa na Wakili Jonas Nkya, wakati ule wa utetezi (mdaiwa) ukiongozwa na wakili wa kujitegemea  Ernest Swai.
Mbele ya Hakimu Is -Haq Kuppa, Wakili Nkya alidai mahakamani hapo kwamba tukio hilo lilitokea Novemba 20 mwaka jana ambapo mfanyabiashara huyo alikopeshwa Sh milioni 80 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zake za kibiashara, lakini hakuweza kurejesha.
Wakili huyo aliongeza kwamba ilipofika Mei 22 mwaka huu mdaiwa ambaye ni Husseni alimtuma mdogo wake aitwaye Hassan Mkangala, apeleke Sh milioni 5 kwa Anna na kiasi kilichobakia hajalipa tena hadi sasa.
Upande wa utetezi uliiomba mahakama hiyo iwape muda wa siku 6 ili waweze kujibu madai ya walalamikaji.
Hakimu Kuppa aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 15 mwaka huu.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx