MFANYABIASHARA na
mmiliki wa maduka ya nguo jijini Dar es Salaam, Hussein Mkangala (38),
maarufu ‘Hussein Pamba Kali’ amepandishwa kizimbani wiki hii funguliwa
kesi ya madai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni
Upende wa mashtaka umedai Mkangala anadaiwa Sh milioni 75 na Anna Kiabi.
Shauri namba 146/2016
kwa mara ya kwanza lilitajwa jana katika mahakama hiyo ambapo upande wa
mdai ulikuwa unasimamiwa na Wakili Jonas Nkya, wakati ule wa utetezi
(mdaiwa) ukiongozwa na wakili wa kujitegemea Ernest Swai.
Mbele ya Hakimu Is -Haq
Kuppa, Wakili Nkya alidai mahakamani hapo kwamba tukio hilo lilitokea
Novemba 20 mwaka jana ambapo mfanyabiashara huyo alikopeshwa Sh milioni
80 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zake za kibiashara, lakini hakuweza
kurejesha.
Wakili huyo aliongeza
kwamba ilipofika Mei 22 mwaka huu mdaiwa ambaye ni Husseni alimtuma
mdogo wake aitwaye Hassan Mkangala, apeleke Sh milioni 5 kwa Anna na
kiasi kilichobakia hajalipa tena hadi sasa.
Upande wa utetezi uliiomba mahakama hiyo iwape muda wa siku 6 ili waweze kujibu madai ya walalamikaji.
Hakimu Kuppa aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 15 mwaka huu.