test

Alhamisi, 3 Novemba 2016

VIDEO: Mabishano ya Mbowe na Naibu Spika Kuhusu Tuhuma za Wabunge wa CCM Kuhongwa Milioni 10 Kila Mmoja ili Wapitishe Muswada wa Habari


Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu leo asubuhi  alidai kuwa, mnamo siku ya Jumanne tarehe 25/10/2016 saa mbili usiku kiliitishwa kikao cha wabunge wa CCM ambacho Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikuwa Mwenyekiti, na kilihudhuriwa na Katibu MKuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kwa ajili ya kujadili Muswada wa Habari.

Mbowe alisema kuwa Wabunge wakiwemo Mawaziri walihongwa shilingi milioni 10 kila mmoja ili waweze kusaidia kupitisha Muswada wa Habari unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni kesho.

Lakini Naibu spika alikataa  Waziri mkuu kujibu swali la Mbowe kwa  madai kuwa swali hilo halihusu sera, huku Mbowe akidai linahusu sera kwa kuwa ni rushwa kwa wabunge 
                     ==> Wasikilize Hapo chini

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx