test

Jumamosi, 12 Novemba 2016

‘TULIPATA Wakati Mgumu Kumtambua Mzee Sitta Kama Bado ni Kada wa CCM’ – Mbowe



Freeman Mbowe ni mbunge wa jimbo la Hai na mwenyekiti wa CHADEMA taifa ambaye leo November 11 2016 alipata nafasi ya kuongea wakati wa kuuaga mwili wa Spika mstaafu Samuel Sitta ndani ya bunge Dodoma.

‘Mzee Sitta tulimuona kama kiongozi asiekua mbaguzi wa kiitikadi, aliamini katika kubadilisha kwenda kwenye ubora katika nafasi yote ya utumishi wa UMMA aliyoihudumia, alikua mtu aliejaza matumaini watu wote aliowaongoza wakati wote, alikua mtu wa kuunganisha makundi yote‘ – Mbowe

‘Mara nyingine sisi wapinzani tulipata wakati mgumu sana wa kumtambua Mheshimiwa Sitta bado ni kada wa CCM sababu alikua na uwezo wa kutujaza matumaini, kutupa fursa ya kutusikiliza lakini mwishoni tunakuja kugundua bado ni wa CCM‘ – Freeman Mbowe

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx