test

Jumatatu, 28 Novemba 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 95 & 96 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )



MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
"Ndio hivyo, dokta wake amesema tunaweza kumpoteza mama muda wowote kuanzia leo. Hapa nilipo nimechanganyikiwa"
Nikakata simu, mwili mzima nikawa kama umezizima, picha ya Jonh na Sheila zikanijia kichwani jinsi walivyo kua na furaha, nilipo waona kwenye mgahawa.
"John nilazima ulipe kwa hili. Nikatuua kwa mkono wangu mwenyewe, ole mama yangu afe, nitakufanya kama Derick"
 
ENDELEA
Kila nilicho kifikiria juu ya adhabu nitakayo mpa John, sikupata jibu la uhakika. Nikazima kila kitu na kurudi chumbani kwetu. Nikajilaza kitandani taratibu huku mawazo yakiendelea kuniandama. Kikubwa nikawa ninamfikiria sana mama yangu. Sikulala hadi kunapambazuka.
"Umeamkaje baby?"
Phidaya alinisalimia mara baada ya yeye kuamka.
"Safi vipi?"
"Ahaaa poa, alafu nimeota ndoto mbaya kama nini?"
"Ndoto gani?"
"Nimeota John amekuja hapa tulipo, akiwa na wale watu wake, akatufunga kamba, sote wanne, kisha wakatuweka hapo sebleni. Wakamwaga mafuta ya petroli kila sehemu, na kuwasha moto wao wakaondoka. Ndio nikastuka"
 
"Mmmm hakuna kitu kama hicho"
Niliamua kumfariji Phidaya, kwani sikupenda apoteze amani asubuhi hii, ambayo tunaendelea kujiandaa na maandalizi ya sherehe ya kuzaliwa kwa Junio wetu.
"Hapa nilipo mapigo ya moyo yananienda mbio."
  Nikamvuta karibu yangu na kumlaza kifuani mwangu, taratibu nikaanza kuzichezea nywele zake ndefu na laini.
"Tulia mke wangu"
"Eddy naogopa"
"Umaogopa nini mke wangu"
"Nahisi familia yangu, itapata shida tena. Tena hii itakua kubwa kuliko ya kwanza"
"No baby usiyape nguvu, mawazo hayo mimi nipo. Nitahakikisha hakuna kitakacho haribika wala mtu kunyanyua mkono wake juu ya familia yangu nipo tayari kwa lolote hata kufa ili mradi familia yangu iishi kwa amani"
"Kweli baby?"
 
"Ndio kama aliweza ile mara ya kwanza basi hii ya pili, hato weza kamwe"
Nilizungumza huku nikiwa na jazba ya hasira, kwani hadi hapa ninavyo zidi kumfariji mke wangu, tayari John amesha yaweka maisha ya mama yangu mashakani. Taratibu Phidaya akaanza uchokozi wa kitandani, sikuwa na hiyana zaidi ya kumpa haki yake anayo stahili kama mke wangu. Hadi tunamaliza kila mmoja akawa kwenye furaha isiyo simulika, kwani wote tulifika kwa wakati mmoja mwisho wa mechi yetu.

"Ngoja nikaandae kifungua kinywa"
"Sawa"
Phidaya akanyanyuka na kuingia bafuni, akaoga na kutoka. Akavaa nguo alizo amua kuvaa kwa siku hii yaleo na kwenda nje. Nikachukua simu ya mezani, nikaziingiza namba za Blanka na kumpigia. Simu ikaita baada ya muda ikapokelewa.
"Vipi hali ya mama?"
"Kuna mabadiliko kidogo?"
"Mazuri au mabaya?"
"Mazuri, nilimuonyesha mama picha yako ukiwa na mkeo na mwanao. Kidogo mama alianza kufungua kinywa huku akitabasamu"
 
"Hakusema chochote?"
"Hapana, alitabasamu tu na kutingisha kichwa kama mtu aliye furahi kwa kuiona hiyo picha"
"Poa nitakuja"
"Kwani upo wapi?"
"Nitakuambia siku nyingine. Kwaheri"
Nikakata simu, baada ya kumuona Junio akiingia chumbani huku akilia jambo lililo nistua sana.
"Mona unalia?"
"Mamy kanipiga"
Kidogo mapigo ya moyo yakanitulia.
"Kisa nini?"
"Eti hataki nimsaidie kupika chai"
"Ni hilo au kuna jengine"
"Nihilo dady"
"Mwanao ni muongo"
Phidaya aliingia huku akionekanana kukasirika.
"Amefanyaje?"
"Nimemuambia asicheze mpira ndani, likawa halinielewi. Mpaka akaipiha Tv ya ukutani ikaanguka"
 
"Imevunjika?"
"Hapana, haijavunjika. Tena huku nje usitoke ubaki humu humu na huyo baba yako. Sitaki kukuona huku nje sawa?"
Phidaya alizunguilmza na kutoka nje, nikamnyanyua Junio na kumtupia kitandani nilipo na kumfanya aanze kucheka na kufurahi.
"Huo uronaldo wako, uwe unaufanyia nje sawa mwangu?"
"Sawa dady, twende tukacheze nje"
Junio alizungumza huku akinivuta mkono, nikatizama saa ya ukutani inaonyesha ni saa tatu asubuhi.
"Nenda ukaningoje sebleni nioge mara moja"
"Ok dady"
Junio akatoka nikaingia bafuni na kuoga, kisha, nikavaa nguo za mazoezi na kutoka nje.
"Munaenda wapi?"
Phidaya alutuuliza baada ya kutuona tukitoka mlangoni bila ya kuaga.
"Ufukweni"
"Kifungua kinywa tayari"
"Anzeni tu sisi tunakuja"
"Eddy mbona unapenda kumuendekeza huyo mwanao, kila anacho taka unamfanyia"
Nikamfwata Phidaya na kumbusu mdomoni.
"Tunakuja baby, Shamsa yupo wapi?"
"Yupo jikoni anamalizia kupika"
"Ok tunakuja"
 
Tukatoka na Junio, tukaingia kwenye lifti na kushuka hadi chini, tukitokea gorofa ya saba, yalipo makazi yetu. Tukaelekea kwenye fukwe zilizopo pembezoni mwa hotel hii. Kitu kilicho nishangaza ni jinsi Junio alivyo maarufu kwa watoto wezake ambao tuliwakuta hapa ufweki. Wakaunda timu mbili huku nami nikiwa timu pinzani na Junio. Wakanichagua kua goli kipa na sikuwa na jinsi. Magoli ya viayu tuliyo yaweka hayakuzuia mechi kuanza, huku golikipa wa timu ya Junio, akiwa mzee mwenye mjukuu wake kwenye timu yangu.

Hapa ndipo nilipo pata fursa ya kumtazama Junio vizuri, nakugundua anakipaji kikubwa cha kucheza mpira. Mara kadhaa akawa anapiga mashuti mazito golini mwangu, ambayo niliweza kuyanyaka vizuri. Huku wachezaji wa timu yangu wakinisifia kwamba ninaweza kazi ya kulinda goli. Kitendo cha kuinyaka mipira, ndivyo jinsi Junio alivyo ongeza juhudi ya kucheza na kupiga mashuti mazito golini.
"Kumbe na wewe ni kipa mzuri?"
Mzee wa timu ya Junio ambayo hadi sasa hivi hakuna goli alilo fungwa, aliniuliza tulipokua tukibadilishana magoli, baada ya dakika kumi na tano alizo tuwekea refa wetu kuisha.
 
"Najaribu tuu"
"Hapana, kuna kitu nimekiona ndani yako na huyo mwanao"
"Kitu gani?"
"Muna vipaji vikubwa sana, hakikisha unamuendeleza mwanao katika fani hii, atafanikiwa sana na atakuwa mchezaji mkubwa sana duniani"
Sauti ya filimbi ikatustua mimi na huyu mzee, huki refa akituomba kila mmoja akakae kwenye goli lake, tukafanya kama alivyo tuelekeza.
Mpira ukaanza, japo kuna tifutifu jingi kwenye hii fukwe, ila Junio, anakimbia kuliko watoto wezake ambao mara kadhaa, walikua wakianguka anguka.
Shuti kali alilo lipiga Junio, akiwa karibu yangu, likanipita katikati ya miguu yangu na kwenda mbali kidogo na sehemu tunayo chezea mpira. Nakuwafanya Junio na timu yake kushangilia ushindi wa goli hilo walilo kua wakilitafuta kwa juhudi mara baada ya kipindi cha pili kuanza.
"Hahaaaa haaaaaa"
Nilimuona Phidaya akicheka, huku akiwa na kamera yetu. Nikatambua moja kwa moja anacheka goli, nililo fungwa na Junio. 
 
"Junio kachukue mpira sijui umeenda wapi"
Nilimuambia Junio aufwate mpira wake ambao yeye ndio aliuona sehemu ulipo elekea. Junio akaongozana na wezake wawili kwenda kuutafuta.
"Unacheka nini?"
"Nakucheka wewe, ulivyo fungwa na huyo mwanao, njoo uone hili goli lilivyo ingia"
Nikamfwata Phidaya alipo, akanionyesha video aliyo rekodi, goli lililo pita katikati ya miguu yangu
"Mwanao amekupiga tobo"
"Huyu mtoto, ananguvu za miguu kama hadi ananiogopesha, skija golini"
"Ndio hivyo tumepata mchezaji, mzuri tusubirie atakaye kuja sijui atakuwaje"
"Huyo naomba awe wa kike"
"Kweli ehee"
"Au wewe unataka aweje?"
"Vyovyote Mungu atakavyo tubariki, nenda uwanjani wamesha rudi na mpira"

Mechi ikaendelea huku mipira mingi ikielekezewa golini kwetu, baada ya wachezaji wangu kuchoka sana. Ikanikazimu mara kadhaa nikaiokote mipira inayotoka nje ya goli letu. Mpira mmoja ukapigwa na mchezaji wa timu ya Junio, ukaenda mbali kidogo. Nikaanza kuukimbiza kwa bahati mbaya ukagonga glasi mbili za juisi zilizo wekwa kwenye kijimkeja, huku pembeni yake akiwa amelala, kifudifudi msichana mmoja, aliye valia chupi na sidiri, akiota jua na juisi zikamwagikia ubavunini.
 
"Ahaaaaa jamani"
Akanyanyuka, kitendo cha kunitazama usoni akastuka, kwani ni Sheila. Macho yake akabaki akiwa amenitumbulia. Sikuonyesha dalili yoyote ya kustuka kwani tayari ninatambua kitu kinacho endelea na anatambua kwamba mimi ni marehemu niliye zikwa wiki kadhaa za nyuma.
"Am sorry Madam"(Samahani bibie)
 
Nilibadilisha sauti yangu na kuifanya ya besi. Nikauokota mpira na kuondoka pasipo kutazama nyuma. Nikafika uwanjani, muda wa kucheza ukawa umeisha. Nikamuona Sheila, kwa mbali akiondoka akielekea kwenye hoteli ya pembeni yetu, huku akiwa amejifunga kipande cha mtandio kiunoni mwake. Akaingia kwenye hoteli hiyo yakifahari kama ya yakwetu.
'Sipo nao mbali'
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiondoka na familia yangu. Tukafika ndani na kumkuta Shamsa akiwa anatusubiria sisi, ili tupate kifungua kinywa.
"Jamani mbona mumejaa michanga hivyo?"
Shamsa alituuliza baada ya kutuona mimi na Junio tukiwa tumechafuka sana.
"Si hiyo mijimipira yao. Nendeni mukaoge la sivyo hamuli leo"
"Jamani ndio munatutelekeza na mwanangu"
"Ndio nendeni mukaoge"
Nikataka kuokota soseji moja ila Phidaya akaniwahi kunidaka mkono
 
"Hembu tuachie uchafu wako, nenda ukaoge tunasikia njaa wezenu"
"Tangu lini njaa ikasikika"
"Banaa ehee hivyo hivyo"
"Sema nahisi njaa, sio nasikia njaa"
"Eddy mbona mchokozi lakini, unakuka kuniudhi mapema yote hii"
"Naombaaaa"
"Nini?"
"Kasoseji kiduchuuuuuu"
"Jamani huyu mwanaume mmero ahaaaa"
Phidaya akanikatia kipande kidogo cha soseji na kunilisha.
"Mambo si ndio hayo, kamuogesheni Junio nasikia maji yanamwagika tu huko bafuni kwake."
Nikaingia bafuni kwetu na kuanza kuoga, huku nikiwa na furaha ya mpango wanguy wa kumteketeza John, unaanza kukamilika, kutokana Sheila hajanistukia kwamba ni Eddy mimi na sio Fredy waliye muua. 
 
Nikarudi sebleni nikiwa nimevalia nguo nyengine. Tukapata kifungua kinywa. Tukapamba eneo zima la sebleni kwa ajili ya kesho, siku ya kuzaliwa kwa Junio. Phidaya na Shamsa wakasaidiana kutengeneza keki kubwa. Nikavaa sweta lenye kofia pamoja na miwani nyeusi. 
Nikawaaga kwamba nakwenda kununua vitu baadhi kwa ajili ya kesho. Nikafika kwenye hoteli ya jirani yetu, inayo onekana mmiliki akiwa ni mmoja kutokanana kufanana majengo yake kufanana sana.
Nikaikuta gari ya John kwenye maegesho ya hoteli hii, nikatafuta sehemu ya watu kukaa, nikajipatia kinywaji taratibu nikaanza kushusha tumboni mwangu, huku nikitazama anayetoka na kuingia kwenye hoteli hii yenye watu wengi tofauti na yakwetu, iliyo tulia sana.
 
Hadi kagiza kanaingia sikumuona John wala Sheila wakiwa kwenye eneo hili, nikahisi kukata tamaa ya kuwaona. Nikapiga fumba la mwisho la juisi yangu ninayo kunywa. Nikasimama na kujiweka sawa, kabla sijatoka nikawaona John na Sheila wakiitoka ndani ya lifti, iliyo toka gorofa za juu, wakielekea hadi sehemu ilipo kaunta ya vinywaji. Wakaagizia vinywaji, baada ya muda kidogo John akambusu Sheila na kwenda maeneo ya vyooni.
Nikaelekea sehemu alipo Sheila, nikasimana upande wake wa kushoto. Taratibu nikavua miwani na kuiweka juu ya meza kubwa iliyopo hapa kaunta.
 
Nikamuonyesha muhudumu mzinga wa whayne ninao uhitaji, jambo lililo mfanya Sheila kunitazama huku akiwa amenitumbulia mimacho. Mwili mzima ukaanza kumtetemeka kwa woga, hata simu yake kubwa aliyo ishika ikaanguka chini.
Nikalipa pesa ya mzinga huo, nikamuona John, akiwa anatoka kwenye mlango wa chooni. Nikavaa miwani yangu, taratibu na kuanza kuelekea mlango wa kutokea nje. Huku John akipita nyuma yangu bila ya kunijua. Kwakupitia kioo cha mbele yangu, nikamuona Sheila akininyooshea kidole, mimi huku, akizungumza na John, aliyekua akimbembeleza kutokana, analia kwa woga. Nikatoka nje ya mlango wa hotel. hii.
"Am sorry brother, please wait for me"(Kaka samahani naomba unisubirie tafafadhali)
Niliisikia sauti ya John, ikiniita kwa nyuma na kunifanya nisimame huku chupa yenye whyne, nikiishika vizuri, kwa lolote litakalo tokea kati yetu, huku nikimsubiria kwa hamu anifikie nilipo.

                                                                                                    ****SORRY MADAM****(96)

Nikawaona polisi wawili wakija mbele yangu, jambo lililo nifanya nishindwe kufanya kile nilicho hitaji kukifanya mbele ya John. Nikapiga hatua kwenda mbele, huku nikiipuuzia sauti ya John inayo niomba nisimame. Sikuelekea kwenye hoteli yetu kuepukana na kugundulika sehemu ninayo ishi. Nikafika kwenye kundi la watu wanao elekea barabarani, nikajichanganya nao. Nikageuka nyuma na kumuona John akiendelea kunifwata kwa nyuma
 
'Ngoja nimpeleke peleke huyu mwehu'
Nikazidi kutembea kwa mwendo wa kawaida, hadi nilipo fika kwenye moja ya eneo lililo tulia. Nikasimana na kugeuka nyuma na kumkuta John akiwa ananikaribia kunifwata.
"Brother....."(Kaka.....)
John hakumalizia sentensi yake na kubaki akinitumbulia mimacho.
"Can i help you?"(Ninaweza kukusaidia?)
Nilimuuliza John anaye nishangaa, huku sauti yangu nikiifanya nzito, tofauti na sauti ninayo itumia siku zote na iliyo zoeleka na watu wengi.
"You... you kno......"(Una.....una jua)
John alibabaika kiasi kwamva hata hata alicho kipanga kuzungumza kilimtoka kichwani.
 
”Samahani nilikufananisha"
John alizungumza huku akiondoka kwa aibu, na kutazama tazama chini. Kitu kilicho nifanya nishindwe kumdhuru John ni kamera za ulinzi zilizo fungwa barabarani. Ambazo zipo kwa ajili yàkuchukua matukio yote yatakayo tendeka barabarani hususani ya madereva wanao kwenda kwa kasi. Na endapo ningefanya lolote baya ingekuwa ni viguu kwangu kutoka nje ya nchi hii ya Brazili.
 
Nikamuona John, akirudi Hotelini, ambapo si mbali sana na sehemu tulipo. Ikapita taksi, nikaisimamisha na kuingia ndani, mikamuomba dereva anifikishe kwenye hoteli niliyo fikia jambo lililo mshangaza dereva taksi kwani umbali huo, mtu anaweza kutembea kwa miguu.
"I will pay you"(Nitakulipa)
Dereva taksi akafanya kama nilivyo muagiza. Njiani tukampita John, akirudi hotelini, wala hakuweza kuniona mimi ndani ya gari. Nikafika hotelini. Nikampa dereva kiasi anacho kihitaji. Kabla sijashuka nikamuona John akiingia kwenye hoteli waliyo fikia huku, akitembea kwa mwendo wa haraka akionekana kumuwahi mpeñzi wake Sheila.
             ***
   Nikaingia ndani na kuwakuta Phiday na wanae wakitazama movie kwenye tv, kubwa iliyopo sebleni.
"Mbona umechelewa kurudi?"
Phidaya aliniuliza huku akinyanyuka kwenye sofa, akanipokea chupa ya whyne niliyo ibeba. Akanibusu mdomoni.
 
"Nilikya nashangaa shangaa mji tu"
"Mmmm masaa yote hayo?"
"Ndio, pia kuna kazi nilikua nikiifanya, nitakuambia nikiwa nimetulia"
"Sawa, muda wa chakula, tulikua tunakungoja wewe"
"Dady umesha wahi kuiona movie ya Death Race?"
"Hapana"
"Njoo uicheki"
Nikakaa sehemu alipokua amekaa Phidaya, katikati ya Shamsa na Junio
"Jimovie lenyewe ndio wanauana hivyo?"
Nilimuuliza Junio baada ya kushuhudia tukio la filamu hiyo, ikionyesha mtu akiuliwa vibaya na gari moja kubwa, lenye watu wanao piga risasi.
"Yeaaah wamelipuka, dady cheki kule cheki"
Junio alizidi kupendezewa kwa tukio la gari hilo kubwa kugonga kwenye vyuma vyenye ncha kali na kulipuka vibaya.
"Sasa Junio mwanangu, hapo ni kipi kinacho kufurahisha?"
"Dady lile jigari likubwa lilikua likiwashambalia Frank Sting na Joe"
 
"Eddy narudia tena kukuambia, kwamba umeniharibia mtoto. Hapo hajaanza shule, anawajua masteringi wa movie hizo kama ndio wazazi wake"
"Usimlaumu hata mimi nilivyo kua mtoto nilipenda kutazama sana movie. Junio stering anaitwa nani?"
"Jansan Stathan au Frank Sting"
"Mmmm haya baba, nyanyuka ukale movie yako naiwekaa pause, ukimaliza utaendelea"
Tukanyanyuka sote, na kukaa meza yachakula.
"Shamsa mbona kama haupo sawa?"
"Najisikia sikia kichwa kinauma"
"Umekunywa dawa?"
"Hapana, ila kitapona. Nahisi ni jinsi tulivyo tazama tv muda mrefu, imechangia kichwa kuuma"
"Mmmm pole fanya ule, kisha ukameze dawa. Sawa mwanangu?"
"Sawa baba"
Kwa mara ya kwanza Shamsa kuniita baba, jambo lililo nishanga
za sana kwani siku zote alizoea kuniita Eddy. Furaha ikazidi kuongezeka moyoni mwangu. Kwa kuona Shamsa akiniheshimu kama baba yake mzazi.
 
"Shamsa utaniambia nikupe dawa gani, kwa maana mimi ni dokta"
"Kweli mama?"
"Ndio nilikua dokta, muulizeni huyo baba yanu, tumetokea wapi?"
"Natamani nisome kwa juhudi, ili niwe dokta kama baba na mama yangu"
Shamsa alizingumza kwa sauti yaunyonge iliyo jaa huzuni.
"Usijali utakuwa, tutahakikisha tunakupa chochote utakacho kutoka kwetu"
Phidaya alizungumza huku akimshika shingo Shamsa kumfariji, kutokana Phidaya anatambua historia nzima ya Shamsa baada ya mimi kumuadisia, tukiwa ndani ya ndege tukija Brazili.
 Tukamaliza kula, kabla kila mtu hajaendelea na shughuli yake nikawaomba wanisikilize kwa dakika chache.
"Nilipotoka, nilikwenda kupiga simu. Kuwasiliana na nyumbani nchini Tanzania."
Niliwaongopea kutokana simu nilipila siku mbili za nyuma.
"Nilitaka kujua hali ya mama, ila nikaambiwa kwamba ni mgonjwa sana, amepalalaizi na hawezi kufanya kitu chochote"
Nikamuona Phidaya akistuka kwa taarifa hiyo.
 
"Sasa imekuaje!?"
"Matatizo nahisi ni mambo yao yakisiasa, wamechezeana."
Ilibidi kuficha kwamba John ndio chanzo wa tatizo la mama, baada ya kumuua Fredy ninaye fanana naye sana.
"Dady wamemchezea bibi mziki?"
Swali la Junio likatuashiria kwamba haelewi kitu tunacho kizungumza kwa wakati huu.
"Eheee"
"Kina nani hao?"
"Watu tu utakwenda kuwaona mukienda Tanzania"
"Ngoja Eddy, umesema tukienda Tanzania, ina maana wewe hauendi?"
"Kuna kazi itanilazimu kuifanya hivi karibuni, itawalazimu nyinyi kwenda kabla yangu."
"Kazi gani?"
"Nilikuambia nitakuambia, nikitulia mke wangu"

   Tukamaliza mazungumzo, nikaondoka na kuingia chumbani kwetu, nikafanya maandalizi ya kulala, baada ya muda Phidaya akaingia na kukaa kitandani
"Baby ni kazi gani inayo kufanya ubaki huku peke yako"
Phidaya aliniuliza kwa sauti ya upole, huku akinichezea chezea kifua changu.
 
"Yakumuua John"
"Kumuua John!!?"
"Ndio, nimemuona leo, na ninatambua anapo ishi."
"Sa..sa sasa itakuwaje akituona, si atatuua?"
"Kwa sasa hawezi kuniua"
Nikaanza kumuadisia Phidaya kuanzia mipango ya harusi ilivyo pangwa, hadi kuuawa kwa Ftedy.
"Kwahiyo wanaamini wewe umekufa?"
"Ndio maana yake, nahitaji mutangulie nyumbani mimi niimalizie kazi hiyo ya kumuua yeye kwa mkono wangu."
"Eddy kuwa makini, sihitaji kukupoteza katika hili"
"Usijali mke wangu, nipo makini tena sana"
Tukakumbatiana na Phidaya. Akaingia bafuni akaoga, kisha akarudi kitandani na kujilaza.
"Unajua mama anaweza akapona?"
"Ataponaje?"
"Sisi madaktari, tunambinu za kuwafanya watu walio paralaizi, kuweza kutembea tena"
Maneno ya Phidaya yakanipa matumaini mapya juu ya uwezekano wa mama yangu kupona. 
 
"Mjkienda Tanzania, kuna mtu atawapokea"
"Atatujua?"
"Ndio picha zenu anazo"
"Sawa ila nakuomba Eddy, urudi"
"Nitarudi mke wangu. Tena ngoja nimpigie uzungumze naye"
Nikachukua simu ya mezani na kumpigia Blanka.
"Ndio kaka"
"Hali ya mama inaendeleaje?"
"Kidogo anaonyesha matumaini, japo si sana"
"Msalimie wifi yako"
"Anajua kiswahili au ndio kuch kuch hotae?"
"Anajua mbona, tena zaidi yako"
Nikampa simu Phidaya akazungumza na Blanka, kisha Phidaya akanirudishi simu.
"Ehee kesho kutwa watakuja Tanzania. Watafutie nyumba maeneo ya Masaki au Mbezi beach mimi nitarudi wiki moja baadaye"
 
"Kaka pesa sina kwa sasa"
"Watakuja na pesa zao wenyewe"
"Poa kaka Eddy sasa nikawapokee Ubungo au wapi?"
"Kwa akili zako hujajua hii namba inatokea nchi gani. Kama ni yatanzania kawapokee Ubungo, kama ni ya nchi za watu wakukute uwaja wa ndege"
"Haaaaaa haya mwaya kaka"
Nikakata simu nikimuacha Blanka akicheka kwa jibu nililo mpa.
  Usiku mzima ukawa ni usiku wakuwaza jinsi gani nimuue John pasipo mimi kutiwa hatiani, na kujisababishia matatizo mapya. Nikamuacha Phidaya peke yake kitandani akiwa amepitiwa na usingizi, mimi nikaelekea sebleni. Kitendo cha mimi kukaa kwenye kochi, Shamsa akatoka chumbani kwake.
"Mbona hujalala, hadi sasa hivi?
"Nimekosa tu usingizi, baba"
"Kichwa bado kinauma?"
"Hapana, kichwa hakiniumi, ila kuna jambo linaniumiza sana akili yangu"
 
"Jambo gani?"
"Nikuhusiana na hiyo kazi unayo hitaji kuifanya. Naomba na mimi niwepo"
"Noo Shamsa, hii vita ni yangu na yule John niliye kuadisia"
"Sawa Eddy, ila nahitaji kuwa karibu nawe kutokana wale wezangu wananitafuta kila kona ya dunia hii"
"Kwa nini wanakutafuta?"
"Huwa kwenye kundi lile mtu akitekwa basi nilazima atafutwe popote alipo, kuhofia kutoa siri zao"
"Mmmmm"
"Na mbaya zaidi, wanashirikiana na Al-Kaida ambao nilisha wahi kufanya kazi kwenye kundi hilo zaidi ya mara nane"
Nikabaki nikimshangaa Shamsa kwani hii habari anayo niambia ni ngeni kwenye masikio yangu na niyahatari kupita zote nilizo wahi kuzisikia kwenye maisha yangu. Kwani kundi la Al-Kaida, linatafutwa na nchi kubwa hususani Marekani. Je vita ya mimi peke yangu nitaiwezaje.
"Nikiwa na familia yako, ninahofia kuitia matatizoni kwa ajili yangu, na wale wanavyo jua ni kwamba umeniteka"
"Picha za zenu mulizo ziweka Facebook nahisi ndio chanzo?"
 
"Hizo ndio zilizo niharibia mimi kila kitu, najuta kuziweka. Wanenitumia ujumbe facebook"
"Upo wapi?"
Shansa akanyanyuka na kuingia chumbani kwake, akarudi akiwa ameshika laptop. Akaiweka mezani na kuufungua ujumbe alio tumiwa ambao umeandikwa kwa maandishi ya kiarabu.
"Yana somekaje?"
"Wanasena hivii. MIKONO YAO INAVUJA DAMU, ILIYO SABABISHWA NA WEWE. TUTAKUTAFUTA DUNIA NZIMA. DAMU YAKO ITAKUWA KINYWAJI CHETU."
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio, huku wasiwasi mwingi ukiwa umenijaa moyoni mwangu. Nikamtazama Shamsa jinsi alivyo poteza raha.
 
"Tutafanyaje Eddy na huu ujumbe ni wakwako?"
Sikujua hata nimjibu nini Shamsa zaidi ya kumtazama tu machoni.
"Eddy hapa nilipo raha yote imetoweka moyoni mwangu, sijui hata tunawakimbiaje?"
"Fanya hivi, ifute hiyo account"
"Alafu?"
"Nitajua ni jinsi gani ya wewe kwenda Tanzania. Natambua kuwa kule mutakuwa mupo salama zaidi"
"Una uhakika?"
 
"Ndio ninao uhakika huo. Ila nakuomba uandamane na familia yangu"
Shamsa akakaa kimya kama dakika tano, huku akiwa amesongwa na msongamano wa mawazo kichwani mwake.
"Nitakwenda nao kuhakikisha wanafika salama"
"Asante Shamsa"
"Wewe je, usalama wako utakuaje?"
"Hilo musilihofie sana, nilipo toka nimbali sana"
Nikamfwata na kumkumbatia Shamsa. Nikamruhusu arudi kulala. Mimi nikaendelea kukaa sebleni nikiwa sina amani moyoni mwangu kabisa, huku mawàzo mapya ya Al-Kaidah yakinitawala kichwani
                ***
  Muda wa sherehe ya Junio ikawadia, tuliamua kuialika familia ya jirani yetu. Ambaye alikubali kujumuika nasi, akiwa na mke wao na mtoto mmoja. Ili kuinogesha sherehe, tukaimba wimbo wa siku ya kuzaliwa unao tumika kuibwa katika siku za kuzaliwa.
¶Happy birthday to you×2¶¶
¶Happy birthday ni ya Junio, Happy birthday to you¶¶
   Junio akaizima mishumaa iliyopo juu ya keki kwa kuipuliza kwa nguvu. Mama yake akaanza kukata vipande vidogo vidogo vya keki. Baada ya kumaliza Junio akaanza kutulisha mmoja baada ya mwengine. 
 
"Jamani kuna kitu nahitaji nikifanye, mbele yenu"
Nilizungumza huku nikitabasamu, nikawafanya watu wote kukaa kimya wakisubiria kitu hicho ninacho taraji kukifanya. Taratibu nikamfwata Phidaya alipo, nikapiga magoti huku nikitoa kisanduku kidogo mfukoni mwa suruali yangu, kilicho hifadhi pete ya dhahabu, niliyo inunua siku tulipokua tukifanya manunuzi ya vitu vya Junio, pasipo mtu yoyote kujua hilo.
"Phidaya, upo tayari kuwa mke wangu?"
Nilizungumza kwa sauti ya unyonge na kumfanya Phidaya kuanza kumwagikwa na machozi yafuraha.
 
"Ndio Eddy"
Nikauchukua mkono wa kushoto wa Phidaya, na kuivisha pete kwenye kidole kinacho paswa kuvishwa pete ya uchumba. Watu wote wakapiga makofi ya furaha, huku jamaa tuliye mualika akichukua picha za video kwa kamera yetu. Phidaya akaninyanyu na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa furaha sana.
"Nakupenda Eddy mume wangu"
"Nakupenda pia mke wangu"
Hatukujali uwepo wa watu waliopo ndani ya seble yetu, tukajikuta mimi na Phidaya, tukinyonyana midomo yetu, kwa hisia kali za kimapenzi, zilizo changanyika kwa furaha nzito.
"Mmmm sasa tusherekee"
Shamsa alizungumza huku akiwasha redio kubwa iliyopo sebleni hapa. Kusema kweli japo ni sherehe ya watu wachache, ila ilitupa furaha kubwa sana mioyoni mwetu, huku kila mmoja akionekana kuridhika kwa matukio yote yanayo endelea katika sherehe hii.
 
Hadi inafika jioni kila mmoja akawa amechoka kwa kucheza mziki. Nikatoka na jamaa, niliye mualika kwenda nje kupunga upepo huku Phidaya akibaki na mke wa jamaa, aliye jitambulisja kwa jina la Jordan, pamoja na watoto wetu
"Nimefurahi sana kaka Eddy kunialika kwenye sherehe hii ya leo, kusema kweli ipo boma sana"
"Hata mimi nafurahi kwa kuja kwako, hivi wewe ni mwenyeji wa wapi?"
"Florida Marekani. Wewe je?"
"Tanzania"
"Safi sana, alafu kama nilisha wahi kukuona kwenye matangazo ya magari ya Ford yaliyo zinduliwa mwaka huu?"
"Ndio mimi"
"Du kumbe nipo na mtu mkubwa"
"Kawaida hivi unajishuhulisha na nini?"
"Mimi ni mzalishaji wa movie Hoolywood"
Tuliendelea kuzungumza mambo mengi na jamaa hadi majira ya saa tatu usiku tukarudi juu gorofani. Tukajumuika na familia zetu kupata chakula cha usiku, kisha wao wakaondoka na kurudi vyumbani mwao.
             ***
  Mipango ya kukata tiketi za ndege katika shirika la KLM kwa kupitia mtandao likakamilika usiku.  Muda wa ndege kuondoka ni saa tano asubuhi, ikatulazimu kufika uwanja wa ndege saa nne asubuhi, ambapo, nikakabidhiwa tiketi tatu nilizo zikata usiku wa jana. Nikawakabidhi kila mtu tiketi yake pamoja na namba za Blanka niliye mpa taarifa juu ya kuupokea ugeni wa familia yangu.
 
Nikamkabidhi Junio na Shamsa kila mmoja kiasi cha dola elfu ishirini, wazitunze na zitawasaidia kukiwa na tatizo lolote. Nikamkapa Phidaya dola laki moja na nusu za kumsaidia.
"Nakuomba hizo pesa uzitumie vizuri, japo kwa Tanzania ni pesa nyingi sana, ila kuwa nazo makini"
"Sawa baba Junio"
"Walinde wanangu"
"Nitawalinda, nakuomba na wewe ujilinde mume wangu ninakuhitaji zaidi ya chochote kwenye maisha yangu"
"Sawa mke wangu"
Nikamkumbatia Phidaya, kisha nikamfwata Junio.
"Mlinde mama sawa?"
"Sawa dady"
"Nakuaminia wewe ni mwanaume"
Nikamkumbatia Junio na kumpa tano. Nikamfwata Shamsa aliye onekana muda wote macho yake yakiwa juu juu.
 
"Vipi?"
"Hakuna, kitu baba"
"Ok kuwa makini na familia nzima. Ninakuamini huto niangusha. Mlinde mdogo wako na mama yako"
"Sawa dady"
"You call me dady again?"(Umeniita baba tena?)
"Ndio, unanipa mapenzi bora kama niliyo kua nikiyapata kwa baba yangu.Mungu akubariki"
"Asante kwa kulitambua hilo"
"Nakutakia kazi njema dady"
"Nanyi pia nawatakia safari njema"
Nikawakumbatia wote watatu, nikawaacha waelekee kwenye foleni ya mizigo yao kukaguliwa. Mimi nikaondoka, nikachukua taksi iliyo nifikisha kwenye maduka ya urembo. Nikanunua ndevu bandia.
"Jamani nimepungukiwa na dola kumi nisaidieni tu kuipata hii pochi"
 
"Hatushushi bidhaa zetu, bei ni hiyo tu, chukua pesa yako uondoke dada"
"Lakini jamani kuweni na utu, katika hili. Dola kumi pia munashindwa kunipa hii pochi"
Niliyafwatilia mazungumzo ya muhudumu na dada mmoja aliye shika pochi, aliyo onyesha kuipenda sana. Nikatoa dola mia na kumpa muhudumu huyo anaye bishana na dada huyo anaye onekana ni muongeaji sana.
"Chenchi itakayo baki utampa huyo dada"
Nilimuambia muhudumu huyo, huku nikiwatazama machoni. Nikachukua mfuko wangu nilio nunua vitu ndani ya duka hili ikiwemo sura ya bandia. Nikatoka nje ya duka na kutazama tazama uwezekano wa kupata usafiri wa taksi.
 
"Naitwa Prety wewe je?"
Dada niliye mlipia pochi dukani, alizungumza huku akiwa amesimama pembeni yangu. Huku akiwa amebeba jifuko kubwa lenye vitu vingi ndani yake.
"Eddy. Taksi"
Niliita taksi inayo katiza pembeni yetu.
"Hapana wewe nenda"
Prety alimruhusu dereva wa taksi hiyo kuondoka jambo lililo anza kunikera.
"Mimi nina gari yangu, ile pale nyekundu"
Alinionyesha kagari kadogo, kanako fanana na gari la mchekeshaji maarufu duniani Mr bean.
"Lile ndio gari lako?"
"Ndio twende tukapande"
Prety akanishika mkono hadi kwenye kagari hako. Akanifungulia mlango nikaingia, kisha yeye naye akaingia.
'Mungu wangu hiki kikipata ajali hatutoki humu'
Nilijisemea kimoyo moyo.
"Unakwenda wapi?"
Nikamtajia hoteli ninayo kwenda, akaonekana kufurahi.
"Mimi ninakaa hoteli ile ya pili yake. Nina mwaka sasa ninaishi pale"
"Una kazi gani inayo kufanya ukae pale kwa kipindi chote hicho?"
 
"Ohoo mimi ni mtaalamu wa mambo ya mtandao, chochote unacho hitaji kwenye mtandao ninaweza kukutafutia"
Prety ni muongeaji sana, kiasi kwamba nikajikuta nikiwa ninamshangaa.
"Kabla hatujafika kwako, twende ukapaone kwangu kisha ndio uende kwako"
"Kwa nini?"
"We twende tu"
Nikaanza kumtilia mashaka huyu Prety, isije akawa ametumwa na John. Nikajipa moyo hawezi kunifanyia chochote. Tukafika hotelini, tukaelekea kwenye chumba chake kilicho gorofa ya tano
Chumba chake kimejaa computer si chini ya kumi na zote zimewashwa. Akaanza kuminya moja baada ya nyingine akitazama ujumbe ulio ingia.
"Hapa ndio kwangu, jisikie huru"

   Nikashangaa kumuona Prety akivua sura yake, aliyo nayo. Ndipo nilipo gundua ni sura ya bandia. Akabaki na sura yake halisi ambayo ni nzuri sana.
"Mbona unashangaa?"
"Nashangaa kukuon unavua sura ya bandia"
"Yaa unajua mimi ni Mrashia, dili zangu nyingi ni wizi katika mabenki makubwa na watu matajiri duniani. Huwa siwezi kuifanya kazi yangu kwa sura yangu halisi"
 
"Kwa nini unakua mwizi?"
"Ndio kipaji changu, njoo uone"
Akanipeleka kwenye chumba kimoja, kilicho jaa mitambo mingi kiasi, pamoja na picha nyingi za wasichana kwenye ukuta
"Hii mitambo huwa ninaitumia kutengeneza sura za wasichana ninao hitaji kufamana nao.
"Mmmm"
Akanionyesha jinsi ya anavyo tengeneza sura hizo za bandia. Sikujua ni kwanini emeniamini kwa muda mfupi.
"Kwa nini umeniami na kunileta chumbani kwako. Kama mimi ni askari je?"
 
"Hakuna mtu mwenye kuwajua askari wa nchi yoyote duniani kama mimi. Ungekua askari wala pesa yako nisinge ipoke"
Tukarudi sebleni ambapo akanipa kiti nikae nitazame tazame jinsi anavyo weza kuiba vitu kwa mtandao hususani pesa ndani ya mabenki.
Katika kufungua fungua baadhi ya picha nikamuona John na Sheila.
"Hembu rudisha nyuma hiyo picha niione vizuri"
Akafanya kama nilivyo muagiza, nikaitazama vizuri picha hiyo.
"Hawa ni najirani wangu, nimegundua nao ni matajiri sana. Nipo kwenye mpango wa kuwaibia pesa zao benki. Tena nimesha jenga urafiki na huyu dada."
"Anaitwa nani?"
"Coletha Agray"
 
Nikashangaa jinsi Sheila alivyo badilisha jina.
"Ahaaa naomba unionyeshe chooni"
Prety akaniobyesha chooni, nikaingia huku nikijitahidi kuficha wasiwasi wangu wa kuwajua John na Sheila. Baada ya muda nikasikia Prety akimkaribisha Coletha ambaye ndio Sheila, Nikatoka chooni na kujibanza sehemu ninapo weza kuiona seble vizuri. Nikamuona Sheila akikaa kwenye sofa, huku akiwa na tanasamu na furaha.
'Sheila kifo chako kitakua cha taratibu taratibu, sina haraka na wewe'
Nilijisemea komoyo moyo huku nikimtazama Sheila au Coletha Agrey. Anavyo shusha mafumba ya juisi aliyo andaliwa na Prety
==> ITAENDELEA

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx