test

Jumanne, 8 Novemba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 37 & 38



Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA      
“Detener inmediatemente”(Simamisha hapo hapo)
Frednando alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya muongozaji wa video hiyo kusimamisha sehemu inayo muoenyesha Mercy akimkumbatia Rahab kwa furaha. Mercy akajikuta akiitumbualia macho sehemu hiyo iliyo simamishwa huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana.

ENDELEA  
Kila mmoja aliweza kulishuhudia tendo la Mercy kumimini kiasi cha unga unga mweupe kwenye kinywaji alicho kishika Rahab, pasipo watu wengine kuweza kumuona wakati wa sherehe hiyo kuweza kufanyika. Walio na roho nyepesi wakajikuta wakimaka kwa sauti ya juu, Mercy baada ya kuona kwamba ameweza kugundulika kwa haraka, akapandisha juu gorofani na kuingia chumbani kwake kwani anagundua kinacho kwenda kutokea ndani ya masaa machache mbeleni hakitakuwa ni kizuri kwani anautambua vizuri ukatili wa bosi wake.

Mercy akafungua kabati lake na kutoa begi dogo la mgongoni na kuanza kuingiza kiasi cha pesa alicho kuwa amekihifadho ndani ya kabati hilo kisha kwa haraka akafungua dirisha na kusimama, kabla hajafanuya chochote mlango wake ukapigwa na teke wakaingia walinzi wawili wa Frednando wakiwa na bunduki mikononi mwao

                                                                                           ***
Hali ya Fetty na wezake, zikazzidi kushuhulikiwa na madaktari bingwa waliomo ndnai ya ngome ya bwana Rusev, komandoo wa nchi ya Rusev aliye weza kuisaliti nchi yake na kuunda kikosi chake alicho kipa jina la R.U.P.P(Rusev United Power of People). Kikundi hichi aliweza kukianzisha kwa siri kubwa tangu akiwa ndani ya jeshi pasipo watu wengine kuweza kukifahamu kwa haraka.

Akaweza kutengeneza kambi yake chini ya bahari kaskazini mwa nchi yake ya Urusi, haya yote aliweza kutafanya kwa siri kubwa akishirikia na baadhi ya viongozi wa juu serikalini walio kuwa na uchu mkubwa wa madaraka. Mbaya zaidi ni kwamba viongozi hao walitaka kumgeuka, ila kwa kutumia umahiri wake aliweza kuwaangamiza kwa mkono wake mwenyewe kuhakikisha kwamba siri yake haiwezi kuvuja kwa mtu wa ina yoyote kwamba yeye anamiliki jeshi kubwa la vijana kinyume na sheria za nchi yake..

R.U.P.P, ikazidi kukua miaka kwa miaka na kuzidi kupata wataalamu wakubwa wa mitambo na kuanza kutengeneza silaha za nyuklia kisiri sana.
Ndani ya miaka ishirini ya usiri, siku moja bwana Rusev aliweza kuja kujikuta siri yake ya kuwa ni muasi ndani ya nchi yake ikagundulika, hii ni baada ya siku hiyo kunywa kiasi kikubwa sana cha pombe na kujikuta akilala ma malaya mmoja aliye weza kumpa penzi tamu, hadi akajikuta akianza kumuambia mambo yake ya ndani huku akimuahidi kumpa nafasi ya kuweza kufanya naye kazi.

Binti huyo pasipo kuwa mvumilivu akajikuta akijinadi kwa rafiki zake, juu ya kupata nafasi ya kuajiriwa na bwana Rusev katika kikosi chake cha siri cha R.U.P.P, hii ni mara baada ya binti huyo kutoka kulala na bwana Rusev ambaye kwa kipindi hicho bado alikuwa ndani ya jeshi la nchi ya Rusia.     

     Bwana rusev hakuwa na jinsi zaidi ya kuamua kuiasi nchi yake mara baada ya serikali kuanza kumfwatilia na kumuwekea vikwazo vingia hadi kutaka kumuhukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa, ila haikuwa ni rahisi  kwa serikali, kwnai watu wa bwana Rusev waliweza kumtorosha kiongozi wao huyo walio muabudu kama Mungu wao, na kuweza kumuweka katika mazingira salama ambayo ni ngumu sana kwa mtu yoyote kuweza kumfikia na kumdhuru.
“Jamani tupo wapi?”

Anna alikuwa wa kwanza kuzungumza mara baada ya kuzinduka kutoka usingizini. Akashangaa eneo zima la chumba kikubwa walicho lazwa na kilicho tawaliwa na rangi nyeupe kwenye kuta zake kuanzia chini, pembeni hadi juu. Akawatazama wezake na kuwakuta bado wakiwa wamejilaza kitandani, huku wakiwa na madripu ya maji. Anna akajitazama na yeye na kujikuta akiwa na dripu kwenye mkono wake wa kushoto, nguo walizo kuwa wamezivaa mara ya mwisho hawakujikuta nazo, alijishuhudia akiwa amevishwa mavazi meupe yanayo fanana na wezake.
Baada ya muda kila mmoja akazinduka na wote wanne wakajikuta wakipiwa katika hali ya kuto fahamu ni kitu gani ambacho kinaendelea katika eneo walilo kumbuka.

“Jamani hapa tulipo tunaonekana kila kona”
Fetty alizungumza baada ya kuzitazama kamera za ulinzi zilizo kuwa katika kona nne za chumba walichomo.
“Sasa kamani tutafanyaje, kwa mana hapa mimi sielewi?”
Halima aliuliza akiendelea kuyapepesa macho yake
“Kikubwa tuweni wapole, kwa maana kama hawa watu wangekuwa ni wabaya kwetu wanegesha tuu, ila wemeweza kutuhudumia hadi hapa”
Fetty aliwasisitiza wezake, kabla Agnes hajazungumza, bwana Rusev akaingia huku akiwa ameongozana na walinzi wake wawili pamoja na daktari mmoja, mwenye umri mkubwa kiasi.

“Munaendeleaje mabinti”
Bwana Rusev alizungumza kiswahili fasaha kilicho wafanya wote wanne kushangaa na kumtumbilia macho kwani siku zote walikuwa wanajua kwamba mzee huyo atambui kishwahili
“Munanishangaa mimi kuzungumza kishwahili? Ok tuachane na hayo, kama munavyo weza kujionea mupo katika mikono salama sana, na kwaupande mwingine pia si salama”
Fetty na wezake wakatazama kwa macho yakujiiuliza ni kwanini Bwana Rusev anasema sehemu hiyo ni salama ama si Salama, hapakuwa na aliye kuwa na jibu la kuzungumza kwa mwenzake zaidi ya kukaa kimya kusubiri ni kitu gani ambacho bwana Rusev atazungumza.

“Natambua kwamba nyinyi ni miongoni mwa mabinti mahiri mulio weza kufanya matukio kadhaa kwenye nchi ya Tanzania, na pia hadi sasa hivi bado munaendelea kutafutwa si ndio?”
Anna akajibu kwa kutingisha kichwa akikubali kwamba ni kweli bado wanatafutwa
“Sawa sasa ni hivi, nawapa uchaguzi wa haya nitakayo kwenda kuyazungumza. Kwanza mukikubali kuwa na mimi nitawapa nafasi kubwa ya kuyatambua mambo mengi ambayo hamjawahi kuyajua. Pili mukikataa kuwa na mimi miili yenu itakuwa ni chakula cha papa walio zunguka eneo hili.”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx