test

Jumanne, 22 Novemba 2016

MBUNGE MTATA WA UPINZANI ARUSHA MJINI AZIDI KUPIGA UKUTA MAHAKAMANI NA KURUDISHWA RUMANDE LIVE LEO!!




Hatima ya Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Jonathan Lema itajulikana siku ya leo, kupata dhamana Au lah!



Kesi ya Jinai namba 440,441inayomkabili Lema itasomwa tena siku ya jumanne leo kama ilivyoamuliwa na Mahakama ya hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha tarehe 17 novemba 2016.


================= 
Tayari Mbunge Godbless Lema ameshaingia mahakamani Na saa anashauriana na mawakili wake.
 
Mawakili upande wa serikali wanajitambulisha pamoja na mawakili upande wa Mbunge.
 
Hakimu anapitia marejeo ya kesi ya nyuma iliyofanya Lema asipewe dhamana.
 
Hakimu anatoa rulling anajibu hoja za upande wa serikali kwa queries walizozileta.
 
Hakimu anasema mshtakiwa ana haki ya rufaa na rufaa ni haki yake.
 
Hakimu ameondoa rufaa kuna mambo ya kisheria
 
Hakimu anasema Mawakili walitakiwa kukata rufaa kwenye ile ile Mahakama ya Mwanzo kwa Hakimu Mkazi, ndio mawakili wanaenda kushughulikia na sio kuomba review.
 

Mahakama kuu kanda ya Arusha imetupilia mbali maombi ya mawakili wa Lema ya. kufanya marejeo ya hukumu ya dhamana. Hivyo Mawakili wa Lema wanakata Rufaa kwa hati ya dharura na kesi itasikilizwa tena.
Mawakili wanakata rufaa ndani ya masaa mawili.
Mbunge wa Arusha mjini Lema ametolewa kwenye viwanja vya mahakama kuu, na tayari amepelekwa gerezani, baada ya muda tutawajulisha kinachoendelea, Wakili Peter Kibatala ataongea na Waandishi wa Habari hapo baadae.
 
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema amesharudishwa magereza wakati mawakili wake wakiendelea kukataa rufaa ya kuzuia dhamana.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx