test

Alhamisi, 20 Oktoba 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 71 & 72 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


MUANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA
John akanisogelea hadi sehemu tuliyo jilaza, akanitazama kwa muda, mimi pamoja na mwanangu aliye anza kulia
“Mwanao ni mzuri sana”
John alizungumza huku akimtazama mwanangu pamoja na mama yake aliye jilaza, akiwa ameishiwa nguvu za mwilini mwake
“Goodbye my friend”(Kwaheri rafiki yangu)
John alizungumza kwa sauti ya upole nikastukia risasi kadha zikitua kifuani mwangu na kuninyamazisha kimya katika sehemu niliyo lala

ENDELEA
Sauti ya milio ya ndege nikaanza kuisikia kwa mbali kwenye masikio yangu, taratibu nikajaribu kuyafumbua macho yangu kuweza kuona n kitu gani kinacho endelea ila, ukungu mwingi umawa umetawala kwenye mboni yamacho yangu, jamvo lililo nifanya nisione kitu cha aina yoyote, nikajaribu kupapasa katika sehemu niliyo lala, nikagundua kwamba nimelalia kitanda cha kamba, ila sikuweza kutambua ni sehemu gani niliyopo.Muda jinsi ulivyo yoyoma ndivyo nilivyo weza kugundua kwamba eneo nililopo, kuna watu wanao zungumza lugha nisiyo ijua
"Nipo wapi?"

Nilijarivu kuzungumza huku nikijitahidi kunyanyuka kutoka katika kitanda nilicho lala ila milono ya watu si chini ya wanne wakanirudusha kulala tena kwebye kitanda.Sauti za wanaume pamoja na wanawake zikaendelea kupenya kwenye masikio yangu, nilipo anza kusikia milio ya watoto wadogo wakicheza na wengine kulia ndipo nilipo amini kwamba eneo hili ni salama kwa maisha yangu

 Nikawasikia wakiendelea kunong'oneza, mara sauti ya kike ikasikika, ambayo sikuweza kuisikia tangu wàlipo anza kuzungumza watu hawa, ambao hadi sasa hivi siwezi kuwaona vizuri zaidi ya vivuli vyenye giza, vilivyo simana pembeni ya kitanda nilicho kilalia.Nkasikia wakiyazungumza maneno niliyo yasema dakila kadhaa za nyuma nikiwauliza kwamba hapa nilipo ni wapi
"Hei"
Sauti ya msichana hiyo ilinisemesha, ila sikujua anataka kusema kitu gani
"Nipo wapi, dada?"

Nliyarudia maneno yangu niliyo yazungumza hapo awali
"Unazungumza kiswahili wewe?"
Msichslana huyo aliniuliza, kwa lugha ya kiswahili jamvo lililo nifanya nizidi kufarijika moyoni mwangu na kuamini kwamva nimepata mwokozi katika wakahi huu mgunu nilio nao katika yangu maisha
"Ndio, ndio dada"
Niliitikia kwa haraka ila hata ninaye zungumza naye asibadili mawazo ya kunisaidia mimi
"Unaitwa nani?"
"Eddy, Eddy dada yangu"
Nikamsikia msichana huyo akizungumza na wezake huubakilitaja jina langu, kwa wezake ambao ninaamini hawaijui lugha ya kiswahili tunayo zungumza
"Umetokea wapi?"
"Tanzania dada yangu"
"Ulikuja huku kufanyaje?"
"Wapi, kwani hapa ni wapi?"

Kabla sijajibiwa nilicho kiuliza nikasikia sauti za watu waliomo ndani ya chumba wakisalimia kwa pamoja kwa kutumia lugha wanayo izungumza, sauti nzito ya mwanaume ikaitikia na kuwafanya watu wote kukaa kimya ndani ya chumba tulichopo
"Mumesema, ameamka?"
Mwanaume huyo alizungumza kiswahili cha kuvuta maneo, akionekana kwamba hakifahamu vizuri
"Ndio baba, na anazungumza kiswahili"
"Amesema ametokea wapi?"
"Tanzania, ila hajanitaji ni sehemu gani"
Mwanaume huyo akaendelea kuzungumza kilugha chao, baada ya muda akatoka ndani ya chumba tulichopo
"Eddy baba amrsema tukuache upumzike"
"Ndoja kwanza, unaitwa nani?"
Msichana huyo akakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akajikoholesha kidogo kuliweka koo lake vizuri kisha akanijibu kwa upole
"Nitakujibu, ukiwa vizuri"

Nikamsikia akitoka ndani ya chumba nilichopo, nikajipapasa kifuani mwangu, na kukuta kitambaa kigumu kikiwa kimefungwa kuzunguka usawa wa kifua changu chote
"Ehee Mungu warehema, nisaidie mimi mja wako"
Nilizumgumza kwa sauti ya chini, huku nkihisi machozi yakinitiririka pembezoni mwa macho yangu.Kumbukumbu za maisha yangu ya nyuma nilipo kua bado mdogo zikaanza kunijia kichwani mwangu, picha ya sura ya mana yangu ikaanza kunijia kichwani na iukumbuka baadhinya matukio ya furaha aliyo kua akinifanyia

'Eddy mwanangu jaribu kuishinda hasira yako'
Nimaneno ya mama, niliyo anza kuyakumbuka vizuei na hili tukio lilitokea kipindi nilipo mpiga mwenzangu nilipo kua chekechea hadi akapoteza maisha akiwa anakimbizwa kupelekwa hospitalini
'Usiwe mjinga na wewe utakubali vipi kupigwa na mwanaumwe mwenzio'
Nimanenoya mzee Godwin, alipo kua akinifundisha mbinu za kupigana baada ya kupugwa sana na wezangu nilipo kua darasa la kwanza
'Mwanaume halisi, hupambana hadi dakika ya mwisho ya uhai wake'
'Hata ikiwezekana kutoa roho ya mtu wewe toa tu, ili mradi uwe msindi'

Nimaneno menfine ya mzee Godwin alipokua akinifundisha kadei siku zilivyokua zikienda jambo ambalo alinifanya na mimi ka katili na roho ya kinyama tangu nilipo kua mdogo.
'Uwe unasamehe saba mara sabini, kwani Mungu anawasamehe wale wote walio mkosea'
Nimaneno mengine ya mama, alipokua akinifundisha kusoma biblia kabla ya kulala, kwani alipenda kunikuza katika mazingira ya kidini na kumujua Mungu
'Mimi baba yako, nihodari sana wa kuua pale ninapo kua kwenye uwanya wa vita, risasi yangy moja inapo toka kwenye mdomo wa hii bastola yangu, hua nilazima imuangamize mtu'

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx