test

Jumanne, 4 Oktoba 2016

Kufuatia mauaji ya kinyama DODOMA vyombo vya usalama kuhakikisha wafanyakazi wa NIDA wanafanya kazi kwa usalama



Kufuatia  mauaji ya kinyama kwa watafiti wa Udongo na Maendeleo ya Ardhi  yaliyofanywa na wanakijiji wa  Iringa  Mvumi wilaya ya CHAMWINO Mkoani DODOMA Mkuu wa wilaya ya Tabora Aggrey Mwanry amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Tabora kuhakikisha wafanyakazi wa NIDA wanafanya kazi katika hali ya usalama.
Mwanry ameyasema hayo wakati akizindua rasmi zoezi la usajili wa vitambulisho vya Taifa kwa watumishi wa umma  ambalo linafanyika katika maeneo yote ya mkoa wa Tabora huku akiwahakikishia usalama watumishi wa mamlaka ya hiyo
Nao wakuu wa wilaya  za mkoa wa Tabora wamewataka wananchi  kutoa ushirikiano wa kutoshai katika zoezi hilo
Zoezi la usajili wa vitambulisho vya Taifa limeanza rasmi kwa  kwa watumishi wa umma na baadae kwa wananchi wa kawaida ambapo kwa mkoa wa Tabora litafanyika  kwa siku kumi na nne.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx