Waziri Mkuu Kassim majaliwa amesema hayo katika hafla ya kupokea michango kwa ajili ya waaathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera ambapo makampuni zaidi ya 17 yamewasilisha michango yao ya vifaa na fedha zaidi ya shillingi million mia sita.
Pia waziri mkuu amesema serikali inaendelea na uchunguzi wa kubaini nani alikuwa akichukua pesa katika akaunti bandia iliyofunguliwa na baadhi ya watumishi wa umma kwa ajili ya kukusanya michango ya maafa.
Nao baadhi ya wasamalia wema na makampuni waliochangia misaada hiyo wamewataka watanzania wengine kujitokeza na kuchangia maafa hayo kwani hakuna sababu yakusubiri msaada kutoka nje.

