test

Jumatatu, 12 Septemba 2016

VIDEO KAULI YA WAZIRI NAPE KUHUSU KUKODISHWA NA KUUZWA KWA SIMBA NA YANGA


Jumamosi ya Septemba 10 2016 waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Moses Nnauye alitembelea kwa mara ya kwanza makao makuu ya shirikisho la soka Tanzania TFF toka ateuliwe kuwa waziri wa wizara hiyo, waziri Nape kaeleza kinachotakiwa kufanyika kuhusu suala la uuzwaji na kukodishwa kwa vilabu ikiwemo thamani za vilabu.

“Kumekuwa na mijadala ya mabadiliko ya mifumo namna ya kuendesha vilabu vyetu, huku wakitafuta kauli ya serikali hasa kuhusu michakato inayoendelea ndani ya Simba na Yanga, kimsingi serikali tunaunga mkono mabadiliko chanya katika vilabu, lakini cha kwanza michakato hii lazima iwe na uwazi na wala isigubikwe na rushwa”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx