Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya habari wa chama hicho Tumaini Makene,chama hicho kimetoa wito kwa watanzania wote wanaoishi katika maeneo yaliyoathirika na tetemeko hillo na wengine kutoka nje ya eneo hilo kuwiwa kutoa misaada kwa waathirika wa tukio hilo katika wakati huu mgumu wakukabilliana na wakati huu mgumu.
Amesema viongozi wa chama katika ngazi mbalimbali pamoja na wanachama wote wa Chadema wataungana na kusaidiana na waathirika kwa kila hali.

