test

Jumamosi, 24 Septemba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 13 & 14


MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA....
“Meneja hizo pesa nitoe za benki au zako binafsi?”
“Toa za benki mtu akikuuliza, muambia aje kwangu”
Bwana Turma akiwa anasubiria zoezi la kufungiliwa akauti, gafla milio mingi ya risasi ikaanza kusikika ikitokea nje na kuanza kuwachanganya bwana Turma na muhasibu wake


ENDELEA......
Kitendo cha wasichana, makatili kuiingilia bank ya CNB, na kuwazalilisha wananchi walio kuwemo ndani ya benki kwa kuwatoa nje uchi kinazidi kuiumiza serrikali.Isitoshe inamuwia ugumu Bwana Turma, na akashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano maalumu kwani gari lake la thamani, limehusika katika matumizi ya uvamizi wa Benki.
                                                                                            
Dickson anatoa nje ya kibanda chake, huku akiwa na wasiwasi mwingi akiwatazama askari wawili wanaokuja kwenye kibanda chake
“Habari yako kaka?”
Askari mmoja alimsalimia Dickson
“Salama tuu mambo vipi?”

Dickson alizungumza kwa kujikaza tuu, kuuficha wasiwasi wake kwa maana msichana ambaye ni Rahab aliye muacha ndani anaonekana hana masihara kabisa katika matumizi ya silaha

“Hukuona, msichana aliye vaa akipita katika maeneo haya?”
“Ahaaa kusema kweli, sijamuona kwa maana hizi bunduki kwa jinsi zilivyokuwa zikinguruma huko nje sikudhubutu hata kuitoa miguu yangu”

Askari wakamtzama kwa umakini Dickson, ambaye anazungumza kwa kubabaika
“ Basi tunakuomba ufunge duka lako”
“Sawa”
Askari wakaanza kuondoka na kurudi katika eneo walipo wazao, Dickson akarudi ndani huku jasho jingi lkimwagika mithili ya maji.
“Waameniambia nifunge”

Dickson alimsemesha Rahab ambaye kichwa chake amekiinamisha kwenye ukuta huku sura yake ikitazama juu.
“Dada, dada.Wamesema nifunge duka langu”
Rahab hakujibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya, huku akimtazama Dickson jinsi sura yake inavyo mwaga jasho jingi
“Powa”
Rahab alijibu kwa kifupi, na kuzidi kumchanganya Dickson
“U...takaa humu ndani?”
“Ndio wewe funga”
“Mmmm”

Dickson akabaki akiwa anashangaa  shangaa, Rahab akainyanyua bastola yake na kumuwekea Dickson ya kichwa, mwili mzima wa Dickson ukawa kama umepigwa na shoti ya umeme, taratibu suruali yake ikaanza kutengeneza mchoro sehemua ya zipu, kwani woga umemfanya hadi ameshindwa kuzuia haja ndogo
“Huwa sipendi, nizungumze mara mbili mbili.Potea”

Rahab alizungumza huku sura yake akiwa ameikunja, na anaonekana kuwa na hasira kali.Kwa hahara Dickson akatoka nje ya kibanda chake, na kuaanza kufunga geti la kaduka kake hata baiskeli anazo zitengeneza hakukumbuka kuziingiza ndani.Kwa kuchanganyikiwa akajikuta akitembea asijue ni wapi anaelekea
                                                                                                            
Wote wanne wakiwa na bunduki zao mikononi, wakawa wanaitazama njia ambayo ni yakuingilia kwenye eneo lao la handaki.
“Tutawanyike wawili wawili”

Fetty alizungumza huku akiikoki bunduki yake, Anna akamfwata Fetty huku Halima na Agnes wakiwa wamesimama sehemu moja.Wakatazamana kwa muda pasipo mtu yoyote kuzungumza neno , kisha wakaanza kukimbia mtuni, wakiwa wameganawana kila watu wawili sehemu yao.Fetty na Anna walielekea magharibi mwa msitu wao, huku Agnes na Halima wakielekea Mashariki mwa msitu wao.

Askari wakiongozwa na mbwa wao, walio fundishwa mafunzo maalumu ya kunusa kila sehemu ambayo amepita mtu ambaye askari wanamuhitaji, ndivyo walizidi kuendelea kuingia msituni wakiwa na bunduki zao.Huku kila mmoja akiwa na hasira kali juu, ya maauaji yaliyo tokea siku chache zilizo pita juu ya wezao walio uwawa kwenye kituo cha gesi kwa mlipuko mkali.Amri mmoja iliyo tolewa na mkuu wa jeshi la polisi Bwana Gudluck Nyangoi ni kwamba wahakikishe wanawatia nguvuni ili wahukumiwe kifungo kikali kitakacho ishangaza dunia

Askari wakiongozwa na Kamishina Msaidizi wa Polisi(ACP) Ngurumo, wanaendelea kuuzingira msitu huku wakiwa na imani ya kufanikiwa na abushi yao wanayo kwenda kuifanya kwenye msitu unao sadikika ndipo walipo ingia majambazi kipindi wakitokea kufanya tukioa benki, na maelezo haya yalitolewa na msamaria mwema ambaye, gari lao lilisimamisha kipindi askari wa usalama barabarani walipokuwa wakifanya uchunguzi kwa kila gari ambalo lilikuwa likikatiza katika barabara kuu ya kuelekea mikoa ya Tanga na Arusha

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx