test

Jumamosi, 12 Septemba 2015

Wachimbaji Tanzanite One watishia kugoma kutokana na kutoridhika na Mwekezaji.


Maelfu ya wafanyakazi katika mgodi unaomilikiwa na mwekezaji wa ndani wa Tanzaniate One Mining LTD katika mgodi uliopo mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara wameitaka  tume ya usuluhishi na uamuzi kuridhia matakwa ya kuanzisha mgomo usiokuwa na kikomo wa uchimbaji wa madini ya Tanzanite ili kutoa nafasi kwa mwekezaji huyo kurekebisha mikataba na kulipa madeni aliyoridhia toka kwa mwekezaji wa nje sambamba na kuboresha mazingira ndani ya mgodi huo ambayo yanahatarisha usalama wa afya zao.
Malalamiko hayo wameyatoa kwa katibu mkuu wa usimamizi wa makampuni ya uchimbaji wa madini nchini(TAMICO) Bw.Hassani Amir na kudai licha ya mgodi huo kutembelewa hivi karibunina waziri mwenye dhamana Bw.George Simba Chawene na kutoa malalamiko yao bila ya mafanikio huku wakishindwa kumtambua mkurugenzi wa kampuni hiyo kwa kuwa hajawahi kukutana na wafanyakazi hao tangu aliporithi toka kwa mwekezaji wa nje hali inayowanyima maslahi yao stahiki na kushindwa nani anastahili kuwalipa.
 
Hata hivyo katibu mkuu wa Tamico Bw.Hasani Amiri licha ya kupokea malalamiko ya wafanyakazi hao alipata wakati mgumu wa kukutana na uongozi wa kampuni hiyo ambao haukuhudhuria  kikao hicho huku afisa mwajiri Bw.Kirani Laiza alipotakiwa kutoa maelezo alionekana kushindwa kutoa maelezo akidai wafanyakazi hao walimkata mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Anthony Kukaimu nafasi hiyo.
 
Akitoa hitimisho kwa wafanyakazi hao huku akiwataka kuacha kugoma na badala yake akiahidi kutatua mgogoro huo ikiwa ni pamoja na kuipeleka  kampuni hiyo mahakamani kwa kuwa imekiuka makubaliano ya awali kwa kuvunja  sheria za wafanyakazi wa Migodini.
 

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni