test

Jumanne, 2 Juni 2015

Mrema alia na hujuma za CCM dhidi ya jimbo lake SOMA HAPA>>>>




Mbunge wa jimbo la Vunjo, Augustino Mrema, ameonesha kukata tamaa kutokana na kupewa tuhuma mbalimbali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusiana na ubadhilifu wa fedha jambo ambalo ni kunyume na ukweli uliopo.
 
Akichangia Bungeni mjini Dodoma, amesema kuwa anajua tuhuma hizo ni kutokana na  kutaka kumuangusha kisiasa ili kuweza kuchukua jimbo la Vunjo, na kudai kuwa kamwe wananchi wake wa Vunjo, hawashawishiwi kiurahisi kutokana na kuona juhudi zake katika kutafuta maendeleo.
 
Hizi ni sentensi alizoziongelea Mrema “Mimi pale Jimbo la Vunjo Shule ya Muungano iliungua, nilitoa Mil.21 kwenye mfuko wangu wa Mbunge ili kusaidia, mbona sioni Wizara mmetenga shilingi ngapi?”
 
“Mwisho akaja Katibu Mkuu wa CCM, na nyie CCM mmeanza kushiriki katika uongo.. Katibu Mkuu badala ya kwenda kuwapa pole kwenye Jimbo langu anasema ‘kila Jimbo lina mfuko wa Mbunge ambao ni Mil. 25 kwa miezi mitatu, kwa mwaka ni Mil.100, hamuwezi kuwa na Kiongozi ambae ni Mbunge na wakati huohuo ndie Mwenyekiti wa Mfuko huo, je si atajipendelea?’.. Naomba niulize Serikali, ni kweli Vunjo tumepata Mil. 400 kama alivyosema Kinana au mnanipakazia?”
 
“Kwa nini mnakuja kwangu mnasema maneno ya uongo nyie CCM? Kwa nini CCM mnanichangia kama mpira wa kona kule Vunjo? Kwa nini mnajiunga na Wapinzani kwa kusema maneno ya uongo?”
 
“Mlizonipa ni Mil.150 lakini mnaenda Vunjo mnawaambia watu nimechukua Mil. 400, naomba katika Mil. 400 mtoe hizo Mil.150 mnipe hiyo chenji tena leo hii”
 
“Kwa nini mnaenda kusema hivyo jamani mna ajenda gani na mimi? Uongo huu umenisononesha, na mimi nataka niwaambie CCM kwamba habadilishwi mtu kule Vunjo. Hizi mbinu zinazotumika kunidhoofisha.. Nataka chenji yangu nikafanye nayo Kampeni”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni