test

Ijumaa, 2 Juni 2017

Rwanda yataka kuchukua sehemu ya anga la Tanzania


Serikali ya Rwanda imeiliandikia barua Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) ikitaka kulidhibiti (control) eneo la Kati na Magharibi mwa anga la Tanzania.

Suala hilo limekuja wakati Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) ikijitahidi kulirejesha eneo la anga la mashariki. Eneo hilo linalojumuisha Madagascar, Mauritius, Moroni na Kisiwa cha Mayotte ambalo kwa miaka 39 limekuwa likidhibitiwa na Kenya kutokana na sababu za kiusalama. ICAO iliipa Kenya eneo hilo ilidhibiti kutokana na Tanzania haikuwa na rada za ulinzi za kutosha.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye gazeti la THE CITIZEN la Alhamisi Juni Mosi, 2017, ICAO bado haijaijubu Rwanda ambayo ina rada mbili za kisasa kwa ajili ya ulinzi wa anga.

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari alisema Tanzania kwa sasa inaweza kudhibiti anga lake lote kwa sababu ipo katika mchakato wa kununua rada nne mpya zenye thamani ya Tsh 61.3 bilioni.

Rada hizo zitafungwa katika viwanja vikubwa vitano vya ndege ambavyo ni Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo Dar es Salaam, Abeid Amani Karume Zanzibar, Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro, Mwanza na Songwe.

Mdhibiti ameweka pia Radio yenye ‘Frequency’ za juu kabisa (VHF Radios) eneo la Mnyusi Tanga ambazo zimegharimu Tsh 389.9 milioni.

Tumejidhatiti katika kuhakikisha tunadhibiti eneo letu lote la anga tofauti na sasa ambapo tunadhibiti asilimia 25 pekee ya anga letu kitu ambacho si  hakikubaliki, alisema Johari.

Kushindwa kwa Tanzania kudhibiti eneo la kati na magharibi na kuiachia Rwanda, ina maana kuwa Tanzania itakosa mapato yote yanayotokana na eneo hilo.

Tanzania imekuwa ikipoteza Tsh 1 bilioni kila mwaka kwa kushindwa kudhibiti eneo la mashariki ambalo kwa sasa lipo chini ya Kenya.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni