test

Jumatano, 31 Mei 2017

Breaking News: IGP Simon Sirro Kaongea na Waandishi wa Habari kwa Mara ya Kwanza na Kutangaza Dau la Milioni 10


MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro kwa mara ya kwanza amefanya mazungumzo maalum na wanahabari jijini Dar es Salaam na kutangaza dau nono la Sh10 milioni kwa atakayetoa taarifa kuhusu mauaji ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga. 
“Niwaambie ukweli kuwa katika hili, maneno yatakuwa machache lakini vitendo vitakuwa vingi zaidi,” amesema katika mkutano huo.

Pia IGP Sirro amewatangazia kiama madereva wa bodaboda na kuwataka kuacha kuvunja sheria za barabarani kwa makusudi.

“Huu ni wakati wa kutii utawala wa sheria bila shuruti na nimeshaongea na makamanda wa polisi nchi nzima,” amesema 


==>Msikilize hapo chini akiongea

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni